Mhe. Ngeleja, Mzee Rugemalira amekukosea nini hadi 'umhujumu' hivi?

Juhudi za raisi ni kukusanya fedha binafsi za watu? Raisi siyo hakimu. Suala la Ruge liko mahakamani. Mahakaman itaamua kama alikwiba ama ni tuhuma zilizo kwenye msingi sahihi.

Ngereja ni papala siku zote za kufuata vishindo bila tafakuri. Kama Ruge alimpa fedha, na Ruge bila shaka fedha anazonyingi tu nje ya zile za Escrow. Kwa nini ngelezja hataki kuona kwamba fedha alizopewa na Rugemalila hazikutokana na mgao wa Escrow?

Haimpi ufahamu kwamba Ruge angeweza kutoa zawadi kwa marafiski zake kutoka vyanzo vingine zaidi ya Escrow? Nilidhani kitendo cha Ngeleja kisionekane kuwa ni busara ama uzalendo. Kwa mtazano ni kitendo cha hofu inayotokana na ukwlei anaoufahamu juu ya ushiriki wake katika Escrow na hivyo anajua kabisa kwamba ili haikuwa zawadi bali malipo ya biashara haramu.

Kwa nini sherika isimfuate naye kwa ushiriki wake katika mchakato wa wizi wa fedha za umma, ama asikamatwe kwa kuhodhi mali za wizi?

Kama sheria itazingatiwa na haki itendeke, bila shaka Ngeleja na wadau wenzake watamfuata Rege soon ili wajitetee pamoja. Wote ni syndicate ya wizi wa fedha za Escrow.

Sheria imeweka hukumu za wizi siyo tu kwa kuwa wameiba lakini pia ni namna ya kushambulia spirit ya wizi ambayo kama ikibainika kwamba wezi wanarudisha tu mali na kuachwa, bila shaka wengi wataiba sana , watafanya biashara na hizo fedha, watazitumia kwa nman yoyte watakavyo halafu baadaye watazirudisha, na halafu watanzania watafanya maandamano ya kuwapongeza wezi.

Aliyeibiwa aliumizwa kiasi gai?

Ni hasara gani katika maisha wanaipata wale wanaoibiwa?

Tuhalalishe wizi kuwa ni jambo la kawaida hapa nchini?

Halooo!. Ninaogopa.
Word!
 
Ni kawaida marafiki wakiona unapata majanga wanakusaliti na kujiunga na Adui yako.
 
Fact No. 1: Katika urafiki wenu,Mzee Rugemalira alikupa milioni zaidi ya 40 mwaka 2014.

Fact No. 2: Pesa alizokupa Mzee Rugemalira zilitokana na mgawo wake kwenye masuala ya hisa na Escrow kwa ujumla

Fact No. 3: Ni wewe tu ndiye unayeujua ukweli kama ulifahamu chanzo cha fedha ulizopewa na Mzee Ruge au la na mlichozungumza hadi akakupa.

Fact No. 4: Mzee Rugemalira ameshaburuzwa mahakamani kwa mashtaka yahusuyo sakata la Escrow na ameyakana mashtaka yake yote.

Fact No. 5: Kisheria, Mzee Ruge kukana mashtaka ni kuwa na nia na wajibu wa kutetea uhalali wa fedha zake na mgawo wote alioufanya.

Fact No. 6: Kama waliogawiwa,ukiwemo Ngeleja,wanataka kurejesha pesa,wanapaswa kuzirejesha kwa aliyewapa ambaye ni Mzee Ruge ili azitetee pesa zake mahakamani anaposhtakiwa.

Fact No. 7: Kuzirejesha pesa Serikalini ni 'kuchongea' kuwa chanzo hakikuwa halali na hivyo kuweka ukakasi hadi kwenye mashtaka dhidi ya Mzee Ruge.

