MEYA Jerry Silaa asema SIASA za UJAMAA na KUJITEGEMEA ni MBAYA, NYERERE alituharibu...

Jerry Silaa ni mfano mzuri wa kiburi (arrogance) ambayo aghalabu huwanyemelea binadamu waliopata ngekewa ya mafanikio kidogo. Ironically hawa binadamu wanaopata "mafanikio" ya haraka haraka kwa njia za mashaka ndio wanaoonesha zaidi kiburi cha namna hiyo. Mifano ipo mingi. Unakutana na kijana amehonga-honga all his/her way up, akishafika sasa, simply kwasababu anaweza kusimama mbele za watu wakamsikiliza basi nasaha zake zitakua: "....vijana wasikae tu kulia lia oh serikali hili serikali lile...watu wajitume, wafanye kazi kwa bidii watafanikiwa tu...kama mimi!!" ukweli wa mambo wa "kujituma" kwake "anausahau" kidogo. Kwa sie wengine tunaojua ukweli wa harakati za watu kama hao tunapata shida kweli...
 
Last edited by a moderator:
Sasa inakuwaje unasapoti mambo ya kinda yule, hata maana ya ujamaa na ku I tegemea hajui.
Kuwepo kabla ya uhuru si kigezo maana siye tupo kabla ya uhuru vile vile ns tumepitia yote kianzia uhuru, na tumeona mapinduzi, uhaini wa '64, ujamaa wa '67, njaa ya '74 , vita ya kagera n.k.

Kote tulikopita mpaka sasa hskuna wa kumpiku Mwalimu.

Umaskini, uzembe na uvivu ulioletwa na siasa ya Ujamaa na kujitegemea hujauona? wacha dogo akupe elimu, msome vizuri.
 
nilishawahi kukuambia ,nakuambia tena , na nitakuwa nakuambia kila siku ....... tumia sehemu kubwa ya ubongo wako kufanya maamuzi. sasa huo ushindani unaoufanya kwa kuongezea M kwenye jina la Barack Hussein Obama unatija gani kwako?

That's what he was called by his father.
 

Give us a break...Azimio la Zanzibar????!!!!....ni kitu gani hicho??!!....
Azimio la Arusha was a policy document, unawezaje kulifananisha na kikao cha watu wachache waliokaa kwenye mkutano pale zanzibar na maazimio ya mkutano bado ni siri mpaka leo hazijawa shared to the public.

Kutokana na utata wa yaliyojiri, that is the very reason viongozi wetu wanaendelea kuzungumzia Azimio la Arusha kama Sera ya Chama

Arusha Declaration was everything to us(makabwela) and shall.
...

Historia ina tabia ya kujirudia, MUNGU atusaidie tulione Azimio letu hata kwa sura tofauti likirejea

Mara hulijui, unauliza ni kitu gani, mara unalijua na unasema la watu wachache. Umechanganyikiwa?

Azimio la Zanzibar ndio chanzo cha kuitoa nchi hii kwenye lindi la umaskini ulioletwa na Azimio la Arusha.

Kumbuka, Azimio la Arusha lilikuwa la dikteta mmoja tu, halikuwa na mjadala.
 
Mara hulijui, unauliza ni kitu gani, mara unalijua na unasema la watu wachache. Umechanganyikiwa?

Azimio la Zanzibar ndio chanzo cha kuitoa nchi hii kwenye lindi la umaskini ulioletwa na Azimio la Arusha.

Kumbuka, Azimio la Arusha lilikuwa la dikteta mmoja tu, halikuwa na mjadala.

Chuki yako kwa Mwl. Nyerere inafahamika vema hapa Jukwaani.
 
Nyuma ya Obama namuona shori amevaa Suruali wanaelekea wapi?, halafu kwani Masjid huwa wanaingia na suti?

Egypt_Horo.jpg
 
nngu007
Inawezekana hukuelewa alichosema Jerry Silaa ila ukweli wa mambo kama sio hiyo siasa ya ujamaa na kujitegemea aliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere (R.I.P) Jerry Silaa angekuwa mpiga debe pale Ubungo terminal

Ama angekua anachunga ng'ombe huko maporini! Nchi hii wangekua wanatamba watu wachache wa hapa pwani na makabila machache waliokua wamepiga hatua ktk elimu dunia!
 
