Mhe. Ngeleja, Mzee Rugemalira amekukosea nini hadi 'umhujumu' hivi?

Nafsi yake ina msuta

Sent from my HUAWEI VNS-L31 using JamiiForums mobile app

Nafsi ya Ngeleja sasa ndiyo itamsuta hadi mautini. Hakumfanyia vyema Ruge. Amrudishie Ruge hela yake tena kwa mficho kama alivyopewa kwa mficho.
TRA ndiyo iliyompa hiyo fedha?? Aache utani na fedha ya Ruge. Kama alikuwa anaichukia si amrudishie mwenyewe?? Acheni kumsifu msaka dili. Naamini, hakika kuna kitu Ngeleja anatafuta kwa mkuu nacho sio kingine ila ni kale kanafasi kalikoachwa wazi na Muwongo tu. Kweli, msaka dili hajali hata kumtosa mtu. Ptyuuuuu
 
Unajua ukiwa CCM ata kama wewe ni Prof,ni Dr unashangaa tu akili yako kama uko la pili C refer tu Mwakyembe,uyu nae ngeleja cheki kule ndugai mwenyekiti wao ndo balaa tupu
 
Ushaidi umekamilishwa na Ngeleja, kesi ihukumiwe hatuitaji tarehe isogezwe mbele zaidi
 
Kitendo chake kinaingilia hata kesi iliyoko mahakamani. Hakupaswa kufanya hivo sasa. Angesubiri tu. Afterall wapo waliopewa 1.6Bn fedha za mboga na hawajarudisha

Sent from my SM-A710F using JamiiForums mobile app
 
Zawadi iliyorudi baada ya miaka 3 zawadi gani iyo au ya wizi?Kwani pesa kamrejeshea ruge au TRA? Kwa nn asimrejeshee aliempa?
Kuna kipindi nadhani ilisemwa kwamba bwana Ngeleja alilipa kodi TRA Milioni 13. Ila leo anarudisha zote SERIKALINI. Weird decision. Sijui alipita TRA kukomba zile M13? Harafu eti huyu nae ni Lawyer. Sijui nae ni lawyer msomi?
 
Hata mm sijamuelewa Ngeleja! Ni uoga, unafiki au kujipendekeza?! Anyway majibu yote ni sahihi
 
22844a1bfac2ee29e222783c9b3325fb.jpg

Time will tell!
 
Maswali kadhaa ya kujiuliza kuhusu Mh Ngereja kuzirudisha pesa Serikalini badala ya kwa yule aliyempa:

1) Ni kweli alipewa kwa ajili ya maendeleo ya jimbo lake kama mbunge, mwaka 2014?
2) Kati ya mwaka huo 2014 hadi anazirudisha 2017, alikuwa ameziweka tu benki?
3) Kama alipewa kwa ajili ya maendeleo ya jimbo lake, kwa nini hakuzitumia kama ilivyotakiwa?
4) Kwa nini tusiamini kwamba ndizo pesa zilizotumika kumrudisha Bungeni?
5) Hivi ni kweli Mh Mbunge huyo ana pesa nyingi kiasi cha kusamehe 13m alizolipa TRA kama kodi ya kipato hicho?
6) Kama kweli zilikuwa pesa za msaada, kwa Mbunge kuendeleza jimbo, kwa nini alizilipia kodi, kama pato lake binafsi?
7) Je, kama Lugemarila angempa vifaa badala ya pesa, pia angezilipia kodi?
8) Kuna maswali kadhaa yasiyo na majibu kwa sasa.

PAMOJA NA HAYO MH NGEREJA ANASTAHILI KUPONGEZWA KWA KUIFANYA KESI YA ESCROW KUWA RAHISI - SHAHIDI NA 1.
 
Hyu jamaa sijamuelewa kabisa

Sent from my SM-A7000 using JamiiForums mobile app
 
Huyu Ngereja anafanya danganya toto,ni vile mpinzani wake Tabasamu wa chadema karudi ccm, hivyo amehisi kukatwa na chama kwenye mchujo kuelekea uchaguzi 2020 ndani ya chama chao chini ya mwenyekiti Jpm. Ameona maji yatakuwa marefu kuyavuka kama hatajitahidi kuiondoa hii kashfa, Tabasamu njia itakuwa nyeupe, hivyo Ngereja kaanza kutapatapa mapema kuvuka mto.

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
Hajamsaliti....isipokuwa amefanya kile nafsi inaona inafaa zaidi kuunga mkono juhudi za Rais kupambana na ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.



From Kibiti
Kama Profess Lipumba alivyotoka CUF baada ya ujio wa Lowassa kwenye UKawa
 
Fact No. 1: Katika urafiki wenu,Mzee Rugemalira alikupa milioni zaidi ya 40 mwaka 2014.

Fact No. 2: Pesa alizokupa Mzee Rugemalira zilitokana na mgawo wake kwenye masuala ya hisa na Escrow kwa ujumla

Fact No. 3: Ni wewe tu ndiye unayeujua ukweli kama ulifahamu chanzo cha fedha ulizopewa na Mzee Ruge au la na mlichozungumza hadi akakupa.

Fact No. 4: Mzee Rugemalira ameshaburuzwa mahakamani kwa mashtaka yahusuyo sakata la Escrow na ameyakana mashtaka yake yote.

Fact No. 5: Kisheria, Mzee Ruge kukana mashtaka ni kuwa na nia na wajibu wa kutetea uhalali wa fedha zake na mgawo wote alioufanya.

