BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,118
JF SUMMARY
Jeshi la Polisi linamshikilia Sabihi Mpando, Mkazi wa Chipuputa kwa tuhuma za kumfanyia Ukatili wa Kingono Mgonjwa mwenye mwenye miaka 17 aliyekuwa akimtibu wakiwa Makaburini.
Kaimu Kamanda wa Polisi, Hamis Ramadhani, amesema, Mganga alimlaghai mwathirika na kwenda naye eneo la Makaburi, wakiwa hapo alimwingilia kimwili kinguvu huku akidai anampa Matibabu.
Mtuhumiwa yuko Mahabusu kwaajili ya Mahojiano zaidi ambapo Upelelezi ukikamilka atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
==============
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara likimshikilia mtu mmoja ambaye ni mganga wa kienyeji kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka 17 aliyekuwa akimtibu katika makaburi.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 24, 2023, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Hamis Ramadhani amesema mtuhumiwa alifanya kitendo hicho katika eneo la Mingano Makaburini na kumsababishia maumivu makali sehemu za siri.
Amesema kuwa mnamo Februari 23, 2023 nyakati za usiku, Sabihi Mpando miaka (41) ambaye ni mganga wa kienyeji na mkazi wa Chipuputa alimbaka binti huyo.
“Tukio hilo lilitokea wakiwa katika makaburi ya Mingano na mbinu iliyotumika ni kumlagai mwathiriwa na kwenda naye maeneo ya Makaburi kwa ajili ya kumpa matibabu, kisha kumwingilia kimwili huku akimweleza kuwa ni tiba,” amesema.
Amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa na yupo mahabusu kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo, ambapo upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma.
Katika tukio linguine Jeshi la polisi linafanya uchunguzi wa tukio la mauaji ya mwanamke aliyejulikana kwa jina la Ziada Jafari Kondo (40) mkazi wa Matanki.
“Tukio hili liligundulika mnamo Februari 22 majira ya saa sita usiku huko mtaa wa Wapiwapi “A” Masasi, ambapo alikutwa ameuwawa na watu wasiofahamika wasiofahamika,” amesema.
Amesema uchunguzi wa kitabibu na daktari ulibaini kuwa chanzo cha kifo cha marehemu ni kukosa hewa baada ya kumkaba koo na kunyimwa pumzi.
MWANANCHI