UKAWA kuuza jimbo la Nkenge kwa Dr. Kamala, kuweka mgombea asiyejulikana

Ta Muganyizi

R I P
Oct 19, 2010
5,361
2,734
Naongea haya nikiwa na machungu sana baada ya kuona fitina zinazoendelea kwenye jimbo la Nkenge ambapo baada ya kuondolewa Assumpter Mshama na nafasi yake kuchukuliwa na Dr. Kamala hujuma za ajabu zimeanza.

Inaelekea UKAWA wameamua kuwa mgombea wa UKAWA atakayewania jimbo hilo ni kutoka NCCR – Mageuzi. Sina Ugomvi na NCCR ila ukweli ni kuwa NCCR huku haipo. Mgombea kutoka CHADEMA ndiye anayejulikana bwana Valerian Rugarabamu. Huyu kashiriki kuanzisha misingi na matawi ya CDM kila kata.

Pia maajabu ni kuwa, NCCR katika uchaguzi ujao haina mgombea hata mmoja katika kata 20 za Missenyi, wakati katika kata zote hizo CHADEMA imesimamisha wagombea wa Udiwani. Kinachonishangaza wanaoshangilia UKAWA kumsimamisha mgombea kupitia NCCR – Mageuzi ni watu wa CCM.

Habari nyingine zinadai kuwa iwapo huyo mama wa NCCR atasimamishwa, mwisho wa siku atajiondoa na bwana Kamala apite kiulaini maana huyo mama anaweza kupewa cash nzuri. Huyu Kamanda anayejulikana, aliyepigana kuanzisha matawi na misingi ya chama, akashinda kwenye kura za maoni, leo hii eti ampishe mwingine basi nafuu hata angekuwa ni ndani ya chama lakini chama kingine ambacho hakina hata mgombea mmoja ngazi ya kata?????!!!!!

Pamoja na hayo, huyu bwana wa CDM anaambiwa basi ahamie NCCR!!!! Ghafla!! Hii haiwezekani. Ninachotaka kuwaambia CHADEMA kama mmeona maeneo yote ndo kuna watanzania wenye uchungu na nchi yao, mkaona Kagera ndo mkoa wa kufanyia majaribio na experiment kwamba tupate mabadiliko au tusipate basi to hell with us, itatugharimu. Msiwachezee wananchi(umma) kabisa.

Kwa sababu hizi CHADEMA na Ukawa kwa ujumla, gawaneni majimbo lakini pasipo kutukwaza sisi wananchama kwa kuleta kitu ambacho hata hakipo. Sehemu mnapoona Chama flani kinakubalika wekeni mgombea wa chama husika. Ni sawa muda huu kule kwa akina Kafulila mkamsimamishe mgombea kutoka chama cha NLD au kule kwa akina Joshua Nassari mpeleke CUF.

Fanyeni changes ambazo hazina direct confusion kama ya Babu Duni kuwa mgombea mwenza.
Tambueni katika Sensa ya 2012 Tanzania, Kagera inashika nafasi ya (nne 4) kwa wingi wa watu ikitanguliwa na Dar, Mwanza na Mbeya. Hivo acheni utani aisee ina watu million (2.46) Kama mpango wa hujuma ni wa CCM, basi kuweni makini.
 
Umeeleweka Kamanda, nadhani wahusika watakuwa wamekusikia na watalifanyia kazi kwa maslahi mapana ya mustakabali wetu wa kuking'oa chama cha maombolezo madarakani.
 
Jambo hili limetokea hata Geita mjini jimbo wamepewa CUF wakati CDM ndo ina nguvu imefika mahali watu wamechanganyikiwa hawajui wafanye nini maana CUF ni kama haipo walichokiamua wanachama ni kutopiga kura au kumuunga mwana cdm mwenzao popoye atakapokwenda hasa ACT jambo hili sio zuri kwa afya ya chama
 
Umeeleweka Kamanda, nadhani wahusika watakuwa wamekusikia na watalifanyia kazi kwa maslahi mapana ya mustakabali wetu wa kuking'oa chama cha maombolezo madarakani.

