Mhadhiri Vicensia Shule: Rushwa ya Ngono inatawala Chuo Kikuu DSM

AbaMukulu

JF-Expert Member
Jan 1, 2018
2,048
3,568
Mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) ameandika katika ukurasa wake wa twitter kuhusu kukithiri kwa rushwa ya ngono chuoni hapo

Baba @MagufuliJP umeingia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kufungua maktaba ya kisasa. Rushwa ya ngono imekithiri mno UDSM. Nilitamani nikupokee kwa bango langu ila ulinzi wako umenifanya ninyamae. Nasubiri kusikia toka kwako maana naamini wateule wako ni waadilifu watakwambia ukweli

shule.PNG

MY TAKE:
Taasisi zote zinazohusika zichukulie swala hili kwa uzito wake. Rushwa ya ngono inapelekea wahusika wengi kuonekana vizuri kwenye makaratasi kumbe kichwani ni 'kilaza'

=======

1543382428239.png
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dkt Vicencia Shule, amemuomba Rais Dkt Magufuli kuingilia kati, kutokana na kukithiri kwa rushwa ya ngono chuoni hapo. Dkt Shule alizuiwa kuonesha bango lake kuhusu vitendo hivyo, wakati Rais akizindua maktaba mpya chuoni hapo leo.

=====

UPDATE;

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Vicensia Shule ameitwa kwenye kamati ya maadili ya Chuo hicho kuhusiana na taarifa yake aliyoitoa kwenye mtandao wa Twitter akimuomba rais John Magufuli kuingilia kati kukithiri kwa rushwa ya ngono chuoni hapo.
 
Mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) ameandika katika ukurasa wake wa twitter kuhusu kukithiri kwa rushwa ya ngono chuoni hapo
View attachment 948345

MY TAKE:
Taasisi zote zinazohusika zichukulie swala hili kwa uzito wake. Rushwa ya ngono inapelekea wahusika wengi kuonekana vizuri kwenye makaratasi kumbe kichwani ni 'kilaza'
Amesema mambo mengine anajua yapo lkn hatayasema
 
Mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) ameandika katika ukurasa wake wa twitter kuhusu kukithiri kwa rushwa ya ngono chuoni hapo
View attachment 948345

MY TAKE:
Taasisi zote zinazohusika zichukulie swala hili kwa uzito wake. Rushwa ya ngono inapelekea wahusika wengi kuonekana vizuri kwenye makaratasi kumbe kichwani ni 'kilaza'
Sasa Kwa Nn Hajawataja Hao Wanaopkea Hyo Rushwa Ya Ngono?
 
Aripot kwenye vyombo husika.

Ila hii kitu ni ngumu saana kuisha.



Kwani Magufuli siyo chombo husika? Alikwenda hapo kufanya nini kama siyo chombo? Mhadhiri amesema kuwa alitamani kumfikishia ujumbe kwa namna ambayo Magu angesoma moja kwa moja, lakini akagundua kuna kizuizi, tafsiri yake ni kwamba vyombo husika vinafahamu kiwango cha tatizo lakini havipo tayari kutoa ushirikiano na wala havilifanyii kazi yawezekana ni kutokana na kulindana kwingi.

Bravo Mhadhiri umefanya jambo la kishujaa, anayekulaumu ana lake jambo
 
Back
Top Bottom