Makaayamawe
JF-Expert Member
- Feb 21, 2009
- 341
- 9
Mfanyabiashara Manji sasa ataka kituo cha ITV kifungiwe wiki moja
Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji, ambaye yupo katika malumbano marefu na mfanyabiashara pia maarufu Reginald Mengi, akitaka kitu chake cha televisheni kifungwe kwa wiki moja.Na Fredy Azzah
MGOGORO wa wafanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam, Reginald Mengi na Yusufu Manji umeingia katika sura mpya, baada ya Manji kupeleka malalamiko kwa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), kutaka kituo cha Televisheni cha ITV, kifungiwe kwa wiki moja.
Malalamiko hayo ya Manji yanahusu habari iliyosomwa na ITV Aprili 23, mwaka huu, saa mbili usiku na kufuatiwa na kipindi maalum kilichorushwa siku hiyo hiyo.
Shauri la malalamiko hayo liliwasilishwa jana TCRA na kuanza kufanyiwa kazi siku hiyo hiyo.
Wakili anayemtetea Manji, John Kamugisha alidai mteja wake ameamua kuwasilisha shauri hilo TCRA baada ya kuona kuwa hakutendewa haki katika kipindi maalum cha nusu saa kilichorushwa na ITV.
Katika kipindi hicho Mengi aliwataja wafanyabiashara watano akiwatuhumu kuhusika na vitendo vya ufisadi na kuwaita kuwa mafisadi Papa.
Tunaamini haki itatendeka hapa. Kimsingi tumependekeza kituo hicho kifungiwe kwa angalau wiki moja, alisema.
Alisema, mteja wake hakutendewa haki kwa sababu hakupewa nafasi ya kutoa maoni yake kama sheria ya utangazaji na maadili ya habari nchini yanavyotaka.
Wakati wa kuwasilisha malalamiko hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa ITV na Redio One, Joyce Mhavile na Wakili wa Mengi, Michael Ngalo pia walikuwepo TCRA.
Kwa mujibu wa Kifungu namba 28 cha Sheria ya Utangazaji ya mwaka 2005, mtu yeyote atakayekiuka taratibu za utangazaji, kama hakuna adhabu iliyotajwa kwenye kifungu husika, atatakiwa kulipa faini ya Sh5milioni.
Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji, ambaye yupo katika malumbano marefu na mfanyabiashara pia maarufu Reginald Mengi, akitaka kitu chake cha televisheni kifungwe kwa wiki moja.Na Fredy Azzah
MGOGORO wa wafanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam, Reginald Mengi na Yusufu Manji umeingia katika sura mpya, baada ya Manji kupeleka malalamiko kwa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), kutaka kituo cha Televisheni cha ITV, kifungiwe kwa wiki moja.
Malalamiko hayo ya Manji yanahusu habari iliyosomwa na ITV Aprili 23, mwaka huu, saa mbili usiku na kufuatiwa na kipindi maalum kilichorushwa siku hiyo hiyo.
Shauri la malalamiko hayo liliwasilishwa jana TCRA na kuanza kufanyiwa kazi siku hiyo hiyo.
Wakili anayemtetea Manji, John Kamugisha alidai mteja wake ameamua kuwasilisha shauri hilo TCRA baada ya kuona kuwa hakutendewa haki katika kipindi maalum cha nusu saa kilichorushwa na ITV.
Katika kipindi hicho Mengi aliwataja wafanyabiashara watano akiwatuhumu kuhusika na vitendo vya ufisadi na kuwaita kuwa mafisadi Papa.
Tunaamini haki itatendeka hapa. Kimsingi tumependekeza kituo hicho kifungiwe kwa angalau wiki moja, alisema.
Alisema, mteja wake hakutendewa haki kwa sababu hakupewa nafasi ya kutoa maoni yake kama sheria ya utangazaji na maadili ya habari nchini yanavyotaka.
Wakati wa kuwasilisha malalamiko hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa ITV na Redio One, Joyce Mhavile na Wakili wa Mengi, Michael Ngalo pia walikuwepo TCRA.
Kwa mujibu wa Kifungu namba 28 cha Sheria ya Utangazaji ya mwaka 2005, mtu yeyote atakayekiuka taratibu za utangazaji, kama hakuna adhabu iliyotajwa kwenye kifungu husika, atatakiwa kulipa faini ya Sh5milioni.
Last edited by a moderator: