Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha, linamshikilia na kumhoji anayedaiwa kuwa ni mfuasi wa Chadema, Prosper Mfinanga (40), mkazi wa Kijenge kwa tuhuma za kutembea na bango lenye maandishi yanayodaiwa kuwa ya uchochezi na uvunjifu wa amani.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa, alisema jeshi hilo linamshikilia mfuasi huyo tangu Juni 5, mwaka huu.
Alisema mtuhumiwa huyo alikutwa na bango hilo katika maeneo ya Soko Kuu majira ya saa 11:30 jioni, huku akilitembeza barabarani.
Aidha, Mpwapwa alisema bango hilo lilikuwa na maandishi katika pande mbili, ambapo upande wa kwanza ulisomeka Heri Ukimwi uendelee kuliko CCM iendelee kutawala.
Mpwapwa alisema upande wa pili ulisomeka kama Kumkamata waziri kivuli ni kuvunja sheria za mabunge ya Jumuiya ya Madola huku akisisitiza kuwa maandishi hayo yanaashiria uchochezi ndani ya jamii.
Alisema jeshi hilo kwa sasa linamhoji mtuhumiwa huyo, nia na madhumuni ya kuwa na bango hilo na kujua endapo maandishi hayo, aliandika mwenyewe au aliandikiwa na watu wengine.
Alisema endapo mtuhumiwa huyo atathibitika alihusika na tuhuma zinazomkabili, atafikishwa mahakamani.
Source: IPPMEDIA
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa, alisema jeshi hilo linamshikilia mfuasi huyo tangu Juni 5, mwaka huu.
Alisema mtuhumiwa huyo alikutwa na bango hilo katika maeneo ya Soko Kuu majira ya saa 11:30 jioni, huku akilitembeza barabarani.
Aidha, Mpwapwa alisema bango hilo lilikuwa na maandishi katika pande mbili, ambapo upande wa kwanza ulisomeka Heri Ukimwi uendelee kuliko CCM iendelee kutawala.
Mpwapwa alisema upande wa pili ulisomeka kama Kumkamata waziri kivuli ni kuvunja sheria za mabunge ya Jumuiya ya Madola huku akisisitiza kuwa maandishi hayo yanaashiria uchochezi ndani ya jamii.
Alisema jeshi hilo kwa sasa linamhoji mtuhumiwa huyo, nia na madhumuni ya kuwa na bango hilo na kujua endapo maandishi hayo, aliandika mwenyewe au aliandikiwa na watu wengine.
Alisema endapo mtuhumiwa huyo atathibitika alihusika na tuhuma zinazomkabili, atafikishwa mahakamani.
Source: IPPMEDIA