Mbowe ambana Waziri Mkuu atoe kauli juu ya masuala yanayokwaza demokrasia na utawala bora

Pendeni kuwa wakweli, tena napenda kutoa wito kwa Watanzania wote tuwe tunatafakari kwa kina na kujadili, pamoja na kupima mambo. Mimi ningependa watu watakao ingia kwenye siasa waingie kufuatana na hisia zao pamoja na msukumo wao wa kisiasa na si kwa ukanda wao. Hatuwezi kujenga nchi kwa kuacha watu ambao ni wazoefu au wanauwezo fulani eti kwa sababu ni wa kanda fulani, pia hatuwezi kuacha kutumia watu waliokomaa kisiasa na waadilifu halafu tukachukua watu ambao bado hawajakomaa kisiasa baadae zikatoka kauli za kukidhoofisha chama halafu tuseme eti itifaki ya ukanda ilizingatiwa.

Ili mafanikio yapatikane ni lazima kuwe na watu ambao wana hofu ya Mungu, wachapa kazi, waadilifu na wazalendo hivyo itakuwa rahisi kwa watu wa namna hii kupigania ukweli, na si vinginevyo.

kama mkutano umefanyika na watu waliopatikana kwa siku hiyo ndio hao, pengine wengine walishindwa kufika hakuna tatizo, na pengine hao waliokuwepo hawakuwa wamejiandaa sasa utalazimisha mtu azungumze.

tusipende kutumika na chama cha ccm kwa kuleta mijadala ambayo haina mantiki, nchi inaisha huku tunatumia sababu ambazo hazina msingi kuchafua chadema. Tulete hoja zenye mashiko mwisho wa siku wangezungumza watu mbalimbali mngesema waislamu walikuwa wengi kuliko wakristo au wakristo mbona walikuwa wengi kuliko waislamu.

Mtu anapojiunga na chama huwa akubaliwi au akataliwi kwa sababu ya kabila lake au dini yake bali kwa sababu ya utashi wake yeye mwenyewe na ana haki zote za kugombea nafasi za chama na kuwa kiongozi hivyo vvyote vinapatikana kulingana na sifra za mgombea huyo na si vinginevyo. sasa mnataka mtu akiwa anafaa akataliwe kwa sababu ya ukanda, huu ndio utakuwa ubaguzi.

wewe ni kijana wa chadema uko pale makao makuu mnapewa posho kwa ajili ya kuficha maovu ya chadema na kuisema vibaya CCM na Serikali yake ili kuijenga chadema kisiasa na kuidhohofisha CCM,ukweli ni kwamba chadema ni chama cha kidini na ukabila , hawafahi kupewa madaraka ya kuongoza nchi!
 
Mfa maji haishi tapatapa, hutafuta kila pa kushika hapaoni. CHADEMA chama cha watanzania na vijana wote tutaiondoa CCm 2015. Naomba tuendlee na maandalizi haya kwa kasi bila kukoma.

Huyu mleta mada inaonekana ni miongoni mwa watu waliohudhuria mkutano huo na kunyimwa fursa ya kuzungumza kwa sababu hana wadhifa wowote ndani ya chama na ndio maana analalamika hivyo.

Pili , kuhusu mafunzo kwa madiwani ni kweli yalifanyika kwa madiwani wote wa nchi nzima 578 na yaliendeshwa kwa kanda tatu tofauti, moja ilikuwa na wakufunzi wafuatao, Silivester Masinde, Antony Komu, Josephat Isango,Alex Kasurura ,Kunty ....nyingine ilikuwa na Benson Kigaila,Lazaro Maasay,Jaffar Michael,na wengine na ya tatu ilikuwa na Nyangaki Shilungushela,John Mrema,Shaba, Basil Lema ,Anna Mghwira, Dadi Kombo .