Kwa urafiki wenu na muda wote uliopita tangu ugawiwe mwaka 2014,kwanini wafanya haya ya marejesho sasa? Huku si 'kumhujumu' Mzee Ruge?


Nini kumuhujumu hata akimfyatua risasi poa tu!
 
Hajamsaliti....isipokuwa amefanya kile nafsi inaona inafaa zaidi kuunga mkono juhudi za Rais kupambana na ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.

Sawa kabisa, angerudisha kwa kwa aliyempa hizo hela kwani si ingeleta maana zaidi. Ana maana gani kurudisha TRA kama sio unafiki?
Kwani si angeenda Mkombozi akaomba account ya Ruge akarudisha kama aivyopewa, kwanini ana rudisha TRA? iwekwe account gani?



From Kibiti
 
Hicho alichokifanya Ngeleja ni unafiki mkubwa

Sent from my itel it1516 Plus using JamiiForums mobile app
 
kwan zile hela zilikua za serikali?????
mbona rais mstaafu alisema zilikua sio za umma lumumba wakapiga makofi ???

Sent from my TECNO-J8 using JamiiForums mobile app
Huwa hawakumbuki kabisa.
 
Labda tungemuuliza Ngeleja alichofanya kisheria ninin?kurejesha fedha ambazo kimsingi kesi inaendelea.!!!

Sent from my TECNO H5 using JamiiForums mobile app
 
Maswali kadhaa ya kujiuliza kuhusu Mh Ngereja kuzirudisha pesa Serikalini badala ya kwa yule aliyempa:

1) Ni kweli alipewa kwa ajili ya maendeleo ya jimbo lake kama mbunge, mwaka 2014?
2) Kati ya mwaka huo 2014 hadi anazirudisha 2017, alikuwa ameziweka tu benki?
3) Kama alipewa kwa ajili ya maendeleo ya jimbo lake, kwa nini hakuzitumia kama ilivyotakiwa?
4) Kwa nini tusiamini kwamba ndizo pesa zilizotumika kumrudisha Bungeni?
5) Hivi ni kweli Mh Mbunge huyo ana pesa nyingi kiasi cha kusamehe 13m alizolipa TRA kama kodi ya kipato hicho?
6) Kama kweli zilikuwa pesa za msaada, kwa Mbunge kuendeleza jimbo, kwa nini alizilipia kodi, kama pato lake binafsi?
7) Je, kama Lugemarila angempa vifaa badala ya pesa, pia angezilipia kodi?
8) Kuna maswali kadhaa yasiyo na majibu kwa sasa.

PAMOJA NA HAYO MH NGEREJA ANASTAHILI KUPONGEZWA KWA KUIFANYA KESI YA ESCROW KUWA RAHISI - SHAHIDI NA 1.
Acha Mkapa atuite WAPUMBAVU tu..
 
Nimeshangaa Sana, alipaswa kuzirejesha kwa Rugemalila
Isitoshe kama alipewa kama mchango kwake yeye kama mbunge ili asaidie huduma za jamii, kwanini mpaka sasa hakuzitumia? na kama alishazitumia hizi katoa kwa mantiki gani? na kwanini kazidisha kwasababu sehemu ya hiyo pesa (30%) alishalipa TRA na kwanini anasema anarudisha pesa wakati anakozipeleka siyo waliompatia? neno 'kurudisha' hapa limekaa kichochezi kwa kesi inayoendelea kwasababu anayetakiwa kurudisha ni James Rugemalila in case akishindwa kesi. Najaribu kujiuliza itakuwaje iwapo Rugemalila atashindwa kesi? atatakiwa kurudisha kiasi gani? je watajumlisha na kiasi alichorudisha Ngeleja?
 
Hajamsaliti....isipokuwa amefanya kile nafsi inaona inafaa zaidi kuunga mkono juhudi za Rais kupambana na ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.
Hivi sheria inasemaje kwa mwenye kukamatwa na kithibiti



From Kibiti
Hi
 
Back
Top Bottom