Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,804
- 1,871
Sasa mambo yameiva, asiye na mwana aeleke jiwe!
Mwaka 2005 katika kampeni za uchaguzi CCM walishangazwa na CHADEMA kutumia Helkopta kufanya kampeni katika nchi masikini kama Tanzania. Katika uchaguzi mdogo wa Mara CCM wakaiga matumizi ya Helkopta, lakini baada ya uchaguzi Makamba akapiga marufuku kwa CCM kutumia Helkopta. Kwani mfuko ulitoboka sana bila mafanikio.
Mwaka huu CCM wamekuja na mpya 'Bongo flavor' mpaka asubuhi. Usisahau usafiri wa malori. Baada ya kuona mtindo huo umefanikiwa sana katika kuwakusanya vijana, ukimya wa Mh Slaa umemuishia na sasa ameshaanza kunena. Lakini jibu la KIKWETE NI RAHISI, KAZI NA BURUDANI. Kusanya watu kwanza ndio wape SERA.
Hii ni alama ya kuwa mambo kwa Mh Slaa hayaendi vizuri, na ameshaona kuwa hata lile lengo lake la 25% huenda asilifikie. Na ukizingatia kuwa siku zilizobaki ni chache ndio kiwewe kimempanda.
Hali sio hiyo tu bali mbaya zaidi ni kwamba mfuko wa CHADEMA umeshatoboka wakati ule wa CCM ndio kwanza unajaa.
Sasa Mh Slaa amechanganyikiwa na hajui afanye nini. Pengine kama hapa JF mtapitisha mchango kwani ni Rahisi mkiweka A/C namba.
Mpaka jibu halijapatikana, dawa iliyobaki ni kumkoromea Kikwete ili aachane wa wasanii bora, kitu ambacho ni vigumu kuwezekana.
Mwaka 2005 katika kampeni za uchaguzi CCM walishangazwa na CHADEMA kutumia Helkopta kufanya kampeni katika nchi masikini kama Tanzania. Katika uchaguzi mdogo wa Mara CCM wakaiga matumizi ya Helkopta, lakini baada ya uchaguzi Makamba akapiga marufuku kwa CCM kutumia Helkopta. Kwani mfuko ulitoboka sana bila mafanikio.
Mwaka huu CCM wamekuja na mpya 'Bongo flavor' mpaka asubuhi. Usisahau usafiri wa malori. Baada ya kuona mtindo huo umefanikiwa sana katika kuwakusanya vijana, ukimya wa Mh Slaa umemuishia na sasa ameshaanza kunena. Lakini jibu la KIKWETE NI RAHISI, KAZI NA BURUDANI. Kusanya watu kwanza ndio wape SERA.
Hii ni alama ya kuwa mambo kwa Mh Slaa hayaendi vizuri, na ameshaona kuwa hata lile lengo lake la 25% huenda asilifikie. Na ukizingatia kuwa siku zilizobaki ni chache ndio kiwewe kimempanda.
Hali sio hiyo tu bali mbaya zaidi ni kwamba mfuko wa CHADEMA umeshatoboka wakati ule wa CCM ndio kwanza unajaa.
Sasa Mh Slaa amechanganyikiwa na hajui afanye nini. Pengine kama hapa JF mtapitisha mchango kwani ni Rahisi mkiweka A/C namba.
Mpaka jibu halijapatikana, dawa iliyobaki ni kumkoromea Kikwete ili aachane wa wasanii bora, kitu ambacho ni vigumu kuwezekana.