Sasa huyu yeye anapaswa kufanya utafiti kuwa hao watu walitokea kanda gani na wengine walienda kwa sababu ya nafasi zao kwenye chama .

huyu inawezekana ni msaidizi wa Tuntemeke.......
 
Binafsi nawalaumu sana viongozi wa ccm na naamini wataingia kwenye historia mbaya siku itakapo tokea nchi yetu ikiingia kwenye machafuko makubwa ya udini au ukanda ambao tayari dalili na viashiria vimeanza kujionyesha.

1. Walikisakama kwa propaganda chafu Cuf kilipokuwa na nguvu na kukiita chama cha udini wakimaanisha waislamu lakini viongozi wa ccm hawakuwekwa wazi kuwa wao ni dini gani.

2. Cuf kilipo poteza mvuto wakaanza kukisakama chadema kuwa ni chama cha kikanda, kikabila na chama cha wakristo. Hapa tena hawakusema kuwa wao ni dini gani.

Wamefanikiwa kuwagawa watanzania huku na sisi tukiwa tumeachwa njia panda tusielewe kuwa wale waliosema vyama vile nivya kikanda, kikabila au kidini wanao tuhumu ni dini gani au wa ukanda gani? Tuwaogope.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mimi siamini kama cdm ni chama cha ukanda,udini au ubaguzi wa aina yoyote ile.kingekuwa hivyo hata baraza kivuli la mawaziri lingelenga kwenye ukanda huohuo lakini karibu mikoa yote yenye wabunge wa cdm wapepata.mingine zaidi ya mmoja km mbeya,dsmkwa mtoa hoja,singida,mwanza n.k.mikoa ambayo ni mbali kabisa na kanda ya kasikazini.ila ninacho weza kusema ni kwamba.mkono mtupu haulambwi,palipo na tai wengi ujuwe pana mzoga.uzushi wote wanaozushiwa cdm siyo bure kuna kitu kipo na kitu chenyewe ni ukombozi.haya yote ni mapito hakuna kitu cha bwerere.nauona ukombozi uleeeeee unaletwa na cdm.

kwani umeshawai kumuona makamu mwenyekiti wa chadema taifa mzee said arfi mbunge wa mpanda kati anahusishwa na chadema?hivi hujui ni kwa nini wanamtenga katika siasa zao usilo lijua ni sawa na usiku wa giza kuna kitu nyuma ya pazia usichokijua.

hakuna ukombozi kwa siasa za ukanda ndo maana joshua nasari alisema atakuwa rais wa kaskazini na lema ndio waziri mkuu wake.sasa unasema baraza kivuli kwani ni wakaskazini wangapi wameachwa kwenye baraza hilo hivi unazani kungekuwa na wabunge wa kutosha kuunda baraza kutoka kaskazini hao unaowaona kutoka pande zingine wangepata?

kuna watu kama shibuda hawawezi kupata maana wanawajua sana wakina mbowe na unafiki wao ndo maana leo wanapinga posho huku haohao ndo wakwanza kuchukua na kusema kwamba wanawekewa mbona zitto hawekewi? au yeye si mbunge?
 
Nakubaliana na wewe kiasi: Kenye point ya kwanza, binafsi ningetaka tuachane na huu mkorogo wa wanasiasa kuhutubia makanisani au misikitini.

Waje kama waumini na waondoke. Mkandara huu mwanya unaanza kuleta shida maana watu wanautumia kuunda mtandao na tunajua mambo ya mitandao ndiyo yaliyofikisha hii nchi kibla. Raia wana dini -fine, lakini mwanasiasa ukumbi wake uwe mbali kabisa na sehemu ya kuabudu. aje asali. basi.

Kwenye point ya pili, pia nakubadiliana na wewe. Kama taifa tufike mahali sasa tuwe na defination yetu sisi watanzania juu ya serikali kutokuwa na dini. Hapa naamanisha tu-define serikali kutokuwa na deni kwa mazingira yetu sisi. Shule zilizo chini ya madhehebu ya dini ziwe ni 'private school. Watoto wanaotoka kwenye familia ambazo hazina kipato lakini wanataka kujiunga na hizi shule basi serikali iweke mfumo wa kutoa financial assistance kwenye specific school on behalf ya hawa watoto.