Fact No. 6: Kama waliogawiwa,ukiwemo Ngeleja,wanataka kurejesha pesa,wanapaswa kuzirejesha kwa aliyewapa ambaye ni Mzee Ruge ili azitetee pesa zake mahakamani anaposhtakiwa.

Fact No. 7: Kuzirejesha pesa Serikalini ni 'kuchongea' kuwa chanzo hakikuwa halali na hivyo kuweka ukakasi hadi kwenye mashtaka dhidi ya Mzee Ruge.

Kwa urafiki wenu na muda wote uliopita tangu ugawiwe mwaka 2014,kwanini wafanya haya ya marejesho sasa? Huku si 'kumhujumu' Mzee Ruge?

MSUKUMA HUYU MSHAMBA Kastuka kuwa katika mabilioni yaliyogawiwa na Rugemalila yeye alipewa hela ya vijimboga.

mshamba hata mapadri wamemzidi kwenye negotiation ya mgao. na alikuwa waziri.

alichofanya ni hasira tu. angepewa bilioni asingerudisha hata harufu yake
 
Ngeleja anatokea ukanda uleeeeeee....maarufu kwa kufoji vyeti.....Mimi sio mwanasheria lakini siwez kufanya "blanda" kubwa hivi kisheria...HUKU NI KUJICHOMA
 
Ngeleja ni mwivi tu km wezi wengine
IPO SIKU HAYA MAIGIZO MNAYOTUFANYIA CHAMA chama cha mapinduzi MTAJUTA.
Nahisi ni Tz pekee sijawahi kuona huu upuuzi kokote Duniani.

Sent from my GT-I9060 using JamiiForums mobile app
Ktk bunge la Uingereza ilitokea ktk miaka 2006 hivi ambapo wabunge walikuwa wanaiibia serikali kwa malipo hewa.

Walipogundulika wengine walifanya kama Ngeleja lkn haikizuia hatua ya mashtaka dhidi yao.

Si tukio geni duniani.

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
 
Hajamsaliti....isipokuwa amefanya kile nafsi inaona inafaa zaidi kuunga mkono juhudi za Rais kupambana na ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.



From Kibiti

Juhudi za raisi ni kukusanya fedha binafsi za watu? Raisi siyo hakimu. Suala la Ruge liko mahakamani. Mahakaman itaamua kama alikwiba ama ni tuhuma zilizo kwenye msingi sahihi.

Ngereja ni papala siku zote za kufuata vishindo bila tafakuri. Kama Ruge alimpa fedha, na Ruge bila shaka fedha anazonyingi tu nje ya zile za Escrow. Kwa nini ngelezja hataki kuona kwamba fedha alizopewa na Rugemalila hazikutokana na mgao wa Escrow?

Haimpi ufahamu kwamba Ruge angeweza kutoa zawadi kwa marafiski zake kutoka vyanzo vingine zaidi ya Escrow? Nilidhani kitendo cha Ngeleja kisionekane kuwa ni busara ama uzalendo. Kwa mtazano ni kitendo cha hofu inayotokana na ukwlei anaoufahamu juu ya ushiriki wake katika Escrow na hivyo anajua kabisa kwamba ili haikuwa zawadi bali malipo ya biashara haramu.

Kwa nini sherika isimfuate naye kwa ushiriki wake katika mchakato wa wizi wa fedha za umma, ama asikamatwe kwa kuhodhi mali za wizi?

Kama sheria itazingatiwa na haki itendeke, bila shaka Ngeleja na wadau wenzake watamfuata Rege soon ili wajitetee pamoja. Wote ni syndicate ya wizi wa fedha za Escrow.

Sheria imeweka hukumu za wizi siyo tu kwa kuwa wameiba lakini pia ni namna ya kushambulia spirit ya wizi ambayo kama ikibainika kwamba wezi wanarudisha tu mali na kuachwa, bila shaka wengi wataiba sana , watafanya biashara na hizo fedha, watazitumia kwa nman yoyte watakavyo halafu baadaye watazirudisha, na halafu watanzania watafanya maandamano ya kuwapongeza wezi.

Aliyeibiwa aliumizwa kiasi gai?

Ni hasara gani katika maisha wanaipata wale wanaoibiwa?

Tuhalalishe wizi kuwa ni jambo la kawaida hapa nchini?

Halooo!. Ninaogopa.
 
Nafsi yake ina msuta

Sent from my HUAWEI VNS-L31 using JamiiForums mobile app
Nafsi inge msuta wakati walivyo muita mbunge binadamu kuwa ni ngedere. Huu ni wizi kama wizi mwingine.
Kwa polisi walio makini na intelijensia Ngeleja hakutakiwa kutoka pale Maelezo aende nyumbani. Bali alitakiwa aeleke Segerea kuunganishwa na Ruge.
Huwezi kukaa na pesa za hongo miaka mitatu ndio ushtuke.
Kipindi cha kuzitetea pale bungeni nae alikuwa mstari wa mbele kusema sio za serekali. Leo anazirudisha serekalini...

Sent from my Phantom6 using JamiiForums mobile app
 
Ngeleja hajielewi, hana tofauti na mwenyekiti wake!
Hawa ndiyo watu tunaowapigia kura halafu tunaamini watatuletea maendeleo hata hesabu za logic za darasa la 5 hawajui.Anawarudishia TRA ndio waliompa?Mwenyekiti kawaambukiza kufanya mambo bila utaratibu hata kwa mambo ambayo hayahitaji hata nguvu.Hizi kiki za kijinga hazita waacha salama.
 
Back
Top Bottom