Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,402
- 1,254
Mmeshindwa nini kuhakikisha watu wanapanga foleni (mistari) kwenye vituo vya mabasi?!
Hamna kitu kinachotia aibu na kunikera kuona watu wanaojiita watu wa mijini wakigombania kupanda mabasi. Yaani ni fujo tupu, ustaarab umepotea kabisa. Jamani hata ng'ombe wanaokwenda kunywa maji hujipanga mstari na kusubiria zamu zao!! Pale wanapoonekana kutokuwa na ustaarabu (kama kwenda kuogeshwa kwenye majosho), hujengewa uzio kuwaongoza.
Mmeshindwa nini ninyi kama wahusika wakuu kwenye miendenendo ya wakazi wa jiji hili?! Jamani hili nalo mpaka tupate msaada kutoka kwa wahisani na kwenda kwenye warsha?!
Tafadhali sana, wekeni sheria katika level ya halmashauri kushughulikia hili suala, kweni liko chini yenu. Sheria ziendane na elimu kwa wakazi. Na kwenye vituo vyenye msongamano mkubwa, wekeni uzio wasafiri wajipange kabla ya kupanda mabasi.
Hamna kitu kinachotia aibu na kunikera kuona watu wanaojiita watu wa mijini wakigombania kupanda mabasi. Yaani ni fujo tupu, ustaarab umepotea kabisa. Jamani hata ng'ombe wanaokwenda kunywa maji hujipanga mstari na kusubiria zamu zao!! Pale wanapoonekana kutokuwa na ustaarabu (kama kwenda kuogeshwa kwenye majosho), hujengewa uzio kuwaongoza.
Mmeshindwa nini ninyi kama wahusika wakuu kwenye miendenendo ya wakazi wa jiji hili?! Jamani hili nalo mpaka tupate msaada kutoka kwa wahisani na kwenda kwenye warsha?!
Tafadhali sana, wekeni sheria katika level ya halmashauri kushughulikia hili suala, kweni liko chini yenu. Sheria ziendane na elimu kwa wakazi. Na kwenye vituo vyenye msongamano mkubwa, wekeni uzio wasafiri wajipange kabla ya kupanda mabasi.