babayah67
JF-Expert Member
- Mar 28, 2008
- 493
- 79
Wiki mbili zilizopita nilikuwa Singida Mjini kikazi, nikiwa miongoni mwa Wanafunzi waliosoma Singida kati yaa mwaka 1980 hadi 1984 (Form I - IV) nilikuwa na hamu ya kuitembelea shule yangu, ili kuangalia mandhari yake na pia kuwasalimia walimu wangu kama wangekuwa bado wapo.
Baada ya kumaliza shughuli zangu za siku, jioni moja nilitembea kuelekea Mwenge Sekondari. Nilianza kupatwa na mshtuko mara tu nilipofika pale kwenye mawe mawili ya barabarani karibu na guest ilokuwa ikijulikana kama Victoria, au Mmassy Bakery (alokuwa akisupply mikate na matunda shuleni). Shock yenyewe ni kuwa shule siku hizi haina tena uzio uliokuwa ukizunguuka shule na kupunguza vibaka. Pamoja na hilo, siku hizi hakuna ulinzi wowote magetini, yaani geti A lili linaloingilia ofisini na madarasani, au Geti B, lile linaloingilia nyumba za walimu.
Nilijisikia kutoa machozi nilipotembelea mabwenini. Ukiingia bweni la Jamhuri, Azimio na Kujitegemea hali inatisha sana. Vitanda vibovu, kuta chafu hazijapakwa rangi nafikiri sijui toka sisi tunamaliza shule. Kwa ujumla hali ni mbaya saana. Sehemu tulizokuwa tunafulia na kuogea, siku hizi hazitumiki kabisa, maji hayatoki basi ni taabu tupu.
Nikatembelea bwalo la chakula, ambalo wakati wetu lilikuwa na meza karibu 90 na kila meza ikiwa na mabenchi mawili, sasa hivi niliona meza moja tu. Nilipowauliza wanafunzi wanakaa wapi wakati wa kula walisema wanakula wakiwa wamesimama tu. Kwa ujumla jamani hali ni mbaya saana.
Kwa wanafunzi wanaosoma pale, sitarajii matokeo yao kuwa mazuri.
NB: Namwomba Mbunge wa Singida Mjini MH. AZIM DEWJI aitazame kwa jicho la huruma shule hiyo. Ninaamini anaweza japo kuwapakia rangi ndani ya Mabweni yao vijana wale. Na kuwarekebishia japo Taa za kusomea Madarasani na bwenini.
Baada ya kumaliza shughuli zangu za siku, jioni moja nilitembea kuelekea Mwenge Sekondari. Nilianza kupatwa na mshtuko mara tu nilipofika pale kwenye mawe mawili ya barabarani karibu na guest ilokuwa ikijulikana kama Victoria, au Mmassy Bakery (alokuwa akisupply mikate na matunda shuleni). Shock yenyewe ni kuwa shule siku hizi haina tena uzio uliokuwa ukizunguuka shule na kupunguza vibaka. Pamoja na hilo, siku hizi hakuna ulinzi wowote magetini, yaani geti A lili linaloingilia ofisini na madarasani, au Geti B, lile linaloingilia nyumba za walimu.
Nilijisikia kutoa machozi nilipotembelea mabwenini. Ukiingia bweni la Jamhuri, Azimio na Kujitegemea hali inatisha sana. Vitanda vibovu, kuta chafu hazijapakwa rangi nafikiri sijui toka sisi tunamaliza shule. Kwa ujumla hali ni mbaya saana. Sehemu tulizokuwa tunafulia na kuogea, siku hizi hazitumiki kabisa, maji hayatoki basi ni taabu tupu.
Nikatembelea bwalo la chakula, ambalo wakati wetu lilikuwa na meza karibu 90 na kila meza ikiwa na mabenchi mawili, sasa hivi niliona meza moja tu. Nilipowauliza wanafunzi wanakaa wapi wakati wa kula walisema wanakula wakiwa wamesimama tu. Kwa ujumla jamani hali ni mbaya saana.
Kwa wanafunzi wanaosoma pale, sitarajii matokeo yao kuwa mazuri.
NB: Namwomba Mbunge wa Singida Mjini MH. AZIM DEWJI aitazame kwa jicho la huruma shule hiyo. Ninaamini anaweza japo kuwapakia rangi ndani ya Mabweni yao vijana wale. Na kuwarekebishia japo Taa za kusomea Madarasani na bwenini.