Kama watu wanahama CCM kuja kwetu sababu ni watenda haki, basi tuwasababishie tena tulionao kuwasababishia pa kwenda.

cc. Tumaini Makene hebu wapelekee huu ujumbe
 
Last edited by a moderator:
Jambo hili limetokea hata Geita mjini jimbo wamepewa CUF wakati CDM ndo ina nguvu imefika mahali watu wamechanganyikiwa hawajui wafanye nini maana CUF ni kama haipo walichokiamua wanachama ni kutopiga kura au kumuunga mwana cdm mwenzao popoye atakapokwenda hasa ACT jambo hili sio zuri kwa afya ya chama

Hivi wanadedicate majimbo kwa spellings au wanaangalia hali halisi iliyopo??? Huu utakuwa ni ujinga sasa, wanacheza na akili za wananchi.
 
Ni kama tu Jimbo la Segerea...kule Chadema ndio inawika sana,na kiukweli ndio chama chenye nguvu kuliko vingine ndani ya UKAWA
Lakini mgombea wake ndani ya Chadema anayesimama Segerea hafaamiki kabisa,hana harakati wala hata wananchi hawamuelewi kabisa kabisa...Hivi kwanini huku asingekaa Julius Mtatiro?ambaye anafahamika na ni maarufu?2010 tuliona kazi yake Jimbo la Ubungo..hapa UKAWA watazame upya....#Mtatiro tunamuhitaji sana Bungeni
 
Last edited by a moderator:
Nmependa topic yako mdau,,,watakua na sababu tuwaamin,hafu kumbuka CDM na NCCR zpo UKAWA,,,kama imefkia mpaka hatua ya kumwambia mgombea ahamie NCCR jamaa anakubalka na nadhani wanachi watampa kura popote atapokuwa
 
Ni kama tu Jimbo la Segerea...kule Chadema ndio inawika sana,na kiukweli ndio chama chenye nguvu kuliko vingine ndani ya UKAWA
Lakini mgombea wake ndani ya Chadema anayesimama Segerea hafaamiki kabisa,hana harakati wala hata wananchi hawamuelewi kabisa kabisa...Hivi kwanini huku asingekaa Julius Mtatiro?ambaye anafahamika na ni maarufu?2010 tuliona kazi yake Jimbo la Ubungo..hapa UKAWA watazame upya....#Mtatiro tunamuhitaji sana Bungeni

Mtatiro alshakubali kupsha mgombea wa CHADEMA,chama unachosema kinakubalika ndani ya UKAWA,japokuwa CUF ya Mtatiro inakubalka pia...Anyway,UKAWA fanyeni kaz kwa umakini na umoja,,,wananchi wanaamini ktk umoja wenu...tutawaunga mkono ktk maamuz mtakayofkia kwa umoja wenu,hatutaangalia umaarufu wa mtu mmoja.
 
Last edited by a moderator:
Nmependa topic yako mdau,,,watakua na sababu tuwaamin,hafu kumbuka CDM na NCCR zpo UKAWA,,,kama imefkia mpaka hatua ya kumwambia mgombea ahamie NCCR jamaa anakubalka na nadhani wanachi watampa kura popote atapokuwa

Kiongozi kata 20 hamna mgombea hata mmoja wa Udiwani, kwa hiyo na madiwani woooote wahamie NCCR sasa hapo utakuwa utani kiongozi.
 
Lazima tukubaliane kuwa ndani ya UKAWA kuna manufaa na hasara kwa vyama husika, ila mtoa hoja nakushagaa October tunpigia wagombea wa UKAWA sasa limeuzwaje jimbo ?
 
Naongea haya nikiwa na machungu sana baada ya kuona fitina zinazoendelea kwenye jimbo la Nkenge ambapo baada ya kuondolewa Assumpter Mshama na nafasi yake kuchukuliwa na Dr. Kamala hujuma za ajabu zimeanza.

Inaelekea UKAWA wameamua kuwa mgombea wa UKAWA atakayewania jimbo hilo ni kutoka NCCR – Mageuzi. Sina Ugomvi na NCCR ila ukweli ni kuwa NCCR huku haipo. Mgombea kutoka CHADEMA ndiye anayejulikana bwana Valerian Rugarabamu. Huyu kashiriki kuanzisha misingi na matawi ya CDM kila kata.

Pia maajabu ni kuwa, NCCR katika uchaguzi ujao haina mgombea hata mmoja katika kata 20 za Missenyi, wakati katika kata zote hizo CHADEMA imesimamisha wagombea wa Udiwani. Kinachonishangaza wanaoshangilia UKAWA kumsimamisha mgombea kupitia NCCR – Mageuzi ni watu wa CCM.