Na kama issue itakuwa ni kutoa ruzuku (MOU kama ilivyo sasa) basi ili kuondoa zogo, ama serikali ifute kabisa au serikali iweke wazi ni maeneo gani itatoa subsidies (list) na hivyo dhehebu linalotaka kupata msaada wanatakiwa kufanya nini.

Hii itaondoa malumbano yasiyoisha. Iseme tu tunafuta au kuanzia sasa tutatoa assistance kwa taasisi ya dini i.e inayolima mahindi, au inayotoa matibabu, au inayofagia barabara etc etc ili kila mtu ajue ni mambo gani yanakuwa funded.

Mkuu wangu swlaa la MoU sio ruzuku peke yake bali ukiusoma unajiekleza wazi kwamba ndio kitakuwa chombo kinachoshughulikiwa ELIMU a AFYA nchini. Hizi ruzuku zinakuja tu ktk utekelezaji wa kazi walizopewa na ndio maana unakuta shule ya kanisa lakini watoto wanalipia kama private scholl.

Shule ya Filbert Bay, au Hospital ya Kariuki hawapewi ruzuku hizi isipokuwa za kanisa na ndio maana kuna walimu wa serikali ktk shule sehemu hizo.

Ni muhimu sana kufikiria jinsi Watnzania wanavyofikiria. Sisi ni wanafiki na Matapeli kiasili ukiwapa mwanya dini zao zzinakuwa sababu ya kutumia mianya hiyo. Tumeona vifaa vya Ujenzi vikiingizwa na vyombo vya dini na NGOs kwa ajili ya biashara zao nje kabisa ya malengo ya vyombo hivi.

Nakumbuka mwaka 2009 JK aliondoa kabisa exemption ya tax ktk baadhi ya secta lakini akaacha Matapeli wakubwa wakiendelea kupokea incentive hizi. How can a Preacher become a millionaire? ajenge majumba ya kukodisha hizo fedha kazipata wapi?

Dawa ni kukata kabisa mirija hii yote bila upendeleo wala kuhofia mtu maana dini ni imani ya mtu haina kabisa mahusiano kisiasa isipokuwa ku eliminate imani nyinginezo - Uwanja huo tumeweza kuukemea na tumeacha riuksa ya kila mtu kuabudu kile atakacho kiamini. Dini ktk siasa inaweza kabisa kuua haki na uhuru wa mwananchi kuabudu dini aitakayo.

Kama ulivyosema, shule za makanisa na sijui Bakwata kama zitakuwepo basi wafungue wenyewe na waziendeshe wenyewe bila serikali kuwaingilia isipokuwa ktk mfumo wa elimu yenyewe maana mtihani utakuwa mmoja kama ilivyokuwa zamani au wakati wa mkoloni.

Na serikali itaweza kulipia tu mtoto anayekwenda kusoma ktk shule hizi kama inavyolipia watoto ktk sponsorship nyinginezo wakati huo huo ikijiimarisha ktk shule zake. Kiujumla muafaka wa MoU ndio mbegu ilipandikiza Udini nchini, isipokuwa kwa unafiki wetu hatutaki kuamini kutokana na Udini ulkwisha ota ktk mioyo yetu.

Sikuwahi kusikia Udini wakati wa Nyerere hata mitaani, majumbani watu tulipendana pasipo kujali dini za mtu lakini sio leo hii. Tokea 1992 wakati wa Mwinyi ndio tuliona hata waislaam wenyewe wakiishinikiza Bakwata kuvunjwa ikawa ya kutukana imani nyinginezo, ustaarabu wote ukaisha na mwanzo wa kila mtu kujitazama kwa dini yake.
 
