Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli something is wrong here!

Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli something is wrong here!

Amiri jeshi mkuu ni mfariji mkuu na kutohudhuria kwake kumewasikitisha wananchi
Mfariji niYesu pekee sio Magufuli.
Just thinking louder;

Huyu Mheshimiwa ni kama ana jambo kama sio mwiko fulani kufika kwenye majanga na msiba mizito;

Lilianza tetemeko la Bukoba, ambapo sio tu hakufika na pia kuhakikisha wahanga wake wanasaidiwa na kuhudumiwa kama wanadamu na kwa mujibu wa utamaduni wetu na utu, lakini alifika baadae sana tena kwenda kugomba na kutoa matamko makali.

Likaja la mauaji mabaya sana ya polisi kule Pwani, lakini akaona kwenda kufungua mabweni ya chuo kikuu Dar-Es-Salaam ndio shughuli muhimu na ya maana sana kuliko kwenda kuaga wapendwa hao na kufariji wafiwa.

Juzi tena likaja la ajali na vifo vya watoto wadogo-wanafunzi wapatao 33 kule Arusha, Inasemekana aliwakilishwa na Makamu! Nashangaa mbona hakuwakilishwa kule Dodoma kupokea taarifa ya veti feki? Lakini Arusha kuna umbali gani kwamba asingeweza kwenda kuaga marehemu na kutoa pole na kisha kurudi Dar? Lakini pia kama kawaida tunaambiwa sehemu kubwa ya rambirambi zimetumika visivyo na yuko kimya! Je anafurahia hilo.
 
Hii ni awamu ya 5!
Hakuna kupetiwapetiwa tena.

"Hapa Kazi Tu, sasa wewe tafuta maana ya hiyo sentensi kadili uwezavyo. ila, "Hapa ni Kazi Tu"
 
Kuna wakati fulani nilikuwa nasikiliza redio moja, nadhani ilikuwa inaitwa 'Kwa Neema FM'. Kulikuwa na mtu mmoja alikuwa akieleza kuwa miaka mingi amefanya kazi ya uganga wa kienyeji. Na uganga wake zaidi ilikuwa kuwafanya wachungaji waweze kutenda miujiza wanapokuwa kwenye makanisa yao.

Akasema aliwahudumia wachungaji wengi sana. Akasema hawezi kuwataja lakini ataeleza ishara ya hao wachungaji. Alitaja ishara kadhaa, sikumbuki zote lakini moja kubwa aliyoitaja na ninayoikumbuka alisema, 'hawawezi kuhudhuria msiba wowote maana ndiyo sharti kubwa alilowapa'. Akasema, wafuatilieni wachungaji, na historia zao. Wapo ambao mtagundua hata siku moja hawajawahi kuhudhuria misiba. Watakwenda kuwatazama wagonjwa, watawaombea, lakini wale wagonjwa wakifariki tu, mchungaji hatafika kwenye matanga wala kwenye maziko.

Akihudhuria tu shughuli yoyote ya msiba, anakuwa amekiuka masharti. Hakusema akihudhuria kutatokea nini.
 


Kuna wakati fulani nilikuwa nasikiliza redio moja, nadhani ilikuwa inaitwa 'Kwa Neema FM'. Kulikuwa na mtu mmoja alikuwa akieleza kuwa miaka mingi amefanya kazi ya uganga wa kienyeji. Na uganga wake zaidi ilikuwa kuwafanya wachungaji waweze kutenda miujiza wanapokuwa kwenye makanisa yao.

Akasema aliwahudumia wachungaji wengi sana. Akasema hawezi kuwataja lakini ataeleza ishara ya hao wachungaji. Alitaja ishara kadhaa, sikumbuki zote lakini moja kubwa aliyoitaja na ninayoikumbuka alisema, 'hawawezi kuhudhuria msiba wowote maana ndiyo sharti kubwa alilowapa'. Akasema, wafuatilieni wachungaji, na historia zao. Wapo ambao mtagundua hata siku moja hawajawahi kuhudhuria misiba. Watakwenda kuwatazama wagonjwa, watawaombea, lakini wale wagonjwa wakifariki tu, mchungaji hatafika kwenye matanga wala kwenye maziko.

Akihudhuria tu shughuli yoyote ya msiba, anakuwa amekiuka masharti. Hakusema akihudhuria kutatokea nini.

Mwenye Macho na afahamu, Roho awaambia Makanisa.
Pia Kwa mtini jifunzeni.
 
Mimi Ukinishauri Ndiyo Umeharibu Kabisa
Makonda Nasema Chapakazi
Mnata Kuingilia Uhuru Wangu ?
Kwani Hata Mimi Mbona Naandikwa Kwenye Mitandao.

Rais Wa Bank Ya Dunia Kaacha Kote Kaja Jiji La Makonda, Tena Rais Wa World Bank Ungekuwa Hujaowa Ningekutafutia Mzaramo Mmoja.

Hayo Aliyazungumza Kwenye Uwekaji Jiwe La Msingi Wa Interchange Pale Ubungo
By Jpm
 
Kupanga ni kuchagua.Kifo kikishatokea kimetokea.La msingi ni kwa kiongozi kukaa na kubuni mikakati ya kuzuia vifo.Usipoangalia unakuwa rais wa kutembelea misiba tu jila siku.Gharama za Rais kutembelea kila msiba ni kubwa mno.
I see!!!!
 
Uraisu ni cheo kigumu sana.. Angeenda wangehoji kwann asingewakilishwa.. Hajaenda wanahoji kwanini hajaenda.. Bora tu uwe raia wa kawaida
Uraisi si cheo kigumu hata kidogo ndio maana hakuna taaluma ya uraisi, bali taasisi hii ya uraisi inaweza kuwa ngumu pale tu Raisi anapotaka kumfurahisha kila mtu au kusikiliza matakwa ya kila mtu miongoni mwa raia wote hapa ndipo mambo yatamuwia ugumu. Rais kuhudhuria au kutohudhuria ktk msiba sio matakwa ya kisheria bali ni TRADITION tu.
 
Msukuma alisema kuwa asilimia kubwa ya wabunge wanapotafuta ubunge hawakosi kwenda kwa waganga wa kienyeji na Kama ilivyokawaida kwa mganga wa kienyeji huwezi ukatoka hivihivi lazima akubebeshe kamzigo,labda na mh wetu siku za kuusaka ukuu huenda ni miongoni mwa wale waliopiga hodi kwa mgaga wa kienyeji.

Na ilivyokawaida kwa mgaga wa kienyeji huwezi ukatoka hivihivi,mwenzetu naye atakuwa alipewa masharti ya kutokuwa wa kwanza kufika kwenye majanga Kama haya,majanga ambayo yanaweza yakawa pia ni kafara kwa waganga wa kienyeji.
 
Back
Top Bottom