Mh Godbless Lema amjibu Tendwa

One thing about Godbless Lema, one distinct character, this just one that his enemies don't know about, is; HE RARELY SPEAKS OR WRITES, BUT WHEN HE DOES SO, THUNDER CAN BE HEARD FROM AFAR!!!!

Godbless Lema is one of the few MPs who writes few paragraphs whose content is that of book of Revelation.

.......Ohh...and he means what he says, always has...!!!

Kati ya vichwa vichache nnavyovikubali, hiki ni kimojawapo. U hve said it all Bigirita!
 
Lema aende campaign kokote ila nae akae akijua Arusha kumedorora. Akae atulie, atulize vurugu kwa wafuasi wake afanye shughuli za maendeleo. Wabunge wenzake wa CDM tunaona wanayoyafanya yeye yako wapi? Ajue 2015 iko mlangoni inabisha hodi.......................... Hakuchagyuliwa kwenda mahakani kujibu kesi bli kuhamasisha maendeleo plz

Kwani alikwenda mwenyewe mahakamani?
 
Kwani Hamlijui jeshi la Polisi la Tz?
Wapelekeeni ushahidi kwanza, ndo wafanye kazi!!!
 
Lema amejibu!

[h=6]SALAMU TOKA KWA MH.LEMA

Leo asubuhi nimesikia habari za uzushi na majungu kutoka katika gazeti la Chama Cha Mapinduzi Uhuru pamoja na gazeti la serikali la Habari leo . Hivyo basi kilichosemwa na magezeti ya Uhuru na Habari leo ya leo tarehe 23/2/2012 ni uzushi na propaganda , Magazeti haya ya CCM yatatumika sana kipindi hiki kama yalivyotumika kule Igunga yalipojaribu kutaka kuwatenganisha watu hata kwa dini zao lakini baadae ukweli ulijulikana na ikawa aibu kwao .
Kwa zaidi ya miaka hamsini ya uhuru wa Taifa letu kutoka kwa mkoloni bado Watanzania wa Arumeru sio huru na Watanzania wote kwa ujumla bado wanaishi maisha magumu kama wakimbizi nje ya Nchi yao.
Ninafahamu wajibu wangu katika kupigania demokrasia safi ya Nchi yangu na wakati huu jimbo la Arumeru Mashariki litakuwa mfano wa mapambano hayo na nitakuwa mstari wa mbele bila hofu wala kumuogopa mtu yeyote na wa cheo chochote katika kupigania ukweli na haki.
Wajibu wangu na wa chama changu kwa sasa ni kutoa matumaini kwa watu wote wa Taifa letu , na tunazo sababu za msingi za kwenda kushinda jimbo la Arumeru na ni wito wangu kwa kila kijana wa Arumeru anayeishi mjini kuona fursa hii ni kwa ajili ya ukombozi wa Nchi yetu na sio Arumeru peke yake na hivyo kwenda kutoa elimu vijijini tulikoacha wazee wetu.
Jana nilikuwa Meru , wazee na vijana wamekataa kuburuzwa na siasa za CCM ambazo kwa miaka hamsini ya uhuru wa Nchi hii zimeshindwa kutatua matatizo yao bali kufikiri rushwa ya pesa kipindi hiki cha Kampeni ndio mahitaji yao ya Msingi.
Nimesikia Tendwa msajili wa vyama vya siasa naye ameanza kusaidia CCM kufanya propaganda chafu labda ni vyema akatambua wajibu wake na sio kuanza kufanya kazi za siasa za CCM ni vyema akajua kuwa yeyote anayeitetea uovu leo itakuwa hasara kwake au kwa familia yake kesho .
Mwisho . Ninajua macho ya Watanzania yako Arumeru mashariki , Ninawatia moyo wale mlioko mbali lakini mnapenda mabadiliko , sisi tulioko huku tutapambana kwa niaba yenu kufa na kupona kuhakikisha haki, usawa, na demokrasia vinapata thamani halisi bila uhuni wowote kufanikiwa , Msiogope pengine huwezi kabisa kufika Arumeru kusaidia ukombozi basi wewe huko uliko tuombee kwa Mwenyezi Mungu , hakika hatutakubali uhuni ,udhalimu , na Nguvu ya rushwa iwachagulie ndugu zetu wa Arumeru Mbunge , kama Mbunge mmoja wa CCM Mwigulu Nchemba alivyotamba jana pale katika Hotel ya Mount Meru kuwa pesa bado hazijaanza kumwagwa kwani ndio kwanza ziko njiani zinakuja. Hata hivyo Msiogope Udhalimu utashidwa Arumeru ““ Ni Afadhali vita inayotafuta haki na usawa kuliko Amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa Mwanadamu .
