Mogambi
JF-Expert Member
- May 25, 2012
- 213
- 359
MHESHIMIWA THE DON
DAVID NGOCHO SAMSON
~1~
Geofrey Mtemvu alikulia katika familia yenye uwezo ya Mzee Ally Magubi Mtemvu baada ya wazazi wake kumtelekeza kwa kukosa uwezo wa kumlea. Alichukuliwa na familia ya mzee Ally, akiwa kichanga kabisa pale mama yake mzazi alipomtelekeza mlangoni mwa nyumba ya mzee huyo. Hivyo alikua na kusomeshwa na Mzee Ally hata kufika chuo kikuu. Hakuwahi kufahamu historia hiyo ya kutelekezwa hadi alipomaliza elimu ya chuo kikuu.
Akiwa shule ya sekondari alipata kukutana na binti mmoja aliyejulikana kwa jina la Asha, ambaye alidhani walipendana sana ingawa hawakudumu pamoja, kwa sababu Asha alihamishwa shule na kwenda kusoma huko Arusha.
Kwa kipindi hicho, miaka ya 90 Hadi 2000 mwanzoni, ilikuwa hakuna mawasiliano ya simu za mkononi, njia pekee na rahisi ilikuwa ni kuandikiana barua. Geofrey akawa anatuma barua mara kwa mara lakini hakuwahi kupata majibu kutoka kwa Asha, na hivyo, wakawa wamepotezana kabisa kila mtu akianzisha maisha mapya mbali na mwenzake. Hivyo ndivyo Geofrey alivyoamini. Hata hivyo, hakuvunjika moyo. Aliamini ipo siku wangekutana tena na mpenziwe Asha.
Baada ya kumaliza elimu ya sekondari kidato cha nne alifaulu na kwenda kidato cha tano ambako alijitahidi na kufanikiwa kufaulu kwenda Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Hakuamini macho yake alipomuona Asha. Geof akajua, Mungu alikuwa amewapa nafasi nyingine tena. Akamfuata Asha akiwa mwingi wa bashasha na tabasamu.
Akajaribu kumkumbushia zamani, kwamba daima alikuwa moyoni mwake na alimhitaji sana maishani mwake. Lakini wasemavyo waswahili, asiye bahati habahatiki. Tayari Asha alikuwa na mpenzi mwingine. Hivyo kwa huzuni, Geof alibaki mpweke.
Baada ya chuo kila mtu alitawanyika, na kuanza kuyasaka maisha ambayo yalionekana kuwa magumu licha ya elimu zao za chuo kikuu. Geof alifanikiwa kupata kazi mapema kwani mzee Ally alikuwa na marafiki wengi waliokuwa kwenye vitengo vizuri, na akiwa na digrii ya biashara , Geof aliajiriwa na Shirika la Umeme kama mhasibu jijini Dar es salaam.
Kwa mara ya tatu akawa amekutana na Asha na kwa kipindi hicho Asha alikuwa yuko peke yake, na atafutaye hachoki, Geof alifanikiwa kupata penzi la mwanamke aliyekuwa akimpenda sana, Asha. Geofrey aliamini kuwa walipendana sana. Hakutaka kuchelewesha mambo, akamweleza Asha kuwa alitaka wafunge ndoa mapema ili waishi kama mume na mke.
Hakufurahishwa na wao kuendeleza mahusiano bila ndoa. Asha hakuonekana kuwa na kipingamizi kwa wakati huo, hali hiyo ikampa Geof matumaini kuwa hatimaye angeishi na mwanamke wa ndoto zake. Ilifikia kipindi wakakubaliana kuoana, hatua ya kuanza kuandaa mipango ya kufunga pingu za maisha ili waishi kama mume na mke ikawa wazi.
Mambo yalizidi kupamba moto kuelekea harusi ya wawili hao, lakini kulikuwa na jambo ambalo lilikuwa litokee, jambo hilo lilikuwa moyoni mwa Asha kwa muda mrefu na alikuwa anajitahidi kujinasua lakini likawa linazidi kumshinda.
Historia yake ilichangia kulifanya jambo hilo, kila alipokumbuka limfanye ageuke mnyama, na kumpa taswira mpya kabisa juu ya wanaume. Ukweli ni kwamba, Asha hakuwa na imani na mwanaume. Alikuwa na chuki dhidi ya wanaume, kila siku alijiuliza ni kwa nini wanaume walikuwa laghai.
