Mhe. Rais Kikwete na ziara ya Mabwepande

Mhe. Rais Kikwete na ziara ya Mabwepande

wakati mwingine natamani nisiitwe Mtanzania kutokana na fikra za baadhi ya wananchi wenzangu. Muda wote tunawaza uhasama, vita, kupandikiziana vitu, visasi. Hivi hatupigi hatua nawambieni. Utakuta hata bungeni mtu anatoa hoja nzuri kwavile ni upinzani watu wazima unaodhani wana heshima zao watazomea, watapiga meza ni karaha tu. Mnyika ulitaka afanye nini hapo? Rais kaja jimboni kwake watu wake wanapata huduma kwa hela ya kodi zetu wote unataka avimbe ili iwe nini? Tubadilike bwana yaani hapa kwetu upinzani utadhani ni uhaini. watu badala ya kufanya shughuli za maendeleo kutwa kucha wanahangaika kudhibitiana. hatufiki popote namna hii.

Pole mtazamo hasi, Mimi nimekua katika jiji la dar es salaam mpaka kumaliza chuo kikuu, tatizo la maji nimekua nalo, muda mrefu Serikali ya chama tawala limefumbia macho suala hili, sasa Ndugu Mnyika amechangia kwa namna moja au nyingine kupata sikio la mkuu wa kaya....hili ni jambo jema kwa wananchi, hii ndiyo sababu ya kuleta mada so Bravo Ndugu Mnyika na hongera kwa Mhe. Raisi
 
Asante na ungana na wewe Bongo lala kuwa siasa siyo uadui mkeshemaliza uchaguzi siku zote kina cho baki ni kufanya kazi na kuijenga nchi hivyo wapinzani katika siasa huwa wanafanya vizuri sana kuiamsha na kuikumbusha serikali kwa wakatio huo juu ya wajibu wao siyo wakumbusha tu bali hata kufuatilia yale waliyo yakumbusha.Ila sema sasa hivi Tanzania viongozi wake wengi wananishangaza sana juu ya utendaji wao wa kazi maana kila mmoja ame kuwa ni mtu wa matamko na kutoa maagizo bila ya kufuatilia maagizo hayo.Pia hapa Tanzania kuna tatizo jingine kubwa mno naweza sema huu ni ugonjwa mwingine.mimi nina uita ugonjwa wa kujisifia serikali ikifanya jambo dogo tu basi hujisifia sana nafikiri tufike mahara ambapo tuyatambue mambo yanayotakiwa serikali kujisifia,mie nita toa mfano mmoja hapa una husu masuala ya ujenzi wa daraja.Tulipo fanikiwa kumaliza ujenzi wa Daraja la rufiji linalo julikana kama Mkapa Bridge Serikali ya Ujerumani ili tufia kwamba Tanzania wamefanikiwa kujenga Dara moja,pia tulipo maliza daraja la Umoja brige lilopo katika kijiji cha mtamba suala waka sema tumejenga daraja la pili.sasa tuna jenga malagalasi nina imani tutakapo kamilisha la kikambondi tuta ambiwa tumejenga la nne.Sasa hapa Wajerumani wa maana gani daraja zote sisi ambazo tuna jisifia tume zijenga na serikali kujisifu sana wenzetu wana ziita ni calvat amboa ni wajibu wa Serikali kujenga bila hata kujisifia.hapa nina maanisha tusipende kujisifia muda wakujisifu kwa tanzania bado sana hivyo niwaombe viongozi wote wa serikali na wa vyama vya siasa tuondoke kwanza kwenye ugonjwa huu,ndiyo maana mpaka leo tunajinadi tuu na kujisifu kuwa Tanzania siyo Maskini wakati tuna umaskini mkubwa mno ila hatujitambui.hasa katika kufanya maamuzi.
 
Je tuwashukuru HOME SHOPPING CENTRE kwa kujenga kituo cha polisi na madarasa ya shule ya msingi huko Mabwepande? Wengine wanasema hakuna haja ya kuwashukuru kwani hizo walizojengea ni fedha zetu za kodi ambazo wanapaswa kulipia kwa makontena wanayoyaingiza kwa mlango wa nyuma bila kuyalipia ushuru kwa kutumia ushawishi wa mtoto wa sultani wetu; yaani mtoto wa sultani wetu ni mbia wa HOME SHOPPING CENTRE ndio maana hawalipi ushuru wa forodha!!
 
Ndio na hajawahi na wala hatakaa aufute usemi huo, hapo mkulu nafikiri alikuwa anampa big up kijana kwa jinsi anavyoipeleka puta serikali yake. Nothing more

Huoni kam'binya mkono kwa nguvu, huenda anamwambia "kijana unatupeleka puta mno, utatuharibia chakula wazee"
Na hilo ndo hasa lilimchekesha Mnyika, sio kwamba anamfurahia jamaa ...
 
Back
Top Bottom