Mkuu Molemo sometimes huwa unaandika vitu ambavyo vinakiletea chama taswira mbaya.Deal with this dog safely...!
 
Mkuu nakuhakikishia mwisho wa Tuntemeke umefika.Nilishauri asifukuzwe tangu kipindi kile alivyoanza uasi chamani kwa sababu nilijua mwaka huu tunaanza kupanga safu mpya za uongozi CDM na nakuhakikishia huyu Tuntemeke hatapata hata kazi ya kumfungulia Dr Slaa milango ya gari.Nimhakikishie tu huyu Tuntemeke kuwa Mbowe atachaguliwa tena kwa kishindo kuwa Mkiti wa Chama na Dr Slaa atapitishwa kwa kishindo kuwa Katibu mkuu tena.Halafu 2015 Tuntemeke akiwa hai atashuhudia Dr Slaa akila kiapo cha kuwa Rais wa nchi hii....Tuntemeke ajinyonge kama hapendi kushuhudia haya.

kijana hilo sahau haitotokea kamwe kama uamini subiri utajua ukweli wa yote,nafikiri wewe ni mchanga sana kisiasa ndiyo maana wanena hivyo,Posho unayopewa na chadema ili kuinenea mazuri itakutafuna!
 
Kama ulivyosema, shule za makanisa na sijui Bakwata kama zitakuwepo basi wafungue wenyewe na waziendeshe wenyewe bila serikali kuwaingilia isipokuwa ktk mfumo wa elimu yenyewe maana mtihani utakuwa mmoja kama ilivyokuwazamani au wakati wa mkoloni. Na serikali itaweza kulipia tu mtoto anayekwenda kusoma ktk shule hizi kama inanavyolipia ktk sponsorship nyinginezo wakati huo huo ikijiimarisha ktk shule zake. Kiujumla muafaka wa MoU ndio mbegu ilipandikiza Udini nchini, isipokuwa kwa unafiki wetu hatutaki kuamini kutokana na Udini ulkwisha ota ktk mioyo yetu. Sikuwahi kusikia Udini wakati wa Nyerere hata mitaani, majumbani watu tulipendana pasipo kujali dini za mtu lakini sio leo hii. Tokea 1992 wakati wa Mwinyi ndio tuliona hata waislaam wenyewe wakiishinikiza Bakwata kuvunjwa ikawa ya kutukana imani nyinginezo, ustaarabu wote ukaisha na mwanzo wa kila mtu kujitazama kwa dini yake.


Tangu huo mwaka ulioutaja hii nchi imekuwa kama kichwa cha mwendawazimu. Sifahamu wakubwa wataziba masikio na kufumba macho mpaka lini lakini kama hatukukaa chini na kujipa miongozo kama taifa basi tuna shida huko mbele.

Kuna jambo umegusia kuhusu wahubiri kuwa matajiri haraka. Kwangu mimi hapa kuna biashara nzuri sana, tax-free business. Maana mtu na kikanisha chake anakigeuza kuwa kama duka vile hakuna cha TRA wala jirani yake na TRA. Na mbaya waumini hawawezi kusema sana maana 'mtumishi wa mungu.

Kenya sasa hivi wanajadili kitu kimoja cha maana sana. Wanaangalia ni mambo gani/miradi gani ya kidini ambayo itapata msamaha wa kodi na ipi isipate. Sasa madhebu karibu yote (kama si yote) yanajihusisha na miradi mingi ya kibiashara, lazima tuwe na list ya mambo ya kusamehe kodi na sio kuacha mianya ya watu kujitajirisha.
 
