"....Silaha ya Mnyonge ni umoja...!Wahadhiri wa Chuo Kikuu cha DSM wameamua kuanza mgomo usiokua na kikomo kupinga mafao duni pamoja na madai mengine. Kazi imebaki kwetu wafanyakazi ifikapo Mei tano kumfunga paka kengele.
Wahadhiri wa Chuo Kikuu cha DSM wameamua kuanza mgomo usiokua na kikomo kupinga mafao duni pamoja na madai mengine. Kazi imebaki kwetu wafanyakazi ifikapo Mei tano kumfunga paka kengele.
Tuombe MUNGU nchi isije ikasimama baada ya Mei 5.
Kazi sana hii Tanzania yetu, kama Mhadhiri anagoma eti mshahara mdogo je yule Karani masjala pale Wizara ya Uvuvi si itakuwa balaa. Mungu ibariki Tazania.
Mkuu sina uhakika umetumia vigezo gani ili kuweza kuwalinganisha mwenye haki ya kugoma kati ya mhadhiri na karani wa masijala. Ungewatendea haki iwapo ungetumia vigezo mfano muda wa kufanya kazi, aina ya kazi, ukubwa wa kazi, kiasi cha mshahara na vigezo vingine ili uweze kufikia hitimisho ya yupi anastahili au asiyestahili kugoma.