Hapo awali, Salimu, alikuwa mwanaume aliyekuwa mwanaume wa maisha yake na si Geof. Geof alikuwepo tu kutoa upweke aliokuwa nao, lakini hakuwahi kuingia moyoni mwake japo alijitahidi sana ampende Geof, hata hivyo haikutokea tu. Lakini kwa vile Geof alimpenda, hiyo ilimpa faraja ya kumfanya aonekane miongoni mwa wanawake wenye kupendwa, kwani nani asiyetaka kupendwa? Potelea mbali kupendwa na usiyempenda ilimradi usionekane wewe hupendwi kabisa.
Hiyo ni faraja kubwa, hasa baada ya uliyempenda kukuacha na wewe kujihisi huna thamani na mara tu, mwingine atokee akiwa hanenepi kwa jinsi anavyoelemewa na penzi juu yako! Ni faraja kubwa sana. Lakini pia, alimuonea huruma Geof, mwanaume alikuwa hakati tamaa, alikumbuka harakati zake tangu enzi za sekondari. Alikuwa akimpenda kweli kweli na ilimchukua muda kutamka kile alichokuwa amemwonesha kwa vitendo. Akamtolea nje kiguberi, bila chenga wala soni. Alipomtamkia,
“Sikupendi Geof, sitaki kukutia moyo bure.”
Ni hiyo kumbukumbu iliyomtia huruma walipokutana kwa mara ya tatu akibembeleza pendo. Hilo ndilo lililomuunganisha Asha kwa Geof. Lakini alipokumbuka kwamba alibakia dakika tu kufariki dunia hapo awali, upendo wa Geof kwake ulionekana usanii tupu. Penzi la Asha kwa Salimu lilipotezewa kama ilivyo rahisi kufumba na kufumbua macho. Alimpenda sana mwanaume huyo lakini mwanaume huyo alimwacha katika kipindi kigumu na kwa fedheha kubwa, kitendo kilichosababisha Asha kujinywesha sumu ili ajiue na kuepuka aibu na fedheha ya kuachwa.
Baada ya kupona kifo hicho, alijifunza kitu. Hakukuwa na cha maana kilichokuwa kimtoe uhai, huku mwanaume aliyekuwa afe juu yake akiwa hana habari ya kilichotokea. Mwanaume huyo alimwacha na kumuoa mwanamke mwingine, na hakuwa mwanamke mwingine tu bali rafiki yake mkubwa, waliyesoma na hata kulala pamoja huko chuo kikuu.
Eve!
Eve. Huyo akawa chanzo cha fedheha yake iliiyopelekea kujinywesha sumu, huku yeye akila raha na mwanaume aliyekuwa anampenda. Akamshuhudia kanisani mbele ya askofu wakiwa wanafunga pingu za maisha. Akatamani apae au hata atoweke kama jini, akashindwa na hapo ndipo alipopata wazo la sumu.
Kitendo hicho kiliyabadilisha maisha ya Asha na kumfanya adharau na kupuuza maneno matamu ya wanaume waliomtaka kimapenzi. Alijifunza kwamba, wanaume wote wana uwezo wa kusema maneno hayo. Hata pale Geof aliposema anampenda na alimaanisha, Asha aliitikia tu na kumwambia yeye pia alimpenda sana, lakini asimaanishe hata neno moja. Hakuna neno jipya alilopata kulisema Geof kwa Asha, kwani yote yalisemwa na Salimu hapo awali na matamu zaidi ya hayo.