Huko tunakoelekea sio salama kabisa hasa kama tuna watu kama Nape wanaongea bila kufikiri madhara ya matamshi yao. Kama viongozi wa nchi wana nia ya dhati ya kunusuru taifa hili na mipasuko ya kidini, ukanda, ukabila ningeshauri yafuatayo wenyeviti na makatibu wa vyama vyote vya siasa vyenye usajili wa kudumu wakutane na kuweka framework/miongozo kuhusu yafuatayo:

1. Iwe ni marufuku kwa mwanasiasa yoyote kujiingiza kwenye shughuli za kidini. Hakuna mambo ya harambee, wala kusalimia waumini, au kiongozi wa kisiasa (including rais) kuwa mgeni rasmi kwenye shughuli za dini. Kama anaenda kwenye ibada aende kama mtu wa kawaida na sio vinginevyo.

2. Tuondoe mambo yote yanayohusu dini kwenye elimu, kuanzia vitabu vilivyoandaliwa kwa misingi ya dini. Somo la dini liwe ni suala la mtu binafsi hivyo lisiwe chini ya NECTA. Dini na mambo yote yanagusa dini yawe mambo binafsi.

3. Wanasiasa wakubaliane mambo ambayo ni muhimu kwa umoja wa taifa hivyo kuachana na kauli za kugawa watanzani. Hapa ningeomba nimtaje Nape maana ameonesha kupenda siasa za kugawa watu.

Nchi yoyote iliyostaarabika huwa wanakubaliana mambo muhimu yanatakiwa kuzingatiwa na wanasiasa wote.

4. Tuondoe vile vile memorandum zozote (MOU) zinahusisha taasisi za dini na serikali na kuanza kuwadai waliokuwa wakipewa waturudishie pesa kidogo kidogo walizochukua kutoka kwenye kodi zetu.

5. Tuwe na sheria inayopiga marufuku kwa taasisi ya kidini kujihusisha na shughuli inawakilisha majukumu ya serikali. Taasisi za kidini zikitaka zijiendeshe kifaida kama taasisi binafsi.

Yakiwa hayo FJM nakuunga mkono sanaaa ndugu yangu.!!!
 
Chadema mwendo mdundo hizo ni mbinu ambazo zinatumiwa na magamba ili kukivuruga chama but wameshidwa! watanzania wanashuhudia mambo mazuri yanayofanywa na cdm kwa lengn la kuikomboa nchi yetu kutokana na ubovu wa utawaa uliopo
 
Tangu huo mwaka ulioutaja hii nchi imekuwa kama kichwa cha mwendawazimu. Sifahamu wakubwa wataziba masikio na kufumba macho mpaka lini lakini kama hatukukaa chini na kujipa miongozo kama taifa basi tuna shida huko mbele.

Kuna jambo umegusia kuhusu wahubiri kuwa matajiri haraka. Kwangu mimi hapa kuna biashara nzuri sana, tax-free business. Maana mtu na kikanisha chake anakigeuza kuwa kama duka vile hakuna cha TRA wala jirani yake na TRA. Na mbaya waumini hawawezi kusema sana maana 'mtumishi wa mungu.

Kenya sasa hivi wanajadili kitu kimoja cha maana sana. Wanaangalia ni mambo gani/miradi gani ya kidini ambayo itapata msamaha wa kodi na ipi isipate. Sasa madhebu karibu yote (kama si yote) yanajihusisha na miradi mingi ya kibiashara, lazima tuwe na list ya mambo ya kusamehe kodi na sio kuacha mianya ya watu kujitajirisha.
Kuhusu swala la kutoa tax exemption hili mkuu wangu ni kuondoa kabisa lisiwepo iwe hata kwa viongozi maana sisi wote ni wamoja wenye kufikiria sawa isipokuwa tumezidiana ujanja tu. Sasa ktk ufanya hivyo, ili kutopoteza wawekezaji ni swala la kupunguza corporate tax. Huu ndio mpango mzima maana mashirika yoyote yanayotaka kuwekeza nchi maskini hutazama kwanza kiwango cha corporate tax tukiacha usalama na policies zake ktk ushindani.

