BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Serikali yaiwakia MwanaHalisi
Maulid Ahmed
Daily News; Wednesday,October 08, 2008 @20:03
Serikali imelitaka gazeti la MwanaHalisi kutoa sababu za kujitetea ili lisichukuliwe hatua kutokana na habari iliyoichapisha jana kuwa kuna njama za kumngoa Rais Jakaya Kikwete asiweze kugombea urais mwaka 2010.
Msemaji wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Jacob Tesha katika taarifa yake alisema kuwa agizo hilo limo katika barua iliyotumwa kwa Mhariri Mtendaji wa gazeti hilo, Saed Kubenea ambapo ametakiwa awasilishe maelezo ya kina wizarani hapo kuhusu tuhuma hizo kabla ya kesho jioni.
Katika gazeti hilo la kila wiki toleo la 118, kumeandikwa habari kuwa kuna kundi la mafisadi wakiongozwa na aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz wamejipanga kuhakikisha Rais Kikwete asigombee urais mwaka 2010.
Katika habari hiyo, mtoto wa Rais Ridhiwani anadaiwa kutumiwa na mafisadi hao katika njama hizo za kumngoa baba yake pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao wamekuwa wakishiriki kuwaweka wafuasi wao watakaosaidia kufanikisha njama hizo.
Tesha alisema kuwa kutokana na habari hiyo, serikali imesema kuwa ni ya uchochezi inayolenga kumgombanisha Rais Kikwete na viongozi wengine waandamizi wa CCM na kuleta mtafaruku katika familia yake.
Taarifa hiyo ya serikali iliwaonya baadhi ya waandishi wa habari ambao kwa makusudi wamekuwa wakiandika habari zisizo sahihi na zenye kuchochea chuki miongoni mwa jamii na kusisitiza kuwa uhuru wa habari unaishia pale unapoingilia uhuru wa mtu mwingine.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa gazeti hilo, Saed Kubenea alilieleza gazeti hili kuwa hajapokea taarifa hiyo ya serikali hadi jana jioni na siku nzima ya jana alikuwa ofisini.
Alisisitiza kuwa habari iliyoandikwa katika gazeti lake si mpya na imeshawahi kuandikwa na vyombo vingine vya habari lakini aliongezea kuwa gazeti lake limeiandika kwa undani zaidi.Hata hivyo alisema taarifa hiyo ya serikali ikija tutaipokea, tutaijadili na kuitafakari kisha tutawajibu.
Maulid Ahmed
Daily News; Wednesday,October 08, 2008 @20:03
Serikali imelitaka gazeti la MwanaHalisi kutoa sababu za kujitetea ili lisichukuliwe hatua kutokana na habari iliyoichapisha jana kuwa kuna njama za kumngoa Rais Jakaya Kikwete asiweze kugombea urais mwaka 2010.
Msemaji wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Jacob Tesha katika taarifa yake alisema kuwa agizo hilo limo katika barua iliyotumwa kwa Mhariri Mtendaji wa gazeti hilo, Saed Kubenea ambapo ametakiwa awasilishe maelezo ya kina wizarani hapo kuhusu tuhuma hizo kabla ya kesho jioni.
Katika gazeti hilo la kila wiki toleo la 118, kumeandikwa habari kuwa kuna kundi la mafisadi wakiongozwa na aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz wamejipanga kuhakikisha Rais Kikwete asigombee urais mwaka 2010.
Katika habari hiyo, mtoto wa Rais Ridhiwani anadaiwa kutumiwa na mafisadi hao katika njama hizo za kumngoa baba yake pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao wamekuwa wakishiriki kuwaweka wafuasi wao watakaosaidia kufanikisha njama hizo.
Tesha alisema kuwa kutokana na habari hiyo, serikali imesema kuwa ni ya uchochezi inayolenga kumgombanisha Rais Kikwete na viongozi wengine waandamizi wa CCM na kuleta mtafaruku katika familia yake.
Taarifa hiyo ya serikali iliwaonya baadhi ya waandishi wa habari ambao kwa makusudi wamekuwa wakiandika habari zisizo sahihi na zenye kuchochea chuki miongoni mwa jamii na kusisitiza kuwa uhuru wa habari unaishia pale unapoingilia uhuru wa mtu mwingine.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa gazeti hilo, Saed Kubenea alilieleza gazeti hili kuwa hajapokea taarifa hiyo ya serikali hadi jana jioni na siku nzima ya jana alikuwa ofisini.
Alisisitiza kuwa habari iliyoandikwa katika gazeti lake si mpya na imeshawahi kuandikwa na vyombo vingine vya habari lakini aliongezea kuwa gazeti lake limeiandika kwa undani zaidi.Hata hivyo alisema taarifa hiyo ya serikali ikija tutaipokea, tutaijadili na kuitafakari kisha tutawajibu.