Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
sababu kubwa ya kujitoa ni kuwa chama makao makuu kimeshindwa kutoa fungu la kumwezesha kufanya kampeini badala yake amekuwa akitumia fedha zake
baada ya kupata habari kuwa undp itatoa fedha za kwa ajili ya gharama mbali mbali za vyama kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, ndipo baaadhi ya vyama vikajitutumua kusimamisha wagombea katika nafasi mbali mbali; na baadhi ya wagombe nao wakajitokeza kugombea kupitia vyama mbali mbali. Lengo ikiwa ni kupata fedha zitakazotolewa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa 2010. Ndio maana mwaka huu kama vile kuna utitiri wa wagombea.
Kutokana na malalamiko makubwa kutoka kwa mawakalawa vyama mbali mbali katika chaguzi zilizopita ya kutolipwa baada ya matokeo kutangazwa, tume ya uchaguzi imeamua kuwa itawalipa mawakala yenyewe kwa kutumia fedha zitakazotolewa.
Hivyo vyama vilivyofuata fedha na wagombea waliofuata fedha baada ya kusikia hivyo wameishia nguvu na kukata tamaa. Baadhi ya vyama tayari vimeanza kupigia debe vyama vingine, wagombea kujitoa n.k.
Mapambanouya ukombozi hayataki watu wenye chembe chembe za ufisadi mioyoni mwao.
Tukaze buti wachache watakaobakia!!!!! Mabadiliko yoyote hufanikishwa na wachache kwa maslahi ya wengi.