Hizi exemption ni miaya ya wezi kutumia nafasi hizi kujitajirisha pasipo kulipa kodi wakati ni kodi hizi ndizo zitajenga shule, Hospital na mengineyo. Weka kodi ndogo ya corporate kwa kutazama Kenya, Uganda na nchi jirani yetu ili tuwe competitive na sio kuewezesha matapeli.

Ni vizuri kuwasoma Watanzania (WATU) ktk mazingira yetu hakuna dawa maana utakao waachia ndio wao wata monopolize uingizaji wa vitu vilevile ambavyo walitakiwa wananchi kulipia tax. Kuna viongozi leo hii ukiwakatia kitu wanaingiza gari lako kwa exemption, kuna Mapadri na Masheik ukiwakatia kitu utaingia hata ndege bila ushuru! Dawa ni kukata exemption kabisa lakini kodi iwe ndogo.. wingi wa watu kuingiza mali nchini itatuletea hesabu kubwa zaidi ya hii tunayoipata leo.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Habar wakuu!
Kutokana na vuguvugu la udini ambalo linazidi kusambazwa na baadhi ya viongozi wa kidini hapa nchini pamoja na vyombo vya habari, mhe Mbowe amesema haya yote yanatokana kutokana na serkali dhaifu ambayo inashindwa kukemea mambo kama hayo ambayo madhara yake ni makubwa kwa nchi pia amekemea vikali tabia ya viongozi wa CCM kuwagawa watu kidni na kiukanda na kikabila kwa maslahi mafupi ya chama chao.

Source Mbowe mwenye kwenye hotuba yake bungeni.


Mbowe na spin offs Waislamu bado wanasubiria kauli yake kuhusu msimamo wa Chadema na kanisa ni upi? au anajishaua na sintofahamu? Sema baba tunakusikia kamanda!!!!
 
Mbowe na spin offs Waislamu bado wanasubiria kauli yake kuhusu msimamo wa Chadema na kanisa ni upi? au anajishaua na sintofahamu? Sema baba tunakusikia kamanda!!!!

Kwanini msimamo wa CHADEMA na kanisa? Kuna nini hapo?
 
Binafsi nawalaumu sana viongozi wa ccm na naamini wataingia kwenye historia mbaya siku itakapo tokea nchi yetu ikiingia kwenye machafuko makubwa ya udini au ukanda ambao tayari dalili na viashiria vimeanza kujionyesha.

1. Walikisakama kwa propaganda chafu Cuf kilipokuwa na nguvu na kukiita chama cha udini wakimaanisha waislamu lakini viongozi wa ccm hawakuwekwa wazi kuwa wao ni dini gani.

2. Cuf kilipo poteza mvuto wakaanza kukisakama chadema kuwa ni chama cha kikanda, kikabila na chama cha wakristo. Hapa tena hawakusema kuwa wao ni dini gani.

Wamefanikiwa kuwagawa watanzania huku na sisi tukiwa tumeachwa njia panda tusielewe kuwa wale waliosema vyama vile nivya kikanda, kikabila au kidini wanao tuhumu ni dini gani au wa ukanda gani? Tuwaogope.

Mohamed, mara nyingi machafuko kwenye baadhi ya nchi yameletwa na wale walio madarakani hasa pale wanapoona hawana mvuto kwa umma. Wakati wa uchaguzi mdogo Igunda Mukama alidiriki kufanya press conference na kusema kuwa CHADEMA wameleta makomandoo toka Libya na Pakistan. Sasa hivi Mukama na Nape wamekuwa wanahubiri Ukabila na ukanda. Mambo ya sera au hoja za msingi hakuna, wanaona sasa wagawe watu ili waendelee kuponda maisha.

