Mfugale amuokoa Kamwelwe kutumbuliwa

Mfugale amuokoa Kamwelwe kutumbuliwa

Real Patriotist

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2016
Posts
296
Reaction score
698
Kilichotokea muda mfupi katika ukaguzi wa rais kwenye kalavati la Kayegeya linalounganisha barabara ya Morogoro na Dodoma ambalo hivi siku za karibuni limekwenda na maji hivyo kupelekea serikali kuagiza kutengenezwa daraja eneo hilo.

Kwa kweli usumbufu kwa wasafiri na wasafarishaji wa mizigo umekuwa ni mkubwa sana ukizingatia hiyo ni barabara kuu inayopitisha abiria na mizigo mingi ya ndani na nje ya nchi kwa majirani zetu kama vile Uganda, Rwanda, Burundi, DRC, Zambia, Malawi n.k

Leo Mh. Rais Magufuli akipita maeneo hayo amekagua ujenzi unaoendelea hapo wa daraja ambalo nalo lilienda na maji. Rais amekasirishwa sana na maelezo aliyokuwa anapewa na watendaji wake akiwemo Waziri wa ujenzi na uchukuzi ambaye amekiri makosa na kuomba msamaha wa wazi kwa rais.

Kufuatia hali ya watendaji wale wa Wizara na TANROADS kutokuwa na majibu ya kumridhisha rais, binafsi nimemuona rais akitafakari kwa kina kuona ni hatua gani stahiki ambayo angeweza kuchukua dhidi ya watendaji hao.

Ametafakari kwa muda alipokosa cha kuamua ikabidi auze mchezo kwa wananchi waamue nini afanye ambapo wananchi wamesema awasamehe tu, ila mheshimiwa rais ameagiza kusimamishwa kazi wahandisi takribani 13 wa TANROADS na uchunguzi ufanyike dhidi yao.

Kwa muonekano aliokuwa nao rais alitaka kumtumbua waziri na safu ya maofisa wa TANROADS hasa meneja wa mkoa wa Morogoro lakini akaona anaweza kumtumbua waziri na akamuacha CE wa TANROADS ambaye yeye mwenyewe amekiri laivu ni kutokana na kuguswa na kazi zake anazozifanya zinamkosha.

Kwa Leo ni hilo tu limemuokoa Eng. Kamwelwe kutumbuliwa lakini pia tukumbuke mahusiano makubwa yaliyopo kati ya boss huyo wa TANROADS na Rais pasi na shaka ndio yameathiri maamuzi ya mheshimiwa rais hivyo kuishia kutoa onyo kwa Mfugale na Kamwelwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ni mwendelezo wa mabadiliko Chanya kwa rais Magufuli. Kila siku nawaeleza watu humu kuwa this man is changing for the better.

Ule Utumbuaji wa papara sasa basi.
Je, inawezekana huu ndio mwisho wa utumbuaji wa papara na kukurupuka?! Mkuu kutumbuliwa soon!

P
Mkuu paskal hivi leo nikuulize mbele ya hadhara ya Jf
Wewe ni mwanaharakati wa ccm au chadema au neutral maana ukija kwa chadema huwa unaponda sana ccm na sera zake,ukija tena chadema huwa unawaponda...

Wewe ni mtu gani?
Mwana siasa mlengwa gani?
Sitaki ku tag mada zako hapa ukinilazim nifungue uzi nitafungua ila hebu tufahamishe hapa mkuu..
Naheshim maoni yako
 
Magufuli angekuwa kituko cha ajabu kama angemtumbua Waziri Kamwele halafu amuache Mfugale. Na wala sioni ni kwa jinsi gani Mfugale kamwokoa Kamwele. Wanaosimamia ujenzi wa hizi barabara ni TANROADS, sasa waziri angekuwa na kosa gani?

Hata kama TANROADS iko chini ya Ujenzi lakini kwa kiasi kikubwa sana inajitegemea. Waajiriwa wake sio wa wizara kwa hiyo hawapo chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Waziri wa Ujenzi
 
Kilichotokea muda mfupi katika ukaguzi wa rais kwenye kalavati la Kayegeya linalounganisha barabara ya Morogoro na Dodoma ambalo hivi siku za karibuni limekwenda na maji hivyo kupelekea serikali kuagiza kutengenezwa daraja eneo hilo.

Kwa kweli usumbufu kwa wasafiri na wasafarishaji wa mizigo umekuwa ni mkubwa sana ukizingatia hiyo ni barabara kuu inayopitisha abiria na mizigo mingi ya ndani na nje ya nchi kwa majirani zetu kama vile Uganda, Rwanda, Burundi, DRC, Zambia, Malawi n.k

Leo Mh. Rais Magufuli akipita maeneo hayo amekagua ujenzi unaoendelea hapo wa daraja ambalo nalo lilienda na maji. Rais amekasirishwa sana na maelezo aliyokuwa anapewa na watendaji wake akiwemo Waziri wa ujenzi na uchukuzi ambaye amekiri makosa na kuomba msamaha wa wazi kwa rais.

Kufuatia hali ya watendaji wale wa Wizara na TANROADS kutokuwa na majibu ya kumridhisha rais, binafsi nimemuona rais akitafakari kwa kina kuona ni hatua gani stahiki ambayo angeweza kuchukua dhidi ya watendaji hao.

Ametafakari kwa muda alipokosa cha kuamua ikabidi auze mchezo kwa wananchi waamue nini afanye ambapo wananchi wamesema awasamehe tu, ila mheshimiwa rais ameagiza kusimamishwa kazi wahandisi takribani 13 wa TANROADS na uchunguzi ufanyike dhidi yao.

Kwa muonekano aliokuwa nao rais alitaka kumtumbua waziri na safu ya maofisa wa TANROADS hasa meneja wa mkoa wa Morogoro lakini akaona anaweza kumtumbua waziri na akamuacha CE wa TANROADS ambaye yeye mwenyewe amekiri laivu ni kutokana na kuguswa na kazi zake anazozifanya zinamkosha.

Kwa Leo ni hilo tu limemuokoa Eng. Kamwelwe kutumbuliwa lakini pia tukumbuke mahusiano makubwa yaliyopo kati ya boss huyo wa TANROADS na Rais pasi na shaka ndio yameathiri maamuzi ya mheshimiwa rais hivyo kuishia kutoa onyo kwa Mfugale na Kamwelwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmmmmhh mpaka magari ya Zambia na Malawi yanapitia hapo?
 
Back
Top Bottom