MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,562
Huu ni unyanyasaji kwa hao akina mama.Sasa hao manesi wakikuta department number 2 iko tempered with wanawafanya nini?
Mwanzoni ilikuwa wahusika wanaitwa wanapewa darasa la madhara yake kisha kuambiwa wasirudie. Lakini tatizo likawa sugu, mtu anajikuta kaitwa zaidi ya mara tatu ndo wakaamua kuweka a dhabu inayorange toka kuchota maji ya kituo cha afya to kulipa fine kutokana na idadi ya mara ulizopatikana na kosa hilo. Niliacha wakiwa wanazungumzia uwezekano wa kuwafungulia mashitaka hao wamaume ingawa nayo ilikuwa na ugumu wake kwani inahitaji ushahidi kuwa alimforce kwa kutumia nguvu au hakukuwa na makubaliano sasa wanawake wengi walikuwa wanaogopa kufikia huku hasa ukizingatia mikong'oto walokuwa wanapata baada ya watuhumiwa kutumikia adhabu zao. Mwisho ilipelekea wanawake ambao waume zao wamekubuhu katika hii department walikuwa wanaamua kuacha tu kwenda clinik unless waumwe kitu kingine na hao manesi watakutana nao mwaka mwingine wakati wa kujifungua kama wataamua kujifungulia hospital.
Ilikuwa inasikitisha sana.