Godbless J Lema (Mb)...[/h]
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimemshukia Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, kikisema kuwa ameanza propaganda za kukibeba Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki.
Tendwa alikaririwa na vyombo vya habari akimtahadharisha Mbunge wa CHADEMA katika Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, kutokanyaga kwenye kampeni za uchaguzi huo kwa tishio la kuuawa na viongozi wa kimila (Washiri).
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika, alisema kauli ya Tendwa ni ishara ya kutumia madaraka vibaya kujaribu kuibeba CCM kwenye uchaguzi huo mdogo baada ya wananchi wa Arumeru kuonyesha wanakipenda CHADEMA na kutaka mabadiliko.
"Tendwa akae pembeni aache uchaguzi kwa vyama vya CHADEMA na CCM. Alikwenda kufanya tathmini na amelizungumzia jambo moja ambalo amelifanya propaganda, mbona hazungumzii rushwa iliyofanywa na CCM kwenye kura za maoni?" alihoji Mnyika.
Alisema wadau mbalimbali wamelalamikia vitendo vya rushwa vilivyojitokeza CCM na kwamba yeye kama msajili kuna sheria tatu ambazo zinampa mamlaka ya kuzungumzia hayo.
Alisema kuna sheria ya vyama vya siasa ambayo moja kwa moja inampa wajibu wa kuzungumzia rushwa kadhalika ile ya gharama za uchaguzi ambayo inampa mamlaka ya kufuatilia vitendo hivyo.
"Kama ana nia njema, vitendo vya rushwa ambavyo pia vinazungumzwa na wana-CCM wenyewe angevitolea kauli, kuacha hayo ni kutumia madaraka vibaya. Kuyaacha mambo ya msingi na kulizungumzia moja tu ni propaganda za kuibeba CCM," alisema
Katika hilo, Mnyika alimtaka Tendwa afanye mambo mawili; kwanza atoe ripoti ya kina ya tathmini aliyokwenda kufanya Arumeru na ijulikane wazi na pili, kwa sababu ameitaja CHADEMA awakabidhi nakala ya ripoti kamili aliyoifanya, vinginevyo watachukua hatua.
Mnyika aliwatahadharisha wananchi wa Arumeru Mashariki, kukumbuka kuwa wakati wa kampeni, viongozi wa serikali wamekuwa na kawaida ya kutumika propaganda kusaka ushindi.
"Wanataka wananchi wa Arumeru, wajifunze kilichotokea Tarime mwaka 2008, waliamua kuwa na mshikamano, wakapuuzia propaganda wakaamua kuchagua CHADEMA," alisema Mnyika.
Kwa mujibu wa Mnyika, Machi 3-4 watafanya uteuzi na si kuangalia propaganda kama za Tendwa. Hivyo kuwataka wazee wa Arumeru Mashariki kuwaunga mkono ili kazi waliyoianza mwaka 2010 ilete manufaa.

Source:Tanzania Daima

Wakuu kwani hakuna kifungu cha sheria kinachoruhusu vyama vya siasa kutokuwa na imani na msajili wa vyama?
Na kama kipo kwa nini kisitumike kutokana na maneno yake ya kuharisha maisha ya watu. Hapa tunapata picha hata mauaji yaliyotokea Igunga alikuwa anajua. CDM wakimpeleka mahakamani ninavyowajua watu wa Arusha watamshindilia huko na jinsi walivyo na hasira na CCM lazima makesi yote ya nyuma yatafufuka na yatapata sehemu ya kuwapa wananchi ripoti kwa nini watu wa Igunga, Tarime na kwingineko waliuwawa.

