Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,196
- 25,515
Fact No. 1: Katika urafiki wenu, Mzee Rugemalira alikupa milioni zaidi ya 40 mwaka 2014.
Fact No. 2: Pesa alizokupa Mzee Rugemalira zilitokana na mgawo wake kwenye masuala ya hisa na Escrow kwa ujumla.
Fact No. 3: Ni wewe tu ndiye unayeujua ukweli kama ulifahamu chanzo cha fedha ulizopewa na Mzee Ruge au la na mlichozungumza hadi akakupa.
Fact No. 4: Mzee Rugemalira ameshaburuzwa mahakamani kwa mashtaka yahusuyo sakata la Escrow na ameyakana mashtaka yake yote.
Fact No. 5: Kisheria, Mzee Ruge kukana mashtaka ni kuwa na nia na wajibu wa kutetea uhalali wa fedha zake na mgawo wote alioufanya.
Fact No. 6: Kama waliogawiwa ukiwemo Ngeleja, wanataka kurejesha pesa, wanapaswa kuzirejesha kwa aliyewapa ambaye ni Mzee Ruge ili azitetee pesa zake mahakamani anaposhtakiwa.
Fact No. 7: Kuzirejesha pesa Serikalini ni 'kuchongea' kuwa chanzo hakikuwa halali na hivyo kuweka ukakasi hadi kwenye mashtaka dhidi ya Mzee Ruge.
Kwa urafiki wenu na muda wote uliopita tangu ugawiwe mwaka 2014, kwanini wafanya haya ya marejesho sasa? Huku si 'kumhujumu' Mzee Ruge?
Fact No. 2: Pesa alizokupa Mzee Rugemalira zilitokana na mgawo wake kwenye masuala ya hisa na Escrow kwa ujumla.
Fact No. 3: Ni wewe tu ndiye unayeujua ukweli kama ulifahamu chanzo cha fedha ulizopewa na Mzee Ruge au la na mlichozungumza hadi akakupa.
Fact No. 4: Mzee Rugemalira ameshaburuzwa mahakamani kwa mashtaka yahusuyo sakata la Escrow na ameyakana mashtaka yake yote.
Fact No. 5: Kisheria, Mzee Ruge kukana mashtaka ni kuwa na nia na wajibu wa kutetea uhalali wa fedha zake na mgawo wote alioufanya.
Fact No. 6: Kama waliogawiwa ukiwemo Ngeleja, wanataka kurejesha pesa, wanapaswa kuzirejesha kwa aliyewapa ambaye ni Mzee Ruge ili azitetee pesa zake mahakamani anaposhtakiwa.
Fact No. 7: Kuzirejesha pesa Serikalini ni 'kuchongea' kuwa chanzo hakikuwa halali na hivyo kuweka ukakasi hadi kwenye mashtaka dhidi ya Mzee Ruge.
Kwa urafiki wenu na muda wote uliopita tangu ugawiwe mwaka 2014, kwanini wafanya haya ya marejesho sasa? Huku si 'kumhujumu' Mzee Ruge?