Habari nyingine zinadai kuwa iwapo huyo mama wa NCCR atasimamishwa, mwisho wa siku atajiondoa na bwana Kamala apite kiulaini maana huyo mama anaweza kupewa cash nzuri. Huyu Kamanda anayejulikana, aliyepigana kuanzisha matawi na misingi ya chama, akashinda kwenye kura za maoni, leo hii eti ampishe mwingine basi nafuu hata angekuwa ni ndani ya chama lakini chama kingine ambacho hakina hata mgombea mmoja ngazi ya kata?????!!!!!

Pamoja na hayo, huyu bwana wa CDM anaambiwa basi ahamie NCCR!!!! Ghafla!! Hii haiwezekani. Ninachotaka kuwaambia CHADEMA kama mmeona maeneo yote ndo kuna watanzania wenye uchungu na nchi yao, mkaona Kagera ndo mkoa wa kufanyia majaribio na experiment kwamba tupate mabadiliko au tusipate basi to hell with us, itatugharimu. Msiwachezee wananchi(umma) kabisa.

Kwa sababu hizi CHADEMA na Ukawa kwa ujumla, gawaneni majimbo lakini pasipo kutukwaza sisi wananchama kwa kuleta kitu ambacho hata hakipo. Sehemu mnapoona Chama flani kinakubalika wekeni mgombea wa chama husika. Ni sawa muda huu kule kwa akina Kafulila mkamsimamishe mgombea kutoka chama cha NLD au kule kwa akina Joshua Nassari mpeleke CUF.

Fanyeni changes ambazo hazina direct confusion kama ya Babu Duni kuwa mgombea mwenza.
Tambueni katika Sensa ya 2012 Tanzania, Kagera inashika nafasi ya (nne 4) kwa wingi wa watu ikitanguliwa na Dar, Mwanza na Mbeya. Hivo acheni utani aisee ina watu million (2.46) Kama mpango wa hujuma ni wa CCM, basi kuweni makini.
Tatizo lipo wapi si atapigiwa kura na Ukawa ndiyo maana ya ushirikiano.
 
Lazima tukubaliane kuwa ndani ya UKAWA kuna manufaa na hasara kwa vyama husika, ila mtoa hoja nakushagaa October tunpigia wagombea wa UKAWA sasa limeuzwaje jimbo ?

Soma vizuri.....nasema majimbo yasigawiwe kwa kutumia Spelling bali waangalie hali halisi ya chama kinachokubalika pale. Kama ingekuwa vyama viwili vimesimama side by side basi sawa lakini kimoja ni invisible!!!
 
Tatizo lipo wapi si atapigiwa kura na Ukawa ndiyo maana ya ushirikiano.

Weka concept ya UKAWA i match na realities. Sasa hata Ofisi za Chama hazipo walau kwenye kata 3 kati ya 20 zilizoko mahali. Na kwa hali iliyopo CCM wapo wanashangilia. Pia usigeneralize hoja yangu...nimekuwa specific kwa eneo husika........concept ya ushirikiano naikubali 100% lakini lazima iangalie eneo husika.
 
Haya nayo majambo. Hivi zimebaki siku ngapi kurejesha fomu NEC? Ninakna mihemko ya Lowassa lakini hatusikii wagombea wa ububge wakitangazwa?
 
Jambo hili limetokea hata Geita mjini jimbo wamepewa CUF wakati CDM ndo ina nguvu imefika mahali watu wamechanganyikiwa hawajui wafanye nini maana CUF ni kama haipo walichokiamua wanachama ni kutopiga kura au kumuunga mwana cdm mwenzao popoye atakapokwenda hasa ACT jambo hili sio zuri kwa afya ya chama

Hoja yako ni hatari sana kwa mshikamano ndani ya ukawa
 
Pro-Chadema wanataka kila sehemu wao ndiyo wasimamishe wagombea ubunge sasa huu UKAWA una maana gani, CUF wamepewa majibu 35, NCCR Mageuzi wamepewa majimbo 15, NLD wamepewa majimbo 5, yalibakia yote wamepewa Chadema bado mnataka kuwapora hata haya mliowapa.
 
Pro-Chadema wanataka kila sehemu wao ndiyo wasimamishe wagombea ubunge sasa huu UKAWA una maana gani, CUF wamepewa majibu 35, NCCR Mageuzi wamepewa majimbo 15, NLD wamepewa majimbo 5, yalibakia yote wamepewa Chadema bado mnataka kuwapora hata haya mliowapa.

Usigeneralize issue.....angalia hali halisi ya nani anakubalika na nyie lengo lenu sie tujichanganye ili mpete kilaini.....itakuwa ngumu.
 
Back
Top Bottom