Mgomo wa madaktari - Updates

jigoku

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2011
Posts
2,411
Reaction score
733
Habari nilizozipokea sasa hivi kwa njia ya SMS kutoka kwa doctor mmoja pale Mhimbili zinasema hivi,nanukuu,"Hii ya sasa ni bab kubwa responce ni 100% MPAKA EMERGENCY,intern ndio wamemaliza kikao chao cha kupeana moyo na specialist ndio wanaanza Russian culture nw..together we can make it" mwisho wa kunukuu sms niliyoipokea.

My take; hivi serikali ina shindana na madaktari kwa ajili ya maslahi ya kisiasa? au inatakiwa kulinda afya za wananchi wake?
Maana kama mawaziri wamelalamikiwa na ni kweli wameshindwa kuwajibika kwa nini waendelee kuwepo hapo?na je inawezekanaje kupokea malalamiko ambayo kimsingi wao ndio wanalalamikiwa na kisha wakayafanyia kazi?
Nawasilisha wadau
 
Hiyo imekaa vizuri,hadi kieleweke!!;
 
kwa wale msioamini naomba mtembelee muhimbili.habari zinasema huu mgomo wa leo umezidi ule wa kwanza.madaktari wote wamerespond,specialist wanaendelea na kikao.
 
Dr Wangu wa Muhimbili anasima

"" mgomo hakuna watu wanaendelea na kazi kama kawaida vikao bado vinaendelea"" mwisho wa kunukuu

Sasa tumuamini Doctor wa wapi??? maaana mgomo hakuna:juggle:
 

ahadi unaita dai jipya?
 
Siungi mkono mgomo kwa sababu najua madhara yatakayo tokea kwa masikini wasio na hatia lakini pia nadhani ni fundisho kwa viongozi wetu ambao wanafanya kazi kwa mazoea na kutotaka kushughurikia matatizo mpaka maafa yatokee ndio wanakurupuka. Hofu yangu ni kwamba suala la madaktari likiisha sector nyingine nayo itatangaza mgomo maana walimu wapya walioajiriwa hivi karibuni kuna sehemu nyingi tu za nchi hawajalipwa stahili zao mpaka wengine wameamua kurudi nyumbani.
 
Dr Wangu wa Muhimbili anasima

"" mgomo hakuna watu wanaendelea na kazi kama kawaida vikao bado vinaendelea"" mwisho wa kunukuu

Sasa tumuamini Doctor wa wapi??? maaana mgomo hakuna:juggle:

nenda muhimbili
 

Na nani achukuliwe hatua kutokana na vifo vya wagonjwa vinavyotokea kila siku kutokana na uzembe wa watendaji serikalini kwa matumizi mabaya ya fedha (na hivyo kukosa madawa na vifaa muhimu vya kufanyia kazi), kununua madawa yaliyoisha muda wake na mis-allocation of resources?
 

Hizo ni porojo tu, watabana wataachia kwa kuwa wengi wanafuata mkumbo wa frustrated individuals ambao they have nothing to lose
 
uwaue madaktari? halafu utawatibu wananchi kwa masaburi yako? sitashangaa ukini ndambia kuwa unafanay kazi ukulu. sishangai kabisa ndio type ya watu mnaoongoza nchi
 
Wapi Vimon na Dr. Clinton watupe updates.
 
Hakuna lalamiko jipya labda tu hujaelewa ni nini kilizungumzwa wakati wa mkutano wa madaktari na Pinda na kusimamishwa kazi katibu mkuu na mganga mkuu,pitia huko na utaona kuwa kila kitu kinaenda kama kilivyopangwa na napenda ujue kuwa taaluma ya udaktari ni nyeti sana sio kila mtu anaweza kwenda kama ilivyo ualimu(siwashushii heshima walimu la hasha)
 


Jana nilikwambia kuwa safari hii mtakoma....mgomo uko pale pale
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…