Mh. Lema na CHADEMA acheni ulaghai!

Mh. Lema na CHADEMA acheni ulaghai!

Ukweli ni huu; Mh. Lema alitoa ahadi zile akiwaomba wapiga kura wampe madiwani watakaomsaidia kuidhinisha maamuzi ya ahadi zile pia meya jambo ambalo halikutimia. Kuna ahadi nyingi sana ametekeleza pamoja na misukosuko mingi aliyoipata mahakamani.
 
Mwaka 2010 wakati wa kampeni, ulitoa ahadi ambazo zilisababisha watu wengi wakupe kura nikiwemo mimi.
cha kushangaza mpaka leo(miaka mitatu baadaye) hakuna hata moja iliyotekelezwa.
  1. Kuhamishia stendi kubwa ya mabasi eneo la ngulelo ili kupunguza msongamano mjini.
  2. kujenga Machinga complex kubwa katikati ya jiji la Arusha.
  3. Kuwapa akinamama na vijana mikopo ya kujiendeleza.
Vp na lile trekta ulilolitoa kwa wananchi liko wapi?

CHADEMA na LEMA acheni kudanganya wananchi, msidhani hatuna akili. Tunawangoja kwenye boksi la kura 2015.

Harufu ya choon! (MSALANI)
 
Sasa kama aliahidi kujenga barabara kwa kiwango cha lami, halafu WB wakatoa msaada wa kujenga barabara zetu unataka kusema ni ahadi za benki ya dunia kwenye mkutano wa ccm?
Acha ufala mazee hiyo ndo kazi ya mbunge aliyechaguliwa na wana Arusha

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Huo Mpango wa WB ulikuwepo hata kabla Lema hajafikiria kugombea ubunge! hata angeshinda Mbunge wa TLP hapa Arusha, barabara zingejengwa tu! Lema hana uwezo wa kuilazimisha WB itoe hela ya ujenzi wa barabara!
 
Mkuu wa mkoa bw magesa mulongo aliwaambia wajumbe wa halmashauri kuu ya ccm wilayani arumeru kuwa wachangamkie fursa ya kujenga stand maeneo ya Tengeru kwani ufisadi wa watendaji wa manispaa ya arusha umesababisha zoezi la kujenga stand kuu huko maeneo ya muriet kukwama pamoja na kwamba michoro ya mipango miji inaonesha hivyo.

Dawa ya maendeleo ni kuingo'a ccm na kufanya ukarabati mahususi katika mifumo yetu ya kiutawala,kiutendaji n.k

Tunaanza mwakani kwenye serikali za mitaa.
 
Huyu mtoa mada nina mashaka nilimwona, maana nilikuwa nimekaa mahali na watu kama watano akiwemo diwani moja. Anyway, labda mawazo yao yalifanana.

Katika mazungumzo yetu tulikuwa tunajadili maendeleo ya chama, then jamaa moja kaongelea hii mada ya ahadi za Lema, tena kazungumzia kuwa miaka mitatu imepita hakuna kitu. Japo nilimjibu pale inabidi nirudie hapa.

Hivi miaka mitatu unayozungumzia kwa Lema ni ipi? Lema alivuliwa ubunge, akakaa nje ya bunge almost miaka miwili, yote haya yamesababishwa na serikali ya ccm.
Kuna mambo mengi na muhimu ambayo Lema ameyafanya nchi hii ambayo ni muhimu kuliko ahadi za ubunge.
Kuwapatia watanzania ukombozi wa fikra, ambao umewafanya watanzania wengi wajitambue ni jambo kubwa kuliko Machinga Complex, ni kubwa kuliko ArDF

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Yaani haya magamba hayajatambua kuwa wao ndio kikwazo cha maendeleo Arusha.
 
Acha Porojo, sijakwambia ulinganishe ahadi za LEMA na JK? Machinga Complex iko wapi? na Lile Trekta Liko wapi?


Tafakari sana kabla ya kuja humu na bichwa lako utadhani una akili kumbe umebeba tu.

AMA UMETUMWA NINI?
 
Huo Mpango wa WB ulikuwepo hata kabla Lema hajafikiria kugombea ubunge! hata angeshinda Mbunge wa TLP hapa Arusha, barabara zingejengwa tu! Lema hana uwezo wa kuilazimisha WB itoe hela ya ujenzi wa barabara!
sio lema tu, wabunge wote hawana mamlaka hiyo!
 
Acha Porojo, sijakwambia ulinganishe ahadi za LEMA na JK? Machinga Complex iko wapi? na Lile Trekta Liko wapi?

Sasa si umuulize yeye unatuuliza sisi? Yeye atakupa vipau mbele vya jiji la Arusha kwani jiji haliendeshwi kwa ahadi za wabunge. Kero inapokuwa kubwa jiji ndio huamka na kama mbunge alikuwa amelipgia chapuo ndio hapo utaona kuwa ahadi yake imetimia. hilo trekta ni la kuzo taka au la kulima? Arusha mjini sidhani kama kuna mashamba ya kulima kwa trekta. Leam wapatie wananchi wako hilo trekta wakazoe taka sokoni.
 
Back
Top Bottom