Mh. Hamad Rashid LIVE on Star TV

Mh. Hamad Rashid LIVE on Star TV

yah! He is on air.weekend murua kwa nccr ya mageuzi ya kweli na cuf ya pemba
 
Naona Hamad anasema Katiba ya Jamuhuri ya Muungano inasaidia kuleta migogoro kwenye vyama kwa kuwa inalazimisha watu wawe kwenye vyama ili waweze kuwawakilisha wananchi, matokeo yake ni kwamba watu ambao hawana interest na vyama wanalazimika kuwa wanachama wa vyama flani.

Hii ina maana analaumu kwanini mgombea binafsi hajaruhusiwa?
 
Huku niko mbali sana wala simsikii.Naomba niulizie maswali yangu kwake (a) ......akijibu muulize (b).

(a) Hivi unachotaka hasa ni nini ndani ya CUF?.
(b) Pindi ukipewa ukatibu mkuu hata bila uchaguzi utaridhika na kunyamaza?.
 
Asante Yahya, wewe ni mmoja wa watangazaji wachache wenye uthubutu wa kuyatumia maoni yetu humu.

Alichoongea Hamad juu ya wanahabari kutojiona wasafi nyakati zote, haoni kama ni yaleyale kwa wanasiasa akiwemo yeye?
 
kwa ni nini vyama upinzani nchini vimekuwa vikiandamwa na migogoro,je inasababishwa na wana chama wenyewe ama mamluki kama wanavyodai wenyewe?
 
Ok, wao kama wanasiasa wanaionaje kasi na nguvu ya New Media (mitandao ya wavuti na simu n.k)? Wamejiandaaje kushiriki? Kama hajui maana ya New Media basi mwache usiendelee kumwuliza maana yawezekana anadhani inatakiwa kuwa controlled.
 
Naomba nimuulize Mzee wangu hapo Hamad Rashid, ni kwa nini ameanza harakati za kuwania ukatibu mkuu mapema kiasi hiki tofauti na taratibu za kichama? Je kwa sisi ambao tuliofuatilia kipindi cha mwanzo kabisa bungeni mara baada ya uchaguzi na kuona jinsi alivyokuwa anahangaika kubadili vifungu vya bunge ili kuwe na kambi isiyo rasmi bungeni,atatushawishi vipi kuwa yeye si mroho wa madaraka?
 
Swadakta ndugu Yahya, swali langu:

a} Ukizingatia ukomavu wa Mh.Hamad katika siasa, je ni sahihi kwa yeye kuanzisha chama kingine endapo atafukuzwa CUF???
b} Anaongeleaje muafaka wa CCM na CUF kwa sasa, umemaliza kiini cha tatizo Znz?
c} Muungano; una maslahi kwa Wazanzibari wa kawaida {tofauti na viongozi}?
 
@yahya


Namuuliza Hamad Rashid:

Je yeye akiitwa mroho wa madaraka itakua anaonewa? Alipokuwa mkuu wa kambi ya upinzani hakusema kitu na alipokosa akaanza malumbano bungeni na kambi rasmi. Je, nikisema kuwa kwa sasa anataka ukatibu mkuu kwa nguvu itakuwa namuonea? Kama uchaguz ni 2014, mbona ameanza mapema? Kwani kampeni tayari? Na kwanini hayo madai asiyapeleke kwenye vikao?

Au kama CUF ni wazush, kwanin wasijitenge waanzishe chama chao?
 
Muulize:
Kwanini wakati yeye anatangaza kuwa na ugomvi na mwenzake. maalim Seif mwenyewe hajaonesha uhasama naye na yuko kimya.Hali hii imekujaje?.
 
Huyo jamaa yetu wa TADEA, anadhani kuna haja ya chama chake kuendelea kuwepo? Au vyombo vya habari ndivyo vimemnyima fursa ya kusikika?
 
mimi naomba nimuulize swali hili. Mh Hamadi Rashid wakati CUF inaingia ndoa na cccm hukuliona hili kwamba litadhoofisha chama chenu kisiwe tena chama cha upinzani, mbona hatukusikia ukipinga mfumo huu?
 
Mheshimiwa Ahmad Rashid apambane na asiogope hakuna mtu mwenye hati miliki ya siasa za nchi kila mtu ana haki ya kushiriki katika siasa za nchi. Maalim seif amekwisha nogewa.

Ila na wewe uache tabia ya kuwasakama wapambanaji wengine kama CHADEMA. Chama chenu kimepoteza mwelekeo na sasa kimeacha kuwatumikia wananchi na kuanza kugombea ruzuku ambazo ndio nahisi ni chanzo cha migogoro katika vyama vingi vya siasa.

Na nyie waandishi wa habari muache kutumiwa simameni katika taaluma wanasiasa huwa wanawatumia wakati wakiwa na shida ila mkitoa maovu yao wanawashambulia
 
swali kwa Hamadi. Je haoni cuf kuungana na ccm ndio chanzo cha mgogoro ? Maana imefanya Seif kuacha kufanya siasa za upinzani na kutekeleza sera za ccm? Ile ngangari iko wapi? Je ni lazima Hamad aanzishe chama au awe ktk chama?
 
Yahya,

Asante sana kwa fursa hii.

Naomba umuulize Hamad; kwa maoni yake baada ya kutafakari sana mustakabari wa siasa na nchi ya Tanzania, kama angekuwa na uwezo wa kureshape au kuanzisha upya, nini angefanya tofauti na ni eneo gani linahitaji mabadiliko makubwa?
 
swali langu kwa hamad rashid mohammed ni kitu gani kime kupelekea kutangaza nia?
 
Back
Top Bottom