Huu ni msiba wa taifa maana sikutegemea kabisa mtu kama Mukama kufanya siasa za maji taka kama ambavyo anafanya. Nilidhani ni kwa watu ambao hawajaenda shule kumbe wapi. Lakini mbaya zaidi CC na hata NEC ya CCM walipokutana hawakukemea hili jambo! Ina maana wamebariki siasa za chuki? Unforgivable.
 
bado mbowe alikuwa smart, kwa chama kilichochafuliwa na propaganda za udini za ccm.Na tayari waislam wengi hata humu ndani tayari wapo biased(wameharibiwa akili na ccm).Timing was everything.

Ni wazi kuwa ukiwauliza waislam mauaji waliyokuwa yanawakuta km yalitokana na CDM hawana majibu. Hata mwanama wa cdm aliyefia igunga alikuwa muislam na shujaa wa cdm kwa vile alikuwa na imani na chama na Mbowe kalitaja hilo.

Ni wazi ukiwauliza CUF wamewaenzi mara ngapi wale jamaa waliokufa na kusahaulika ktk mission duni za cuf, majibu hayatakuwa mazuri sana.
Mbole kalisema vyema na kafanya tuming nzuri, kila mtu alitulia na kusikiliza, hapakuwa na kuleta malumbano.

Na ujumbe umefika kwa watanzania wote,kazi kwao kutafakari.
 
Mbowe ambana Pinda polisi kuua raia

Kambi ya Upinzani bungeni imeitaka serikali kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ahadi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuchunguza vifo vya raia vilivyotokea mikononi mwa askari polisi au vyombo vya dola. Julai mwaka jana, Pinda aliahidi kwamba serikali ingechunguza vifo hivyo kwa kutumia sheria ya Inquest kuchunguza mauaji ya raia wakiwa mikononi mwa vyombo vya dola.

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe, akitoa maoni ya upinzani kuhusu makadirio ya Ofisi Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha wa 2012/13 alisema pamoja na ahadi hiyo, bado kumekuwepo na mauaji ya kutisha na ya kikatili kwa raia wakiwa mikononi mwa polisi. Alisema taarifa ya Haki za Binadamu na Utawala Bora zinaonyesha kwamba vifo hivyo vimekuwa vikiongezeka kila mwaka na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa.

Ni muhimu tukatambua kuwa kila kifo cha mtu ni tofauti na cha mwingine, na hutokea katika mazingira tofauti. Hivyo, kwa kuzingatia kilio cha wananchi ambao Serikali ina wajibu wa kuwalinda, vifo vyote ambavyo vimetokea kwa sababu ya matumizi ya nguvu, kikiwamo kifo cha raia kilichotokea akiwa chini ya uangalizi wa vyombo vya dola, ni vema serikali ikazingatia mazingira husika, alisema.

Alisema taarifa ya haki za binadamu ya mwaka jana inaeleza kwamba kuanzia Januari hadi Desemba 2011, takribani watu 25 wamefariki wakiwa mikononi mwa polisi na maafisa wengine wa ulinzi na matukio mengine yakiwaacha zaidi ya watu 50 na majeraha.

Alikumbusha kwamba ripoti hizo zinaonyesha mauaji ya raia mikononi mwa polisi yameendelea kuongezeka ambapo watu watano walifia mikononi mwa polisi mwaka 2008, watu 15 mwaka 2009 hadi watu 52 mwaka 2010 na katika kipindi cha Januari hadi Mei mwaka jana, watu 9 walikuwa wameripotiwa kuuawa katika eneo la Nyamongo, Tarime mkoani Mara.

Kambi ya Upinzani tunatambua kuwa taarifa hizi za mauaji zinawagusa askari Polisi pia kwa kuwa kwa mwaka uliopita katika maeneo ya Tarime, Tabora, Shinyanga, Arusha na Rukwa polisi watano waliuawa na wananchitunaamini kuwa kuacha kuchukua hatua dhidi ya polisi wachache wanaolichafua jeshi la polisi kwa ujumla inasababisha picha mbaya ya taifa letu kitaifa na kimataifa, alisema Mbowe.

