Mganga Mkuu wilaya ya Moshi Mjini afariki dunia akiwa guest house

Quimica

JF-Expert Member
Feb 21, 2018
1,029
1,254
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Moshi (DMO) mkoani Kilimanjaro, Dk Alex Kazula amekutwa amefariki dunia kwenye nyumba ya kulala wageni 'gesti' huku kifo chake kikigubikwa na utata.

Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kisare Makori amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mwili wa Dk Kazula ulikutwa jana Oktoba 9, 2023 kwenye moja ya nyumba ya kulala wageni akiwa ameshafariki dunia.

Amesema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama wanachunguza kifo cha daktari huyo ili kujua chanzo chake.

Kwa upande mwingine, Kamanda wa Polisi Mko wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema wanashikiliwa wanawake wawili kwa kukutwa na simu za marehemu.


Chanzo: Mwananchi
 
Ngono, ngono, ngono....
Matatizo ya vijana kupenda umalaya na kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume matokeo yake huwa hayo.
Jamaa kanywa masuper shaft, kachukua mademu wawili kawaingiza guest, moyo umezidiwa kusukuma damu kwa sababu ya athari za madawa ya nguvu za kiume, jamaa kapoteza fahamu na hakuna msaada wa haraka, kikichofuata ni mauti.

Young man, Doctor mkuu wa wilaya katangulia kaburini.
 
Back
Top Bottom