Hali hiyo ikamjengea usugu moyoni mwake dhidi ya habari za mapenzi. Dhidi ya wanaume. Ikaumba chuki ya Siri dhidi yao, akiwa kila mara akitafakari jinsi gani angelipa kisasi dhidi yao. Hakuona njia nyingine zaidi ya kutumia njia ile ile iliyotumiwa na Salimu. Kukoleza penzi, likishakolea vya kutosha, kulimwaga na kuchukua mpenzi mpya. Akapanga maisha yake yote huo uwe utaratibu wake. Hakujali tena. Kama alionja kifo na kukitema kabla hakijamtenda ubaya, kwa nini wanaume wasikionje? Alijifariji kwa tafakuri hiyo.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
David
0629077792 WhatsApp
DAVID NGOCHO SAMSON
~1~
Geofrey Mtemvu alikulia katika familia yenye uwezo ya Mzee Ally Magubi Mtemvu baada ya wazazi wake kumtelekeza kwa kukosa uwezo wa kumlea. Alichukuliwa na familia ya mzee Ally, akiwa kichanga kabisa pale mama yake mzazi alipomtelekeza mlangoni mwa nyumba ya mzee huyo. Hivyo alikua na kusomeshwa na Mzee Ally hata kufika chuo kikuu. Hakuwahi kufahamu historia hiyo ya kutelekezwa hadi alipomaliza elimu ya chuo kikuu.
Akiwa shule ya sekondari alipata kukutana na binti mmoja aliyejulikana kwa jina la Asha, ambaye alidhani walipendana sana ingawa hawakudumu pamoja, kwa sababu Asha alihamishwa shule na kwenda kusoma huko Arusha.
Kwa kipindi hicho, miaka ya 90 Hadi 2000 mwanzoni, ilikuwa hakuna mawasiliano ya simu za mkononi, njia pekee na rahisi ilikuwa ni kuandikiana barua. Geofrey akawa anatuma barua mara kwa mara lakini hakuwahi kupata majibu kutoka kwa Asha, na hivyo, wakawa wamepotezana kabisa kila mtu akianzisha maisha mapya mbali na mwenzake. Hivyo ndivyo Geofrey alivyoamini. Hata hivyo, hakuvunjika moyo. Aliamini ipo siku wangekutana tena na mpenziwe Asha.
Baada ya kumaliza elimu ya sekondari kidato cha nne alifaulu na kwenda kidato cha tano ambako alijitahidi na kufanikiwa kufaulu kwenda Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Hakuamini macho yake alipomuona Asha. Geof akajua, Mungu alikuwa amewapa nafasi nyingine tena. Akamfuata Asha akiwa mwingi wa bashasha na tabasamu.
Akajaribu kumkumbushia zamani, kwamba daima alikuwa moyoni mwake na alimhitaji sana maishani mwake. Lakini wasemavyo waswahili, asiye bahati habahatiki. Tayari Asha alikuwa na mpenzi mwingine. Hivyo kwa huzuni, Geof alibaki mpweke.
Baada ya chuo kila mtu alitawanyika, na kuanza kuyasaka maisha ambayo yalionekana kuwa magumu licha ya elimu zao za chuo kikuu. Geof alifanikiwa kupata kazi mapema kwani mzee Ally alikuwa na marafiki wengi waliokuwa kwenye vitengo vizuri, na akiwa na digrii ya biashara , Geof aliajiriwa na Shirika la Umeme kama mhasibu jijini Dar es salaam.
Kwa mara ya tatu akawa amekutana na Asha na kwa kipindi hicho Asha alikuwa yuko peke yake, na atafutaye hachoki, Geof alifanikiwa kupata penzi la mwanamke aliyekuwa akimpenda sana, Asha. Geofrey aliamini kuwa walipendana sana. Hakutaka kuchelewesha mambo, akamweleza Asha kuwa alitaka wafunge ndoa mapema ili waishi kama mume na mke.
Hakufurahishwa na wao kuendeleza mahusiano bila ndoa. Asha hakuonekana kuwa na kipingamizi kwa wakati huo, hali hiyo ikampa Geof matumaini kuwa hatimaye angeishi na mwanamke wa ndoto zake. Ilifikia kipindi wakakubaliana kuoana, hatua ya kuanza kuandaa mipango ya kufunga pingu za maisha ili waishi kama mume na mke ikawa wazi.
Mambo yalizidi kupamba moto kuelekea harusi ya wawili hao, lakini kulikuwa na jambo ambalo lilikuwa litokee, jambo hilo lilikuwa moyoni mwa Asha kwa muda mrefu na alikuwa anajitahidi kujinasua lakini likawa linazidi kumshinda.
Historia yake ilichangia kulifanya jambo hilo, kila alipokumbuka limfanye ageuke mnyama, na kumpa taswira mpya kabisa juu ya wanaume. Ukweli ni kwamba, Asha hakuwa na imani na mwanaume. Alikuwa na chuki dhidi ya wanaume, kila siku alijiuliza ni kwa nini wanaume walikuwa laghai.