Mbowe ambaye ni mbunge wa Hai (Chadema), alizungumzia pia unyanyasaji wa kisiasa unaowakuta wafuasi na viongozi wa vyama vya upinzani akieleza kwamba matukio hayo yamekuwa yakidhihirika zaidi kwenye chaguzi ndogo za madiwani, ubunge au vijiji na vitongoji hapa.

Alitolea mfano kujeruhiwa kwa wabunge wa Chadema wakati wa uchaguzi mdogo wa madiwani jijini Mwanza, Aprili mwaka huu (Highness Kiwia- Ilemelela na Salvatory Machemli- Ukerewe) walikatwa mapanga wakati wa uchaguzi mdogo wa Udiwani wa Kata ya Kirumba na wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Alisema polisi wakishindwa kuzuia tukio hilo pamoja na kuwa walifika katika eneo la tukio tena wakiwa na silaha.

Manyanyaso haya hayawezi kuvumiliwa tena ni lazima kama taifa tujue kuwa nchi hii ni ya vyama vingi vya siasa na hivyo kila raia ana haki ya kujiunga na chama chochote cha siasa bila shinikizo. Hii ni kwa sababu bado mikutano ya kisiasa na hata mikutano ya waheshimiwa wabunge wa upinzani inavamiwa mara kwa mara mathalani uvamizi aliofanyiwa Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, alisema Mbowe.

SHEREHE ZA UHURU, TAIFA
Akizungumzia maadhimisho mbalimbali, alisema siyo lazima sherehe zote zifanyike kila mwaka kwa kuwa zinatumia fedha nyingi bila tija huku akiitaka Serikali iweke wazi kiasi cha fedha kilichotumika kwenye maadhimisho ya Jubilee ya miaka 50 tangu Tanganyika ipate uhuru. Alisema gazeti moja liliripoti kwamba katika maadhimisho hayo, serikali ilitumia Sh. bilioni 64; taarifa ambazo hazikuwahi kukanushwa na serikali.

Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali itoe tamko kuhusu matumizi hayo pamoja na mchanganuo wake ili kutekeleza dhana nzima ya uwazi na ukwelitaarifa za gharama za sherehe hizi za Kitaifa zikawekwa hadharani, zikiwemo gharama za mbio za mwenge ili umma wa Watanzania waweze kuchambua na kuona kama kweli bado ni tija na kipaumbele kwa Taifa kuendeleza sherehe hizi kwa mfumo tulio nao leo, alisema.

Alizungumzia tatizo la chaguzi nchini na kusema kuwa kumekuwa na ushahidi kuwa watendaji wa serikali wamekuwa wakiingilia mchakato huo kwa faida ya chama tawala.

Alinukuu barua ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, B.B Kichinda, ya Mei 23, mwaka huu yenye Kumb. Na FA.291/300/08/25 kwenda kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya na nakala zake kusambazwa kwa wakuu wote wa Wilaya za Mkoa wa Mara, iliyoeleza "Yah: Kusimamisha uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji katika mamlaka za serikali za mitaa"

Alisema katika barua hiyo, Kichinda aliwaelekeza watendaji hao kwamba chaguzi hizo zinasimamishwa ili kupisha uchaguzi wa CCM.

"Kwa barua hii ni dhahiri kuwa Katibu huyu amepewa maagizo kutoka ngazi ya juu na kwa mujibu wa tangazo la Serikali Na 51 la tarehe 17 Disemba, 2010 mwenye dhamana ya kutoa maelekezo hayo ni Waziri Mkuu kwani ndio msimamizi mkuu wa Tamisemi... barua hii ilifuatiwa na agizo la wakurugenzi watendaji wa Halmashauri mbalimbali za Wilaya za Mkoa wa Mara na kusimamisha chaguzi hizo," alisema.

Alimtaka Waziri Mkuu kutoa kauli ya Serikali juu ya kusimamishwa kwa chaguzi hizo ili kupisha uchaguzi wa CCM.​
 
Back
Top Bottom