OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 437
Wakuu salama?
Hatimaye siasa za Tanzania zachukuwa sura mpya.
Habari nilizozipata muda huu ni kwamba Mathias Manga, bilionea wa jiji la Arusha, na Diwani wa Kata ya Mlangarini Arumeru Magharibi (CCM), amepigwa risasi na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo wakati akielekea nyumbani.
Imeelezwa kuwa watu hao walifanya jitihada zote lengo ilikuwa ni kumteka lakini mfanyabiashara huyo alijitetea mpaka akajitoa ndio wakaamua kumpiga risasi.
Niko nafuatilia kwa karibu kujuwa soon nitawapa updates japo kwa habari za haraka haraka wanasema kuna siasa ndani yake.
======================
Updates
Amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Selian iliyopo mkoani humo, Waandishi wa habari waliopo Arusha ambao wamezuiwa kuingia katika chumba alicholazwa wamesema amepigwa risasi katika eneo la Mgongoni (Hajaumia sana).