Vyuo vipi unaongelea Boss, ni hivi vilivyong'olewa meno na kuwa " toothless au? Unazungumzia vyuo hivi ambavyo vimeshindwa ku- claim hata ile " university autonomy" yake?.
Ni hivi ambavyo maprofesa wake wanawafundisha wanafunzi na kuwatunuku degree kisha wakipewa viti vyeusi na vipaza sauti na wanasiasa wanasema wasomi wake hawaajiriki?...
Ni hivi Vyuo ambavyo miaka ya 2015 walifanya tafiti wakabaini kuwa wasomi wengi pamoja na kuwa na stadi ngumu "hard skills" kama vyeti na matokeo mazuri kitaaluma " good G.P.A hawana stadi laini " soft skills" ambazo ni muhimu zaidi kazini?
Teh!..ni hivi vilivyotunga Sheria mbovu ya kuwabana wahadhiri wake kufikia ngazi za U-profesa halafu vinawastafisha mapema na kuanza kuwatafuta tena kama "emeritus professors"?
Ni hivi ambavyo wasilisho la andiko la Profesa "Inaugural lectures" hufanyika kama masika ya jangwani?. Aiseee.....au..ni...
Ni vyuo hivi ambavyo maprofesa wake wakipewa ulaji wa kisiasa wanashukuru na kusema "wametoka mavumbini" Profesa anapaita Chuo mavumbini kweli?....tena Chuo kikongwe na kikubwa Afrika ,Bigiii mbona sikuelewi unazungumzia vyuo vipi?
Ni hivi ambavyo umoja wa wahadhiri unachukuliwa kama jukwaa la harakati za kisiasa na kuchukiwa, kiasi cha kutoa matamko yanayopungana na utawala?.. Unazungumzia Vyuo vipi Bigii?....
Hivi ambavyo wahadhiri wake badala ya kujitahidi kuwa sehemu ya kusukuma mabadiliko ya kijamii, kisiasa na kiuchumi wanakimbizana kusifia kila kitu ili kuandaliwa vyeo vya kisiasa?..
Unazungumzia vyuo vipi Bigii?.. Au hukumsika yule Profesa aliyesema degree holder warudi VETA?
My take; Vyuo hivi kwanza vinapaswa ku- claim autonomy yake kwa walioipoka kwanza ndiyo waje na masuala mengine. Tunafahamu Vyuo vina " code of professionalism na code of ethics" wasimamie hayo kwanza .