JUAN MANUEL
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 8,482
- 18,273
Kagera yamejaa manunda balaa,soko,stendi havijajengwa,sio kwa sababu hakuna rasilimali kisa tu ni kwamba ni mipango iliyobuniwa na Chadema,na Uongozi wa Mkoa hautaki kuunga mkono,unafsnya figisu figisu,hiyo miradi isijengwe,Mh. hongera sana, sielewi kama unaelewa msingi wa pongezi zangu. Ninamaanisha, hawamu hii ya tano mmeweza kuelewa kwamba mkoa wa Kagera na watendaji wa serikali ni "mizigo", wababaishaji, wazembe, wezi n.k .. Kimsingi si waadirifu hata kidogo.
Na naona hili umeweza kulibaini vizuri sana na hii inatokana na safari ambazo umeshazifanya katika mkoa huu, nadhani hii ni mara ya nne kama sikosei na kila ukirudi mambo ni yale yale. Nakusihi mh. Waziri mkuu, tumbua. Kuna watu manunda, hayasikii mvua wala jua, hebu fanya kuwaweka benchi kwanza wakuu kadhaa wa Idara hasa hasa hapa manispaa.
Mie nakusihi tu, kwamba najua unakereka sana na aina ya viongozi eneo hili, usipate kigugumizi kuwafyekelea ziwani. Wanafanya vile eti kisa ni mbali na Dar/Dom na kwasababu huu mkoa uko pembezoni kabisa na kwamba hata media zingine hazifiki kama maeneo ya karibu na Ikulu
Ondoka na vichwa kadhaa mh
Bei ya viwanja ni kubwa sana,ukilinganisha na mikoa kama Dodoma,Pwani au Singida
Sent using Jamii Forums mobile app