dropingcoco
Senior Member
- Jun 21, 2008
- 124
- 11
Najua unapita JF kwa hiyo sina wasiwasi na ujumbe wangu huu kwako. Arusha pale soko kuu kuna wimbi kubwa la watoto ambao umri wao unadhihirisha wazi kwamba wanatakiwa kuwa shule, na nahisi wengine wamekimbia shule ili wakafanye biashara ya kuuza mifuko na kubeba vifurushi vya wamama waliotoka kwenye manunuzi hapo sokoni. Wale watoto wanakera sana, na kama mtu unayependa taifa lako huwezi kuona kundi kubwa kama lile la watoto likiwa pale bila kupata elimu wakati tunasema watanzania tunapambana na Ujinga, Umaskini na Maradhi. Kwa mtindo huu ujinga hautakaa uishe hapa nchini. Chama cha magamba kimeshindwa kuwashughulikia, tuna imani na chama chetu cha ukombozi. hivyo basi tungeomba tuone unachukua hatua kama mbunge tulie na imani nae. Na pia sehemu zingine za nchi zenye sura kama hii basi nadhani kilio cha sisi watanzania wenye lengo zuri na nchi yetu kitakuwa kimesikika, na kuweza kuchukuliwa hatua ili tuweze kumshinda huyu adui Ujinga.
Nawakilisha
Nawakilisha