Mhadhiri Bashir Ally (UDSM) Atafutiwe Jimbo!

Mhadhiri Bashir Ally (UDSM) Atafutiwe Jimbo!

Omutwale

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2008
Posts
1,429
Reaction score
1,053
bashiru.jpg

Bwana Bashiru Ally, Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Bwana Bashiru Ally ni miongoni mwa vijana waliofuzu makuzi ya kitaaluma na kijamii kutoka kwa watu wanaoheshimika na historia ya nchi hii; ile ambayo haikuhifadhiwa rasmi vitabuni. Enzi zetu tukiwa masomoni Bwana Bashir na Omar Ilyas ni miongoni mwa vijana waliopendwa na kujiweka karibu na Marehemu Prof. Haroub Othman (former VC-UDSM). Hali halisi inajidhirisha kuwa Bwana Bashir ndiye aliyefuzu kuyashika vema mafunzo na weledi wa Prof. Haroub Othman. Baada ya kuachana kitambo, miaka ya hivi karibuni nimekuwa nikimsikiliza, kumuona au kumsoma kupitia vyombo vya habari. Mara nyingine kwa bahati tumewahi kukutana kwenye mikutano.

Hivi majuzi Bwana Bashiru alishiriki mjadala wa DW juu ya miaka 15 ya mapambano dhidi ya ugaidi. Msimamo na utetezi wa mtazamo wake juu ya jinsi vita hii inavyopiganwa nakubaliana nao kwa asilimia 100-"Mbinu zinazotumika kupambana na ugaidi ni za kigaidi na hivyo zinazidisha ugaidi"

Bwana Bashiru ni mtu aliyejipambanua kuwa na msimamo usiyoyumba katika masuala ya Kitaifa na yale yote anayoyaamini baada ya kuyatafiti kwa kina. Si mtu wa papara na kuropoka. Hisia zake juu ya jambo lolote hazijathibitika kufungamana na imani au itikadi. Kiufupi ni mtu-huru, mwenye fikra chanya kwa mustakhabari wa jambo lolote analoshiriki kulitenda au kulipendekeza. Tuna uhaba wa watu wenye sifa hizi katika utungaji wa sera na kuisimamia serikali. Kumuacha aendelee kuongea na makaratasi au kuwasilisha hoja zake kwa Power Point mikutanoni na kisha akitoka ukumbini hakuna wa kuzitekeleza ni matumizi mabovu ya rasilimali watu wa nchi hii.

Ili Taifa liweze kunufaika na weledi wa Bwana Bashiru, naomba ashawishiwe kujiunga rasmi na siasa za majukwaani na atafutiwe jimbo ili kuanzia 2016 inshallah Taifa linufaike na vipawa vyake. Binafsi sijali atajiunga na CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, n.k ilimradi tu asijiunge na ccm, mahali ambako mawazo mapya na utendaji ni dhambi. Akitaka Jimbo nitamchagulia Bukoba Vijijini na nitakuwa tayari kuanza kumpigia kampeni. Naamini maeneo yenye wapiga kura wengi kama Ibwera na Katoro hatutakuwa nahaja kabisa ya kupita kupiga kampeni.

Eid Mubraak!

Cc: FaizaFoxy, Ritz, omar Ilyas, njiwa, Nivea
 
Nitamshawishi atumie vema jukwaa alilonalo UDSM kuzalisha vijana watakaokuwa na kufuzu kwa misingi na vigezo kama ambavyo yeye amerithishwa na Haroub. Bila shaka itakuwa na manufaa zaidi
Mie nadhani utakuwa ni ushauri mzuri na wenye manufaa kwa Taifa. Lakini si mbaya pia kushiriki moja kwa moja toka uwanja wa mapambano walau kwa kutumia Sabbatical Leave ya miaka 5. Toka hapo akirejea ataweza kuoanisha kiada (curriculum) na mahitaji halisi kwenye uwanja wa mapambano!
 
Bashiru zamani nilimwona kama msomi ambaye alikuwa anataka kuibadilisha hii nchi, ila nilimushuhudia kwenye kituo kimoja cha tv wakijadili kuhusiana na mabomu yaliyolipuliwa arusha, alikuwa anaongea kama mtu aliyetekwa na siasa za udini, badala ya kuongea hali halisi alijifunua na tukamujua namna alivyo, kwa ufipi mi namwona kama mtu hatari sana na hasa kwa kueneza propaganda za udini. Siku hizi hachambui mambo kama msomi mwenye kutaka kuleta mabadiliko ila anaongea km mtetezi wa dini fulani na pia kama mchocheza na mchonganishi
 
Bashiru zamani nilimwona kama msomi ambaye alikuwa anataka kuibadilisha hii nchi, ila nilimushuhudia kwenye kituo kimoja cha tv wakijadili kuhusiana na mabomu yaliyolipuliwa arusha, alikuwa anaongea kama mtu aliyetekwa na siasa za udini, badala ya kuongea hali halisi alijifunua na tukamujua namna alivyo, kwa ufipi mi namwona kama mtu hatari sana na hasa kwa kueneza propaganda za udini. Siku hizi hachambui mambo kama msomi mwenye kutaka kuleta mabadiliko ila anaongea km mtetezi wa dini fulani na pia kama mchocheza na mchonganishi

I knew it'd turn out this way! There is nothing nowadays that could be discussed in here regarding Tanzanian society without this :'udini' thing, especially when a muslim or muslims are part of the subject. The stone age still exists.
 
Nchi hii watu wanasoma ili wawe wanasiasa? Mtu anakuwa doctor au prof anaacha kuhudumia wananchi kwa kufanya research ili kuweka mazingira mazuri ya utafit anakimbulia kazi ambazo hata Lusinde darasa la 7 anafanya na ofcpz hawana tofauti ktk output zao.

