Just thinking louder;
Huyu Mheshimiwa ni kama ana jambo kama sio mwiko fulani kufika kwenye majanga na msiba mizito;
Lilianza tetemeko la Bukoba, ambapo sio tu hakufika na pia kuhakikisha wahanga wake wanasaidiwa na kuhudumiwa kama wanadamu na kwa mujibu wa utamaduni wetu na utu, lakini alifika baadae sana tena kwenda kugomba na kutoa matamko makali.
Likaja la mauaji mabaya sana ya polisi kule Pwani, lakini akaona kwenda kufungua mabweni ya chuo kikuu Dar-Es-Salaam ndio shughuli muhimu na ya maana sana kuliko kwenda kuaga wapendwa hao na kufariji wafiwa.
Juzi tena likaja la ajali na vifo vya watoto wadogo-wanafunzi wapatao 33 kule Arusha, Inasemekana aliwakilishwa na Makamu! Nashangaa mbona hakuwakilishwa kule Dodoma kupokea taarifa ya veti feki? Lakini Arusha kuna umbali gani kwamba asingeweza kwenda kuaga marehemu na kutoa pole na kisha kurudi Dar? Lakini pia kama kawaida tunaambiwa sehemu kubwa ya rambirambi zimetumika visivyo na yuko kimya! Je anafurahia hilo.