Jasusi , Tatizo langu ni vyama kutokuwa specific katika maelezo yao. Ninavyofahamu, chini ya mpango wa CCM, kijiji kinarusiwa kuuza au kugawa ardhi ya ekali 100 mpaka 500 bila idhini ya serikali kuu (stand to be corrected). Lakini ukiangalia hapa tunaongelea mwekezaji wa maelfu ya ekali ambapo mwenye jicho katika maamuzi ni serikali kuu.
Tuna choice mbili, either tuwe kama wajamaa au tufuate uwekezaji wa kipepari ambao misingi yake ni wachache kuwa super rich regardless kwa serikali kuwa na tight land law.
Ninakubaliana na wewe, Viongozi wetu wasipokuwa makini na swala la ardhi, tunaweza tukajikuta tuko kama Kenya lakini vile vile utakuwa ni ujinga kuogopa kufanya maamuzi ambayo yataonekana ni mabaya kisiasa.