Why why why my country? Prof Anna Tiba, Mwandosya, Hemed Msolla et al. Yani uprof wenu mnaiexercise bungeni ambako hata non-elite anaweza perform?

Sasa kijana kama huyu anataka kuzamia huko nae, mweeee kazi iko. Nimekuwa mfuatiliaji wa siasa za nje kidogo, ukichunguza mabunge mengi wazee ndio wako huko wkt ss vijana ndio option yenye ulaji tunaiona. Ka
MzLendo si uanzishe kitu ili kusaidia watu wengi kwa kutumia ujuzi wako wa darasani?

Inakatisha tamaa wasomi kukimbilia dodoma kwa kweli na vyuoi wanabaki ma-TA na Ass Lecturers
 
Unamtaftia au atafte? Au aamue kugombea. Acha siasa kwenye maisha ya mtu
 
Mie nadhani utakuwa ni ushauri mzuri na wenye manufaa kwa Taifa. Lakini si mbaya pia kushiriki moja kwa moja toka uwanja wa mapambano walau kwa kutumia Sabbatical Leave ya miaka 5. Toka hapo akirejea ataweza kuoanisha kiada (curriculum) na mahitaji halisi kwenye uwanja wa mapambano!
hapo ndo tunapokosea......
siyo kila mtu mwenye upeo fulani lazima aingie kwenye siasa, tunahitaji wataalamu wengi zaidi ya wanasiasa... wataalamu ambao hawajafungwa siasani ndo pekee ambao wanaweza kututoa point moja kwenda nyingine. si tunashuhudia wenyewe hapa jinsi ambavyo watu wengi tuliowaamini sana kwa utaalamu wao wanavyotuangusha wakienda huko ulingoni?
Mi nadhani hapo alipo patamuwezesha kusambaza hayo mazuri aliyonayo vizuri zaidi kuliko akienda jimboni
 
Ukimsikiliza kwa makengeza unaweza kusema ulivyoandika lakini ukimpata hasa kwenye mijadala yenye kuhusisha dini utatambua bado hajafika unaposema ww.mshauri aende ccm ndiko wanakotafutia watu majimbo kwingine atafute mwenyewe
 
Nitamshawishi atumie vema jukwaa alilonalo UDSM kuzalisha vijana watakaokuwa na kufuzu kwa misingi na vigezo kama ambavyo yeye amerithishwa na Haroub
Bila shaka itakuwa na manufaa zaidi

binafsi nashauri aendelee na kazi ya kufundisha vijana,
kuwa mchambuzi wa siasa na kuwa mwanasiasa ni kazi 2 tofauti
 
Unamtaftia au atafte? Au aamue kugombea. Acha siasa kwenye maisha ya mtu
 
huyu mtu yuko smart sana.. suala la kuwa mbunge au lah ni lake mwenyewe.. hata hapo UD anaihudumia jamii vzur xana....!
 
Bashiru zamani nilimwona kama msomi ambaye alikuwa anataka kuibadilisha hii nchi, ila nilimushuhudia kwenye kituo kimoja cha tv wakijadili kuhusiana na mabomu yaliyolipuliwa arusha, alikuwa anaongea kama mtu aliyetekwa na siasa za udini, badala ya kuongea hali halisi alijifunua na tukamujua namna alivyo, kwa ufipi mi namwona kama mtu hatari sana na hasa kwa kueneza propaganda za udini. Siku hizi hachambui mambo kama msomi mwenye kutaka kuleta mabadiliko ila anaongea km mtetezi wa dini fulani na pia kama mchocheza na mchonganishi

kwann mkiona majina ya kiislam roho zenu zinawajaa chuki, husda, fitna na upumbavu? Mnadhani mnayofundishwa huko makanisani na akina slaa hatuyajui? Hii nchi siyo ya kanisa wala ya wakristo peke yao wala sio ya waislam peke yao. Ndio chuki mliyonayo kwa kikwete kisa dini yake. Mtakufa km mimbwa koko na chadema yenu ya kiliberali
 
haha..mmeshafikia hapo?Si wa kile kitengo cha wapiga matarumbeta wa kukodi toka chuo kilichoipa nchi hasara UDSM.?Haha...napita tuu.
 
Akiingia kwenye hawezi kuwa na hiyo misimamo yake km ni cdm ajue kina Mbowe watamdrive na atageuka kuwa mburula. Mwache aeneze maarifa.
 
Ni mwl mzuri sana ktk ufundishaji kama ilivyo kwa dr bana ila kwenye mijadala hayuko objective sana.
 
kwann mkiona majina ya kiislam roho zenu zinawajaa chuki, husda, fitna na upumbavu? Mnadhani mnayofundishwa huko makanisani na akina slaa hatuyajui? Hii nchi siyo ya kanisa wala ya wakristo peke yao wala sio ya waislam peke yao. Ndio chuki mliyonayo kwa kikwete kisa dini yake. Mtakufa km mimbwa koko na chadema yenu ya kiliberali
Kwani nasi hatujui wakuu wa idara za kitaaluma na wahadhiri wanavyofanya kwa wanafunzi wakiislamu na mabaya kwa wakristo kusudi muonekane mnafaulu kumbe wapi majina yenu
 
I knew it'd turn out this way! There is nothing nowadays that could be discussed in here regarding Tanzanian society without this :'udini' thing, especially when a muslim or muslims are part of the subject. The stone age still exists.

Definition ya mdini Hapa Tanzania ni Muislamu yoyote ambaye yupo katika wazifa wowote ule...
 
Back
Top Bottom