Mh. Rais Magufuli, usipoongeza mshahara 2020 ruhusu uhamisho

Black Mirror

JF-Expert Member
Oct 17, 2019
829
1,034
Mheshimiwa Rais Magufuli wa Tanzania, wewe ndiye mwenye mamlaka ya mwisho kwa kila kitu hapa Tanzania. Mara nyingi umekuwa ukiwasihi watumishi wavumilie kuhusu kuongezewa mishahara kama inavyopaswa kuwa kwani sasa hivi unajenga nchi, lakini mheshimiwa unapaswa ukumbuke kuwa maisha hayasimami kwa watu kusubiria nchi ijengwe halafu yaendelee. Maisha yanaendelea wakati wote na wala hayasimami watu wanawaza mstakabali wa watoto wao, wake zao, ndugu zao na maisha yao.

Ukweli ulio hai ni kwamba sekta ya utumishi wa umma inapitia katika kupindi kigumu sana kuliko miaka yote na pengine kuliko tawala zote. Watumishi wa umma wana hali ngumu kimaisha, japo si wote maana wapo ambao wanakula keki ya Taifa sanjari na wewe.

Watumishi walio wengi uliwapunguzia mshahara kupitia kuongeza makato ya bodi ya mikopo kutoka 8% hadi 15% (haya ni maumivu makubwa sana). Mh Rais, mfano unapaswa ukumbuke bado watumishi hao hao wanakatwa kodi kubwa sana ya kutisha kuliko wafanya biashara, lakini wakirudi makwao bado wanakumbana na changamoto sawa na wananchi wengine mfno bei juu za vyakula na gharama nyingine kama kawaida.

Mh. Rais, juzi ulitoa kauli ya kuanza kufifisha tena matumaini ya watumishi wa umma uliposema kuwa hata wewe mshahara haukutoshi. Hii kauli inaashiria May 01/2020 hakuna tamko la kuongezewa mshahara. Hivyo basi nakuomba Mh Rais, Mei hiyo uruhusu watumishi waondolewe vikwazo vya kuhama. Hii ni kwa sababu kuwa miaka ya hivi karibuni kumekuwepo na wimbi kubwa la watumishi wa umma kutaka kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine, hasa walimu.

Walio wengi wanahitaji kuhama kutokana na ugumu wa maisha ulioimarishwa kipindi hiki. Hivyo, watumishi wanahitaji kuhama ili kupunguza ugumu huo kwani wengine wanajaribu kuchungulia mazingira rafiki ambayo walau yatawapa unafuu wa kuishi.

Mh Rais, basi walau siku hiyo waondolee vikwazo watu wahame tu bila bughudha zilizopo kwa sasa. Utakuwa umefanya la maana sana kwani tayari tunajua sasa hivi unajenga nchi; maslahi ya watumishi yanapaswa kusubiri japo maisha hayawasubiri na hata kodi tu twajua huwezi kupunguza pia.

Wasaidie watumishi tafadhali sana.
 
Kutokana na umuhimu wa mwezi October ya mwaka huu, hoja za bandiko hili zitatimizwa mwaka huu, mishahara itapanda, annual increments zitalipwa tena with arrears, madeni ya walimu yatalipwa, na ajira mpya zitafunguliwa.


P
 
Kutokana na umuhimu wa mwezi October ya mwaka huu, hoja za bandiko hili zitatimizwa mwaka huu, mishahara itapanda, annual increments zitalipwa tena with arrears, madeni ya walimu yatalipwa, na ajira mpya zitafunguliwa.

P
Ndugu yangu Mayalla P, October hii wala si muhimu sana km ambavyo wengi tulizoea huko nyuma...miaka ile masaa km haya wanasiasa wanajikomba kwa raia ili october wasiwaangushe ila kipindi hiki hakuna kitu kama icho maana chama tawala kina zaidi ya uhakika kuwa ndicho kitashinda tena kwa kishindo..ni jambo lipi litamsukuma mkuu wa nchi kutekeleza yote haya?

Yangu na wewe ni macho ngoja tusubiri muda ufike. Mei mosi siyo mbali sana japo sijui inafanyikia viwanja vipi.
 
Ndugu yangu Mayalla P, Octaber hii wala si muhimu sana km ambavyo wengi tulizoea huko nyuma...miaka ile masaa km haya wanasiasa wanajikomba kwa raia ili october wasiwaangushe ila kipindi hiki hakuna kitu kama icho maana chama tawala kina zaidi ya uhakika kuwa ndicho kitashinda tena kwa kishindo..ni jambo lipi litamsukuma mkuu wa nchi kutekeleza yote haya? Yangu na wewe ni macho ngoja tusubiri muda ufike. Mei mosi siyo mbali sana japo sijui inafanyikia viwanja vipi.
Uhakika wa ushindi upo, kwa kuanzia tuu ushindi wa 51% simple majority tayari upo na utapatikania mezani kwa CCM kupita bila kupingwa, lakini kinachotafutwa sio simple majority, ni landslide victory ya 99.9% kama kwenye serikali za mitaa, kiukweli rais Magufuli anakubalika sana na hili nimelizungumza hapa

P
 
Hahahaaa,nacheka lakini moyoni naumia sana,nashindwa kuonyesha maumivubyangu wazi wazi kwa sababu kuna "ML" na "uhujumu uchumi" ngoja niendelee kuonyesha meno tu kwa usalama wangu na ndugu zangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaumizwa na nini wakati huo ndio ukweli wenyewe halisi wa kitakachotokea, kuumia na kuficha maumivu na badala yake kuonyesha meno ili kulinda usalama wako, kwa kuhofia ML na Uhujumu, kunaonyesha kweli wewe ni fisadi!. Mtu safi asiye fisadi hawezi kuogopa ML na uhujumu!.

ila pia naungana na wewe kama kwa kunyamaza kimya kutakuepusha na mengi, bora nyamaza and be safe kuliko kupiga kelele na kuoneka shujaa behind bars!.
Na hili nimeisha shauri humu

P
 
Kwahiyo ataongeza mishahara kwa sababu mwezi Oktoba kuna uchaguzi!
Kama ndivyo, huyu hastahili kuchaguliwa tena kwani katika miaka yake mitano ya mwisho atawatesa sana watanzania na wafanyakazi kwa ujumla. Pascal Mayalla,
 
Back
Top Bottom