Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,280
Leopold II alitawala Congo na ilijulikana kama nchi ilikuwa mali yake binafsi, miaka ya 1835. Tofauti na ilivyokuwa South Afrika kama koloni la Uingereza Congo ilikuwa nchi huru chini ya Mfalime Leopard II
Leopold alizaliwa katika familia ya kifalme mwaka 1835, ujana wake ulikuwa wa kawaida katika makuzi ya kifalme, alitumia muda wake mwingi kujifunza kuwinda, kulenga shabaha, alijiunga na jeshi na alimuoa mtoto wa mfalme wa Austria lakini hakuna aliyetegemea kua atakuja kuwa muuaji wa kushindana na Hitler.
Leopold II aliapishwa kuwa mfalme mwaka 1865 na alitawala Ubelgiji, ndoto yake kubwa ikiwa kuiona Ubelgiji ikiwa na koloni nje ya Ulaya kama ilivyokuwa kwa mataifa makubwa kama Uingereza, Ufaransa, Hispania na Ureno.
Jicho lake la kwanza lilikuwa kuichukua Ufilipino wakati huo likiwa koloni la Hispania. Alitengeneza dili na Malkia Isabella, lakini kabla ya makubaliano kufikia mwisho, malikia Isabella alipinduliwa. Leopard alianza kuangaza macho katika bara la Afrika.
Mwaka 1878, Henry Stanley inasadikika alikutana na Dr. Livingstone katikati ya msitu wa mvua wa Kongo. Magazeti yaliandika habari hii ya kuwapongeza mashujaa hawa wawili kwa kugundua msitu wa Kongo lakini hakuna aliyeuliza wawili hawa walifuata nini kule.
Miaka michache kabla ya mkutano wa Henry Stanley na Dr. Livingston, Leopold II alianzisha African Society iliyoshughulika kuchunguza bara la Afrika na yeye akiwa mfadhili mkuu. Mfalme alipeleka zawadi nyingi kwa raia wa Kongo ikiwemo nguo na magari.
Mfalme Leopold II alifanikiwa kushawishi Congress iliyofanyika 1885 Berlin kuwa Kongo ni nchi huru. Utawala wa Leopold II ulikuwa wa ki dikteta na wa kutisha. Aliua maelfu bila kujali mradi walikwenda kuchimba dhahabu, kuwinda tembo ili apate meno. Wananchi walilimishwa mashamba makubwa ya mpira.
Vijana walilazimishwa kwenda kuvuna raba, aliyeleta kiwango kidogo cha raba alikatwa mkono kama huyo kijana kwenye picha,
Udhalimu uliyofanywa katika nchi huru ya Kongo ulikuwa mkubwa kiasi cha kuwapa hofu nchi nyingine za Ulaya zilizokuwa na makoloni Afrika.
Huyu baba aliitwa Nsala, hapa anaangalia viganja na miguu ya binti yake wa miaka mitano aliyekatwa kama adhabu ya yeye kutokwenda kazini.
Adhabu ya mwanaume ambae hakwenda kazini.
Leopold alizaliwa katika familia ya kifalme mwaka 1835, ujana wake ulikuwa wa kawaida katika makuzi ya kifalme, alitumia muda wake mwingi kujifunza kuwinda, kulenga shabaha, alijiunga na jeshi na alimuoa mtoto wa mfalme wa Austria lakini hakuna aliyetegemea kua atakuja kuwa muuaji wa kushindana na Hitler.
Leopold II aliapishwa kuwa mfalme mwaka 1865 na alitawala Ubelgiji, ndoto yake kubwa ikiwa kuiona Ubelgiji ikiwa na koloni nje ya Ulaya kama ilivyokuwa kwa mataifa makubwa kama Uingereza, Ufaransa, Hispania na Ureno.
Jicho lake la kwanza lilikuwa kuichukua Ufilipino wakati huo likiwa koloni la Hispania. Alitengeneza dili na Malkia Isabella, lakini kabla ya makubaliano kufikia mwisho, malikia Isabella alipinduliwa. Leopard alianza kuangaza macho katika bara la Afrika.
Mwaka 1878, Henry Stanley inasadikika alikutana na Dr. Livingstone katikati ya msitu wa mvua wa Kongo. Magazeti yaliandika habari hii ya kuwapongeza mashujaa hawa wawili kwa kugundua msitu wa Kongo lakini hakuna aliyeuliza wawili hawa walifuata nini kule.
Miaka michache kabla ya mkutano wa Henry Stanley na Dr. Livingston, Leopold II alianzisha African Society iliyoshughulika kuchunguza bara la Afrika na yeye akiwa mfadhili mkuu. Mfalme alipeleka zawadi nyingi kwa raia wa Kongo ikiwemo nguo na magari.
Mfalme Leopold II alifanikiwa kushawishi Congress iliyofanyika 1885 Berlin kuwa Kongo ni nchi huru. Utawala wa Leopold II ulikuwa wa ki dikteta na wa kutisha. Aliua maelfu bila kujali mradi walikwenda kuchimba dhahabu, kuwinda tembo ili apate meno. Wananchi walilimishwa mashamba makubwa ya mpira.
Vijana walilazimishwa kwenda kuvuna raba, aliyeleta kiwango kidogo cha raba alikatwa mkono kama huyo kijana kwenye picha,
Udhalimu uliyofanywa katika nchi huru ya Kongo ulikuwa mkubwa kiasi cha kuwapa hofu nchi nyingine za Ulaya zilizokuwa na makoloni Afrika.
Huyu baba aliitwa Nsala, hapa anaangalia viganja na miguu ya binti yake wa miaka mitano aliyekatwa kama adhabu ya yeye kutokwenda kazini.
Adhabu ya mwanaume ambae hakwenda kazini.