Mhe. Rais Kikwete na ziara ya Mabwepande

Mhe. Rais Kikwete na ziara ya Mabwepande

Huyu ni kiongozi wa nchi na zaidi ya yote ni mzee hivyo ni kama mzazi huwezi kuleta dharau za kifala,ukileta ujinga wajanja wanang'oa jicho.
 
Huyu si ndiye alisema jk ni dhaifu?

ni kelele hizo za Mnyika ndio zimesababisha Jk aende kimara na sasa hivi maji yameanza kutoka huko baada ya maandamano na kelele nyingi.sasa mlitaka asimpokee wakati yeye ni mbunge?ili iweje?sasa nyie mlitaka amtwange makofi?huyo jk ilikuwa aende kimara siku nyingi lakini akaahirisha.leo kaenda na full band,magari ya washawasha,FFU kibao,utafikiri kaambiwa kimara kuna magaidi wengi!hawa jamaa wanaogopa sana Chadema na ngome zao!
 
Elewa kuwa kazi mojawapo ya upinzani ni kuikosoa serikali, kuielekeza, kutoa maoni na kutoa njia mbadala kwa masuala muhimu. Upinzani sio uadui kama wengine wanavyochukulia. Kuna mambo mengi ambayo upinzani umepigania na kutoa maoni na serikali imeyatekeleza. Lengo ni moja, kuleta maendeleo kwa Watanzania, tatizo ni njia gani itumike kuharakisha lengo hili. kwa bahati mbaya sana nchi yetu haina sera za Kitaifa ambapo kila chama cha siasa kinatakiwa kieleze ni kwa namna gani itatekeleza na wananchi wakiikubali njia hiyo basi watakichagua chama husika. Hali ilivyo hivi sasa ni kubeza, matusi, kejeli na chuki ambavyo mwananchi wa kawaida haimsaidii.

Kwa kumalizia Mhe. Mnyika hana sababu ya kumchukia Rais Kikwete, na akiwa karibu nae basi labda atafanikiwa kwa urahisi sana kutimiza ahadi zake kwa wananchi waliomchagua wala sio kusaliti chama chake. Na hivyo ndivyo inavyoelekea hasa kuhusiana na swala la maji. Si lazima kusubiri mpaka chama chake kiingie madarakani.


Wako wabunge ambao badala ya kupigania maendeleo ya wananchi waliowachagua wanapoteza muda kwa maandamano yasiyo na tija. Kwa mfano kwa nini kung"ang"ania kufanya maandamano kuhusu kushuka kwa Elimu badala ya kukaa na wananchi waliowachagua kupanga mikakati ya kuimarisha elimu katika maeneo yao? Sababu za kushuka elimu ni nyingi, na nyingine ziko ndani ya uwezo wa wapigakura waliowachagua kama vile kuondoa utoro, mimba na ndoa za utotoni kwa hayo kuna haja ya kufanya maandamano? Ni bora kutoa maoni kwa vyombo husika au kamati iliyoteuliwa kuliko kupoteza nguvu kazi kwa kufanya maandamano. Wako watu wachache wanaofikiri kushirikiana na chama tawala ni usaliti. Tuondoe fikra hizi.
 
Hapa JK anamwabia Mnyika, wewe ndie ulieniambia mimi dhaifu...nakuvunja mkono!
 
Asinge msalimia mgepiga kelele kuwa chadema wanapenda shali!
Mnyika ana simamia ukweli kila siku na hato acha!
 
Siasa siyo uadui,japokuwa kigwangalla na bashe walishikana bastola ila ata wao ukiwauliza watakwambia ilikuwa utani tu
 
siasa sio uadui ,sisi sote ni watanzania na nia yetu ni kuleta maendeleo katika taifa letu japo tunatofautina we ccm fisadi mimi mzalendo mpenda maendeleo chadema,wewe unayetaka mnyika na jk wasielewane kisa vyama tofauti utakuwa hujui maana ya siasa, ni lazima utakuwa kati ya maccm (magamba) wanao changanya siasa na vitu vingine kama dini na ukabila.
 
Please go and try somewhere else. Jamii Forums is NOT odinary forum where you can post whatever comes in your medula oblingata.

Please behave.
 
Wataenda mwishowe watarudi maana hawana wa Kumlilia shida zao-Dkt Jakaya november 2010 kwenye Ufunguz wa Bunge la 10.Hapo Mnyika anamsalimia Dkt Jakaya Kikwete yuleyule waliosema hawamtambui,Siasa ni Kama kinyonga Rangi yake inategemea alipo!
 
heshima ni kitu cha bure, hata kama kama ukubalina na mbinu za mtu katika kuliongoza taifa aina maana huwezi kumueshimu kama binadamu mwenzako na wala huwezi mtolea JK nafasi yake ya uraisi. Hivyo anapaswa kumuheshimu kama raia mwenzake na raisi wake.

