sinajinasasa
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 2,989
- 4,130
Mkuu umeanzisha mada kubwa sana ambayo itakugharimu kuibeba. Tatizo lako umeelekeza mashambulizi kwa kanisa katoliki,na hilo ni kosa kubwa wanalolifanya SDA church, kanisa hili linatoa mahubiri kwa namna ya kukosoa imani za dini nyingine wakijisahau kuwa wao pia wamo katika grave danger. wa SDA wagekuwa na mioyo laini ya kujifunza zaidi Mungu angewafunulia ukweli wote, lakini kanisa hili kupitia GC yaani Mkutano Mkuu wa kanisa hili, imetupilia mbali kweli nyingi ambazo mjumbe wa Mungu aliagizwa kwa kanisa hili ili iwe chachu kwa ulimwengu wote, lakini kwa vile wamejaa kiburi cha uzima na kwakujifanya wanajuakila kitu, Mungu amewaacha waendelee na hekima yao.
Kanisa hili halitambui karama za unabii zilizoko nje zaidi ya kutoka GC, hivyo tena sauti ya upole ya Mungu kwa kanisa hili huzimwa na makao makuu ya kanisa hilo.
Kanisa hili mbali na kukosea kutafsiri unabii wa Ufunuo na wa Danieli, doctrine zao pia zina kasoro nyingi sana. Mfano doctine yao au kung'ang'ania kufundisha kuwa siku ya saba ambayo ni Sabato ni jumamosi!! hili ni kosa kwa vile wanathibitisha kwa jumamosi ni siku ya saba kwa vile wanatumia kalenda ya kirumi ambayo ni Gregorian kalenda, kalenda hiyo ndio kalenda kuu ya kanisa katoliki ambayo yeye mleta mada anawaponda. Wasabato hujikita zaidi kuthibitisha hayo kwa siku za pasaka na ijumaa kuu ya wakatoliki. Biblia inaagiza sikukuu ya pasaka iadhimishwe mwezi wa Abibu tarehe 14. (mwezi wa Abibu ni mwezi wa kwanza kwa kalenda ya kiebrania).
Sipingani sana na mleta uzi isipokuwa presentation yake imejaa kiburi na kupoteza maana. Dini zote zilizopo sokoni leo ukianzia Waislamu, Wasabato wa SDA na wengineo wa jumamosi, Waprotestant wote pamoja na mama yao Romani katoliki, wapo katika hatari kuu ya mafundisho yao.
Ninawaombea wote humu mnaopitia uzi huu, Mungu muumbaji awezeshe wote kwa roho wake, aangazie nuru yake mioyoni mwenu, mpate kuwa na mioyo sikivu ili mpate kuijua kweli yote ambayo Mungu mwenyewe ameagiza kuwa
atatufunulia na kutupeleka kwenye kweli yote. Ezekieli 34:1-16 na Yohana 16:13
Kanisa hili halitambui karama za unabii zilizoko nje zaidi ya kutoka GC, hivyo tena sauti ya upole ya Mungu kwa kanisa hili huzimwa na makao makuu ya kanisa hilo.
Kanisa hili mbali na kukosea kutafsiri unabii wa Ufunuo na wa Danieli, doctrine zao pia zina kasoro nyingi sana. Mfano doctine yao au kung'ang'ania kufundisha kuwa siku ya saba ambayo ni Sabato ni jumamosi!! hili ni kosa kwa vile wanathibitisha kwa jumamosi ni siku ya saba kwa vile wanatumia kalenda ya kirumi ambayo ni Gregorian kalenda, kalenda hiyo ndio kalenda kuu ya kanisa katoliki ambayo yeye mleta mada anawaponda. Wasabato hujikita zaidi kuthibitisha hayo kwa siku za pasaka na ijumaa kuu ya wakatoliki. Biblia inaagiza sikukuu ya pasaka iadhimishwe mwezi wa Abibu tarehe 14. (mwezi wa Abibu ni mwezi wa kwanza kwa kalenda ya kiebrania).
Sipingani sana na mleta uzi isipokuwa presentation yake imejaa kiburi na kupoteza maana. Dini zote zilizopo sokoni leo ukianzia Waislamu, Wasabato wa SDA na wengineo wa jumamosi, Waprotestant wote pamoja na mama yao Romani katoliki, wapo katika hatari kuu ya mafundisho yao.
Ninawaombea wote humu mnaopitia uzi huu, Mungu muumbaji awezeshe wote kwa roho wake, aangazie nuru yake mioyoni mwenu, mpate kuwa na mioyo sikivu ili mpate kuijua kweli yote ambayo Mungu mwenyewe ameagiza kuwa
atatufunulia na kutupeleka kwenye kweli yote. Ezekieli 34:1-16 na Yohana 16:13