Mh.Spika Mimi naunga hoja Mkono 100%, Lakini kule..

Mh.Spika Mimi naunga hoja Mkono 100%, Lakini kule..

Many MP not know what doing in parliament specially ccm special seats. their head is ornament for horny old MP or head is hair garden. Big head like elephant small brain like pig. I am not know what they doing in parliament.
 
Hawa jamaa hawaeleweki kabisa Mbunge anasimama na kusifu Serikali kuwa ni sikivu,inajali watu wake,inamipango madhubuti kuiniua uchumi wa watu wake na kadharika ikiwa sambamba na kuunga mkono hoja zitolewazo na mawaziri katika kuwasilisha bajeti.
Wanapokuja kunichosha ni kuwa baada ya kutoa sifa zote hizo,Mbunge husika anaanza kulalamika mara ooh serikali imetutelekeza wakazi wa jimbo la ..... mara ooh serikali haikamilishi miradi kwa wakati muafaka na kero nyingi nyingi.
Ni bora mnapopata nafasi kuchangia muwe straight to point sio kuzunguka zunguka.

ndio ujue kuwa ni wanafiki na wasaliti wanajifanya watetea wananchi kumbe uongo lao ni moja
 
Spika Makinda: Sasa tunaendelea na majadiliano kuhusu bajeti ya wizara ya miundombinu,Anayeanza kuchangia kwa asubuhi ya leo Mheshimiwa Diana Chilolo,Atafuatiwa na Mheshimiwa Peter Serukamba,Kangi Lugora na Suzanne Lymo.

Diana Chilolo: Mheshimiwa Supika,Nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuchangia kwenye bajeti hii ya wizara ya miundombinu.Kwanza kabisa napenda kumpongeza waziri Makufuri kwa Kazi nzuri sana anayoifanya ya kuhakikisha nchi yetu inapata miundombinu iliyo bora na ya kisasa kabisa,Kwakweli nampongeza kwa hilo waziri Makufuri kwani ni jembe hasa.

Mheshimiwa Supika,Pamoja na pongezi hizo lakini pia jimbo langu limekuwa katika kilio cha muda mrefu juu ya miradi ya barabara ambayo serikali yetu iliahidi kuikamilisha lakini huu mwaka wa kumi sasa hakuna kilichofanyika.

Mheshimiwa waziri we we mwenyewe ni shahidi mwaka Jana mwezi wa kumi na mbili ulikuja katika jumbo langu na nikakutembeza na nadhani mwenyewe umejionea hali ya barabara jinsi ilivyokuwa mbaya,Na uliniahidi kwenye bajeti ijayo miradi ya barabara kwenye jimbo langu itatengewa fungu la fedha lakini nikiangalia kwenye hiki kitabu cha bajeti ya wizara yako ninaona tu jina la jimbo langu lakini sioni fungu la fedha lilotengwa kwaajili ya miradi ya barabara ya jimbo langu,Sasa sijui ndiyo kusema umetudharau mimi na wale ninaowakilisha kwenye langu au Vipi?Baada ya kusema hayo niseme tu kwamba nakushukuru Mheshimiwa Supika kwa kunipatia fursa hii ya kuchangia kwenye hoja iliyoko mezani na ninamalizia kwa kusema...

Ninaunga mkoani hoja kwa asilimia mia moja (Anapigiwa makofi kwa nguvu ikifuatiwa na vigelegele kama vile wako kwenye SEND OFF wakiongozwa na Mheshimiwa Asha Bakari).

Hawa ndiyo Wabunge wetu wanaotuwakilisha Bungeni wakitimiza wajibu wao wa kuisimamia serikali.Kwanini Tanzania tusiendelee?
 
Kwa maelezo hayo huyu mbunge haungi hoja mkono kwa 100%. Lakini kwa vile mdomo wake hauna mawasiliano mazuri na akili yake anajikuta anasema kile asichokiamini. Wapo wengi tu sio huyu peke yake.
 
Spika Makinda: Sasa tunaendelea na majadiliano kuhusu bajeti ya wizara ya miundombinu,Anayeanza kuchangia kwa asubuhi ya leo Mheshimiwa Diana Chilolo,Atafuatiwa na Mheshimiwa Peter Serukamba,Kangi Lugora na Suzanne Lymo.

Diana Chilolo: Mheshimiwa Supika,Nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuchangia kwenye bajeti hii ya wizara ya miundombinu.Kwanza kabisa napenda kumpongeza waziri Makufuri kwa Kazi nzuri sana anayoifanya ya kuhakikisha nchi yetu inapata miundombinu iliyo bora na ya kisasa kabisa,Kwakweli nampongeza kwa hilo waziri Makufuri kwani ni jembe hasa.

Mheshimiwa Supika,Pamoja na pongezi hizo lakini pia jimbo langu limekuwa katika kilio cha muda mrefu juu ya miradi ya barabara ambayo serikali yetu iliahidi kuikamilisha lakini huu mwaka wa kumi sasa hakuna kilichofanyika.Mheshimiwa waziri we we mwenyewe ni shahidi mwaka Jana mwezi wa kumi na mbili ulikuja katika jumbo langu na nikakutembeza na nadhani mwenyewe umejionea hali ya barabara jinsi ilivyokuwa mbaya,Na uliniahidi kwenye bajeti ijayo miradi ya barabara kwenye jimbo langu itatengewa fungu la fedha lakini nikiangalia kwenye hiki kitabu cha bajeti ya wizara yako ninaona tu jina la jimbo langu lakini sioni fungu la fedha lilotengwa kwaajili ya miradi ya barabara ya jimbo langu,Sasa sijui ndiyo kusema umetudharau mimi na wale ninaowakilisha kwenye langu au Vipi?Baada ya kusema hayo niseme tu kwamba nakushukuru Mheshimiwa Supika kwa kunipatia fursa hii ya kuchangia kwenye hoja iliyoko mezani na ninamalizia kwa kusema...