Ikija bungeni ni vita vingine huko ndio pa kumkosoa na uongozi wake nanilii, hapo nayeye anafanya kazi yake kama mwangalizi wa siasa za ujumla.
 
J4MAYOKA,

Hii thread yako nimegundua mambo mawili,

1. Upeo wako unakuambia siasa ni uadui na vita au kama unatambua hilo, ni kuwa unataka kucheza siasa chafu tu. Kamanda, siasa ni tofauti ya itikadi, mawazo, sera na mengineyo. Hili ni tatizo kwa waTanzania wengi, wanadhani mkiwa vyama tofauti mnakuwa maadui. Hapana, wote ni waTanzania ila mnamitazamo tofauti katika kutatua matatizo. Wanaweza kulia pamoja, kucheka pamoja, kusikitika pamoja na hata kushirikia na katika sherehe na harusi. Sio ugomvi ni tofauti ya ideas

2. Inaonekana umeanzisha thread hii kupotosha na kutaka kufanya propaganda za kuwa chonganisha CHADEMA na Nd. Mnyika. Ushindwe. Hizi ni propaganada zisio na tija na zinaongeza uadui na chuki kwa waTanzania.

Mwisho, tambua kuwa ili kutatua matatizo ya mTanzania ni lazima kuwe na mawazo tofauti na at the end of the day, CHADEMA, CCM, CUF , NCCR, TLP etc lazima wakae kwenye common ground na wafanye kazi pamoja.Hii ni common sense, I know is not common.

By the way, I like the picture. Inaonyesha ukomavu wa kisiasa.
 
hicho kichwa cha mnyika ndio kina mnyima huyu jamaa kikwete usingizi,hapo tz kuna watu wachache sana kama mh john mnyika.....mungu mbariki mh john mnyika
 
Hizi taarabu za kudhani siasa ni mapanga na mangumi peleka kwa kina madelu mchemba na nepi,acheki ukenge masisiem tutawachapa kwa hoja dhidi ya udhAifu wenu na ufisadi wenu....
 
Elewa kuwa kazi mojawapo ya upinzani ni kuikosoa serikali, kuielekeza, kutoa maoni na kutoa njia mbadala kwa masuala muhimu. Upinzani sio uadui kama wengine wanavyochukulia. Kuna mambo mengi ambayo upinzani umepigania na kutoa maoni na serikali imeyatekeleza. Lengo ni moja, kuleta maendeleo kwa Watanzania, tatizo ni njia gani itumike kuharakisha lengo hili. kwa bahati mbaya sana nchi yetu haina sera za Kitaifa ambapo kila chama cha siasa kinatakiwa kieleze ni kwa namna gani itatekeleza na wananchi wakiikubali njia hiyo basi watakichagua chama husika. Hali ilivyo hivi sasa ni kubeza, matusi, kejeli na chuki ambavyo mwananchi wa kawaida haimsaidii.

Kwa kumalizia Mhe. Mnyika hana sababu ya kumchukia Rais Kikwete, na akiwa karibu nae basi labda atafanikiwa kwa urahisi sana kutimiza ahadi zake kwa wananchi waliomchagua wala sio kusaliti chama chake. Na hivyo ndivyo inavyoelekea hasa kuhusiana na swala la maji. Si lazima kusubiri mpaka chama chake kiingie madarakani.


Wako wabunge ambao badala ya kupigania maendeleo ya wananchi waliowachagua wanapoteza muda kwa maandamano yasiyo na tija. Kwa mfano kwa nini kung"ang"ania kufanya maandamano kuhusu kushuka kwa Elimu badala ya kukaa na wananchi waliowachagua kupanga mikakati ya kuimarisha elimu katika maeneo yao? Sababu za kushuka elimu ni nyingi, na nyingine ziko ndani ya uwezo wa wapigakura waliowachagua kama vile kuondoa utoro, mimba na ndoa za utotoni kwa hayo kuna haja ya kufanya maandamano? Ni bora kutoa maoni kwa vyombo husika au kamati iliyoteuliwa kuliko kupoteza nguvu kazi kwa kufanya maandamano. Wako watu wachache wanaofikiri kushirikiana na chama tawala ni usaliti. Tuondoe fikra hizi.
Well said mkuu.

Lakini pia na upande wa pili uangaliwe. Mfano: Wabunge wa upinzani wanapokuwa na hoja binafsi ya kushauri serikali, kwa nini spika au naibu wanataharuki, wakati lengo ni kushauri ili kujenga?
 
Back
Top Bottom