Hapo awali, Salimu, alikuwa mwanaume aliyekuwa mwanaume wa maisha yake na si Geof. Geof alikuwepo tu kutoa upweke aliokuwa nao, lakini hakuwahi kuingia moyoni mwake japo alijitahidi sana ampende Geof, hata hivyo haikutokea tu. Lakini kwa vile Geof alimpenda, hiyo ilimpa faraja ya kumfanya aonekane miongoni mwa wanawake wenye kupendwa, kwani nani asiyetaka kupendwa? Potelea mbali kupendwa na usiyempenda ilimradi usionekane wewe hupendwi kabisa.
Hiyo ni faraja kubwa, hasa baada ya uliyempenda kukuacha na wewe kujihisi huna thamani na mara tu, mwingine atokee akiwa hanenepi kwa jinsi anavyoelemewa na penzi juu yako! Ni faraja kubwa sana. Lakini pia, alimuonea huruma Geof, mwanaume alikuwa hakati tamaa, alikumbuka harakati zake tangu enzi za sekondari. Alikuwa akimpenda kweli kweli na ilimchukua muda kutamka kile alichokuwa amemwonesha kwa vitendo. Akamtolea nje kiguberi, bila chenga wala soni. Alipomtamkia,
“Sikupendi Geof, sitaki kukutia moyo bure.”
Ni hiyo kumbukumbu iliyomtia huruma walipokutana kwa mara ya tatu akibembeleza pendo. Hilo ndilo lililomuunganisha Asha kwa Geof. Lakini alipokumbuka kwamba alibakia dakika tu kufariki dunia hapo awali, upendo wa Geof kwake ulionekana usanii tupu. Penzi la Asha kwa Salimu lilipotezewa kama ilivyo rahisi kufumba na kufumbua macho. Alimpenda sana mwanaume huyo lakini mwanaume huyo alimwacha katika kipindi kigumu na kwa fedheha kubwa, kitendo kilichosababisha Asha kujinywesha sumu ili ajiue na kuepuka aibu na fedheha ya kuachwa.
Baada ya kupona kifo hicho, alijifunza kitu. Hakukuwa na cha maana kilichokuwa kimtoe uhai, huku mwanaume aliyekuwa afe juu yake akiwa hana habari ya kilichotokea. Mwanaume huyo alimwacha na kumuoa mwanamke mwingine, na hakuwa mwanamke mwingine tu bali rafiki yake mkubwa, waliyesoma na hata kulala pamoja huko chuo kikuu.
Eve!
Eve. Huyo akawa chanzo cha fedheha yake iliiyopelekea kujinywesha sumu, huku yeye akila raha na mwanaume aliyekuwa anampenda. Akamshuhudia kanisani mbele ya askofu wakiwa wanafunga pingu za maisha. Akatamani apae au hata atoweke kama jini, akashindwa na hapo ndipo alipopata wazo la sumu.
Kitendo hicho kiliyabadilisha maisha ya Asha na kumfanya adharau na kupuuza maneno matamu ya wanaume waliomtaka kimapenzi. Alijifunza kwamba, wanaume wote wana uwezo wa kusema maneno hayo. Hata pale Geof aliposema anampenda na alimaanisha, Asha aliitikia tu na kumwambia yeye pia alimpenda sana, lakini asimaanishe hata neno moja. Hakuna neno jipya alilopata kulisema Geof kwa Asha, kwani yote yalisemwa na Salimu hapo awali na matamu zaidi ya hayo.
Hali hiyo ikamjengea usugu moyoni mwake dhidi ya habari za mapenzi. Dhidi ya wanaume. Ikaumba chuki ya Siri dhidi yao, akiwa kila mara akitafakari jinsi gani angelipa kisasi dhidi yao. Hakuona njia nyingine zaidi ya kutumia njia ile ile iliyotumiwa na Salimu. Kukoleza penzi, likishakolea vya kutosha, kulimwaga na kuchukua mpenzi mpya. Akapanga maisha yake yote huo uwe utaratibu wake. Hakujali tena. Kama alionja kifo na kukitema kabla hakijamtenda ubaya, kwa nini wanaume wasikionje? Alijifariji kwa tafakuri hiyo.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
David
0629077792 WhatsApp