Mgomo wa wanafunzi halali kweli???

ELIESKIA

Senior Member
Jul 21, 2011
120
15
Hivi ni mimi peke yangu au kuna wengine wanaodhani kwamba wanafunzi nao kuandamana ni ujinga tu...


MAANDAMANO.JPG
SERIKALI imelazimika kutumia Jeshi la Polisi katika harakati zake za kudhibiti mgomo wa walimu ambao jana uliingia katika siku yake ya pili, huku maandamano ya wanafunzi yakiendelea katika baadhi ya maeneo na Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kulazimika kuwadhibiti.

Taarifa kutoka mikoa kadhaa zinaonyesha kuwa polisi waliwakamata viongozi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), ngazi za mikoa na wilaya, huku baadhi yao wakifikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuchochea mgomo ambao Serikali tayari imesema kuwa ni haramu.

Kukamatwa kwa viongozi hao kulikwenda sambamba na tamko la baadhi ya wakuu wa mikoa na baadhi ya makamanda wa polisi ambao walionya kwamba wangewachukulia hatua za kisheria walimu ambao wangeendelea kugoma.

Wakati Serikali ikichukua hatua hiyo, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), limeitaka Serikali kuacha kujitetea katika suala hilo na kulipa madai ya wanataaluma hao wa sekta ya elimu.

Mkoani Dar es Salaam, FFU walitawanya maandamano ya wanafunzi katika eneo la Kunduchi, Kinondoni na kuwakamata baadhi yao. Waliandamana kwa madai ya kudai haki yao ya kufundishwa.
Kundi kubwa la wanafunzi waliodaiwa kwamba walikuwa wakitoka katika shule mbalimbali za Manispaa ya Kinondoni waliandamana katika maeneo ya Mbezi Machimbo, huku askari wa FFU wakijaribu kuwazuia na kuwaelekeza kurudi nyumbani.

NOTE: watoto ni haki yao kuendelezwa na haki huwa haiombwi inadaiwa . ni nani amesimama kuwatetea? wenyewe wameamua kujitetea
 
Hivi ni mimi peke yangu au kuna wengine wanaodhani kwamba wanafunzi nao kuandamana ni ujinga tu...
Wanafunzi siyo wajinga bali walimu waliogoma ndiyo wajinga, Iweje watumie watoto wadogo hao kufikisha ujumbe wao? kwani wameshindwa kusimama wao kama wao kudai haki zao kama kweli ni madai ya msingi? Inaonekana ni jinsi gani walivyo mambumbumbu au madai yao siyo halali
 
Wanafunzi siyo wajinga bali walimu waliogoma ndiyo wajinga, Iweje watumie watoto wadogo hao kufikisha ujumbe wao? kwani wameshindwa kusimama wao kama wao kudai haki zao kama kweli ni madai ya msingi? Inaonekana ni jinsi gani walivyo mambumbumbu au madai yao siyo halali

Wewe thatha inaonekana reasoning na thinking capacity yako ndogo sana mwl mbumbumbu mjinga? Hata shule yaelekea ulienda kuattend tu. Wanafunzi wa cku hizi sio wale wa enzi zako maandamano washayazoea kwani wanaona hata kaka zao tuliopo vyuoni tunaandamana madr wanaandamana why not them sasa eti watoto wadogo wanatumiwa! Walimu waliogoma wapo nyumbani maloyalists tu ndo wako makazini ina maana hawajagoma sasa wao ndo wanawatumia watoto? Think big n outside the box!


Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Mi nafikiri hakuna mwalimu ambae anamhusisha mwanafunzi kwenye mgomo zaidi ya
mwanafunzi huyo kuwa na muamko wa kiuanaharakati na hivyo kusababisha
yeye mwenyewe kudai haki ya kufundishwa kwa kuandamana na la sivyo itakua
ni mbinu ya kuchafua mgomo wa waalimu ambao hauhusishi mwanafunz inagwaje yeye ni muathirika
moja kwa moja
 
Walimu kwakweli wanasikitisha sana na mipango yao. mgomo wenyewe na uzugaji mbaya sana wanawahusisha watoto. waqo wanajificha. fuaten majadiliano mgomo ni mgumu na hautekelezeki. Afu waacheni watoto wetu maana wao sio wasemaji wenu.
 
Sio halali maana suala lao lipo mahakami kwa hiyo ni bora wasiingilie huo mhimili wa serikali waende tu madarasani
 
Back
Top Bottom