Masanilo
Platinum Member
- Oct 2, 2007
- 22,286
- 4,493
- Thread starter
- #41
Mimi wala simtetei kwa chochote, tunachobishania hapa ni namba tu. Kwa mihula ya masomo hiyo inaweza kuwa miaka miwili, na inaweza kuwa miaka mitatu pia kutegemea ameanza kipindi gani cha mwaka. Kama alianza December 1994 na akamaliza December 1996 hiyo ni miaka miwili. Na kama ameanza Januari 1994 akamaliza December 1996 hapo itakuwa miaka 3. Hata kama alianza March 1994 na akamaliza Nov/Dec 1996 bado itakuwa miaka mitatu. Yaani katika akademia hatuhesabu miaka kwa hesabu ya kutoa, kuna vyuo hapa duniani vinaanza masomo Januari, June, September. Na isitoshe kuna baadhi ya vyuo unaweza kusoma credit nyingi kwa mwaka mmoja, kiasi kwamba ukafupisha muda wa masomo, ili mradi uwee umekamilisha credit zinazohitajika katika program nzima. Katika baadhi ya nchi hili linawezekama ila kwa Tanzania haliwezekani.
Crap.....!