Tunaweza kuziba masikio lakini tujue tunayeumia ni sisi, yeye kesha maliza kama kuku anayearisha. Ikiwezekana mashitaka yasifunguliwe hapa nchini. CDM sasa tulikuwa tunamtafuta mchawi wetu tumempata, wananchi tunasubiri mtuokoe tuishi nchi yetu kwa amani sio kwa maagizo ya kuua. Inawezekana kaenda kutengeneza mtandao wa kumwangamiza Mh Lema lakini kakwama ikabidi atapike tu.
 
chadema au lema hawana wanasheria?
tendwa ni wakufungulia mashtaka,ushahidi uko wazi,kama ametumwa na wazee wa washiri yeye ni shahidi nakama ni propaganda yeye ni mtuhumiwa.
katika nchi inayodai inafuata utawala wa sheria haiwezekani mtu amtume mtu mwingine kupeleka taarifa za kumwua mtu na akaachwa hivihivi.

chadema wasiligeuze hili kuwa la kisiasa hili ni kosa na linatakiwa kuwa mahakamani.nitawashangaa sana kama wataenda kwenye kampeni huku tendwa akiwa akiwa uraini.

Mkuu naomba nikusahihishe. Tanzania haifuati utawala wa sheria. Sheria zimetungwa kuwaadhibu walalahoi, na sio kiongozi wa serikali! Tanzania inatawaliwa kwa interest ya watu fulani waliokabidhiwa dhamana ya kuongoza. Hakuna rule of law Mkuu. Ushahidi wa hili upo jinsi mambo yanavyopelekwa. Huyu Tendwa ni msajili wa vyama vya siasa, sasa inakuaje anaonekana kukibeba chama fulani? Kimsingi hatakiwi kuwa mwanachama wa chama chochote.
 
Huo ndio ushujaa na ukomavu wa kisiasa, mapambano yaendelee mpaka Demokrasia ifunguke
na kufikia percent 100% tupo karibu sana kwa pamoja tutaweza.
 
Jeshi lililo makini lingeweza kuchukulia serious hi taarifa za Tendwa, tusisibiri mpaka mauaji yatokee ndiyo wachukue hatua, na hii ndio udhaifu wa jeshi la polisi wanashughulikia reaction. Mwiteni Tendwa aeleze ni wazee gani hao na wao waitwe kwa mahojiano na karipio kali

Wewe upo TZ hii, umeyasikia ya huko Songea, wananchi wanavyomiminiwa risasi kama mvua kisa ni wauwaji ambao hawajulikani, badala yake wamejeuziwa kibao kuwa wanataka kwenda kuiba Ikulu, ha hah hah hii ndio Tanzania bana. TZ hakuna Polisi tuna Green Guard wa CCM.
 
Huo ndio ushujaa na ukomavu wa kisiasa, mapambano yaendelee mpaka Demokrasia ifunguke
na kufikia percent 100% tupo karibu sana kwa pamoja tutaweza.

"Wajibu wangu na wa chama changu kwa sasa ni kutoa matumaini
kwa watu wote wa Taifa letu , na tunazo sababu za msingi za kwenda
kushinda jimbo la Arumeru na ni wito wangu kwa kila kijana wa Arumeru
anayeishi mjini kuona fursa hii ni kwa ajili ya ukombozi wa Nchi yetu na sio
Arumeru peke yake na hivyo kwenda kutoa elimu vijijini tulikoacha wazee wetu".
quoted Hon G.Lema.

Salute!!
Ujumbe huu uwaendee Vijana wote Tanzania.
 
Naomba mtu anisaidie na summary ya ilichoandikwa hapo, nimesikia uvivu kusoma

Mkuu kwenye jukwaa la siasa huwa hatusaidiani ku summarize. huwa tunasaidiana kujadili hoja husika na kama huelewi au huna mchango unasoma kama (guest) then una log off.
 
Tendwa lazima afanye hivyo kwasababu CCM (Chai Chapati Maharage) ndio Boss wake. Ila asubiri kunyewa tu.
 
Back
Top Bottom