Ninaunga mkoani hoja kwa asilimia mia moja (Anapigiwa makofi kwa nguvu ikifuatiwa na vigelegele kama vile wako kwenye SEND OFF wakiongozwa na Mheshimiwa Asha Bakari).
 
Kwa maelezo hayo huyu mbunge haungi hoja mkono kwa 100%. Lakini kwa vile mdomo wake hauna mawasiliano mazuri na akili yake anajikuta anasema kile asichokiamini. Wapo wengi tu sio huyu peke yake.

Inaonesha mleta mada nae ni hali kadhalika; "Ninaunga mkoani hoja".
 
Inaonesha mleta mada nae ni hali kadhalika; "Ninaunga mkoani hoja".

Ni simu ndiyo inayofanya hivyo inasumbua sana kimtindo na mtindo wake wa kuleta three options of words choice inasumbua sana!
 
Kuna mtindo wa ajabu wa asilimia kubwa ya wabunge hasa wa CCM kuunga mkono hoja kwa asilmia mia halafu anaanza kulalamikia serikali matatizo lukuki jimboni kwake ikiwemo huduma za maji, barabara, afya, umeme, elimu, ... baada ya kumaliza anarudia tena kuunga mkono hoja asilmia 100%. Je, ni matatizo ya akili au ni ushabiki wa kinafki tu?
 
Mkuu huo ni unafiki na ufinyu Wa akili Wa wabunge Wa ccm Mwenyekiti wao kaisaini rasimu ya katiba ya time ya warioba kaikabidhi binge an agenda bungeni anaikataa ni akili za aina gani hizo?
 
Ndo uwezo wao wa kufikiri ulipofikia
Nakubaliana nawe kabisa. Mada hii ililetwa hapa zaidi ya mwaka mmoja uliopita, na badala ya kusoma ( kama wanasoma) na kuelewa kisha kujirekebisha wao wanarudia yale yale. Juzi akichangia Lissu alijaribu kuwakumbusha wabunge wajibu wao wa kikatiba ni nini bila kujali Mbunge anatoka chama gani dhidi ya kuisimamia serikali na kiwajibisha.
Ajabu bado waliendelea kutoelewa anawaambia nini na kuendelea kuponda upinzani, kopongeza 100% serikali kisha kulalamika sana kuwa wamesahauliwa.
Hivi waziri uliyempongeza 100% kuonyesha kuridhika na anayofanya jimboni kwako anahaja gani kuhangaika tena na kilio chako?
NI KWELI KUWA AKILI ZAO HAPO NDIO MWISHO
 
Nakubaliana nawe kabisa. Mada hii ililetwa hapa zaidi ya mwaka mmoja uliopita, na badala ya kusoma ( kama wanasoma) na kuelewa kisha kujirekebisha wao wanarudia yale yale. Juzi akichangia Lissu alijaribu kuwakumbusha wabunge wajibu wao wa kikatiba ni nini bila kujali Mbunge anatoka chama gani dhidi ya kuisimamia serikali na kiwajibisha.
Ajabu bado waliendelea kutoelewa anawaambia nini na kuendelea kuponda upinzani, kopongeza 100% serikali kisha kulalamika sana kuwa wamesahauliwa.
Hivi waziri uliyempongeza 100% kuonyesha kuridhika na anayofanya jimboni kwako anahaja gani kuhangaika tena na kilio chako?
NI KWELI KUWA AKILI ZAO HAPO NDIO MWISHO

Tuweke vigezo kwa mtu kuwa mbunge
 
"Mh! Spika!,

Awali ya yote napenda kuunga mkono hoja, ni kweli chama cha mapinduzi kimefanya mengi mazuri nchi hii, na bajeti hii imemjali mwananchi wa hali ya chini,

Mh. Spika, Naona upinzani umefikia pabaya, wanaikashifu serikali ya CCM kama vile hatufanyi hata zuri moja.

CCM imejenga sekondari za kata nchi nzima, imejenga zahanati kila kona ya nchi hii, imejenga barabara za lami nchi nzima, imejenga miradi ya maji kote nchini, madawa yanapatikana hata ktk zahanati za pembezoni. na wananchi "wetu" wanafurahia maisha sasa na wanaipongeza serikali ya chama cha mapinduzi,

Ila wenzetu wa upinzani hawayaoni mazuri ya CCM na matunda ya utawala wa serikali ya chama cha upinzani.

mh. Spika kabla sijaenda mbele nitake nieleze kule jimboni kwangu -------- hakuna shule za kata ktk kata 9 kati ya 14, maji yamekuwa ndoto, hakuna hata kipande kimoja cha barabara ya lami, kuna kituo kimoja tu cha afya tena hakuna dawa za kutosha, na zaidi ya yote wanafunzi wanakaa chini wawapo madarasani. Naomba nisaidiwe na waziri mwenye dhamana anijibu.

Mh. Spika, Naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.(makofi) kwa! kwa! kwa! kwa! kwa! kwa!
 
Sishangai maana kuwa mwanaCCM tu ni sawa na mwendawazimu..

Lakini wenyewe wanaelewana na makofi anapigiwa..
 
Japo ninaungana nawe kusikitikia hayo, ila usishangae sana.

Ubunge sio taaluma.

Rejea moja ya sifa za kuwa mbunge: "Kujua kusoma na kuandika...."
 
Back
Top Bottom