Last edited by a moderator:
FaizaFoxy Niwekee ya kusujudu sio ya mawaidha halafu niwekee na ya wanawake wakichanganyikana na wanaume
 
Last edited by a moderator:

Give us a break...Azimio la Zanzibar????!!!!....ni kitu gani hicho??!!....
Azimio la Arusha was a policy document, unawezaje kulifananisha na kikao cha watu wachache waliokaa kwenye mkutano pale zanzibar na maazimio ya mkutano bado ni siri mpaka leo hazijawa shared to the public.

Kutokana na utata wa yaliyojiri, that is the very reason viongozi wetu wanaendelea kuzungumzia Azimio la Arusha kama Sera ya Chama

Arusha Declaration was everything to us(makabwela) and shall.
...

Historia ina tabia ya kujirudia, MUNGU atusaidie tulione Azimio letu hata kwa sura tofauti likirejea
azimio la arusha ni zuri lkn baadhi ya vipengele havitekelezeki. mbona hata mwalimu alikubali kuwa azimio lilifeli? mwalimu alituunganisha kwa kuwa wamoja. namkumbuka kwa hilo. aliharibu uchumi wetu kwa kufadhili nchi za kusini na kuwarudisha akina obote / museveni madarakani
 
nani dogo? cha msingi hapa ni kunata na beat tu, hata kama akileta mziki gani anaweza akakaa tu...

mwishone akaanza ubishi tu...

wewe dogo. kutokana na michango yako, inaelekea nimekuzidi umri that's why nakuita dogo. pili, michango yako imekaa kitoto sana hivyo u deserve kuitwa dogo
 
Umaskini, uzembe na uvivu ulioletwa na siasa ya Ujamaa na kujitegemea hujauona? wacha dogo akupe elimu, msome vizuri.
Uvivu, uzembe, umasikini vyote vikokatika state of mind ya mtu mwenyewe.
Mimi ni mmoja nimelelewa katika mfumo wa Siasa ya Ujamaa na ujitegemea, ni mfumo unamjenga mtu kiakili na kiuzoefu.
Mtu anayejitegemea hawezi kuwa masikini, na ndio maana kinda wako narudia hana uzoefu wala msingi wa kiitikadi wa kumwelewesha mtu kile asichokifahamu.
 
Uyu kilaza hawezi kupoteza muda wake kukaa chini na kusoma walau page 5 kwa siku ndiomaana anongea kwa kuguess tu without credible evidence as a leader.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ujamaa na kujtegemea ilkuwa idea nzuri kwa taifa ambalo lilikuwa ndo linaanza kuchipua.......
 
Uvivu, uzembe, umasikini vyote vikokatika state of mind ya mtu mwenyewe.
Mimi ni mmoja nimelelewa katika mfumo wa Siasa ya Ujamaa na ujitegemea, ni mfumo unamjenga mtu kiakili na kiuzoefu.
Mtu anayejitegemea hawezi kuwa masikini, na ndio maana kinda wako narudia hana uzoefu wala msingi wa kiitikadi wa kumwelewesha mtu kile asichokifahamu.
Mwenzako chama kimemlevya, haoni hasikii milele.


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Miaka michache tu toka kifo cha Muasisi wa taifa hili na Chama tawala anapatikana Meya toka Chama kilichoasisiwa na Hayati Mwl Nyerere tena Meya msomi mwenye uthubutu wa kusema "Nyerere alituharibu" Kweli?
Ujamaa ni mbaya kwa sababu unawafanya Wananchi kuwa wavivu na wategemezi!
Meya anazungumzia ubaya wa Ujamaa au athari zilizotokana na watu walioshindwa kuuelewa na kuutekeleza Ujamaa? Hasa Viongozi wanafiki waliomdanganya Nyerere kuwa ni Wajamaa kumbe siyo?
Mstahiki Meya anaweza kutuonyesha ni wapi Ujamaa unatetea uvivu na utegemezi na siyo Udugu na Kujitegemea?
Ujamaa wetu ulijengwa juu ya Msingi mkuu wa Azimio la Arusha. Meya na atuonyeshe wapi kwenye Azimio hilo tunaambiwa tuwe wavivu na wategemezi? Mstahiki meya anaufahamu Ujamaa?
Ni lini Chama chake kimeachana rasmi na Ujamaa na kuwa Mabepari? Ni hatua zipi Chama hiki kilichukua kuisaidia jamii ya Kitanzania kutoka kwenye Ujamaa na kuingia Ubepari hasa ikizingatiwa kuwa Sheria za Mchezo zinatofautiana. Msingi wa Ubepari umejengwa juu ya kanuni ya "Law of the jungle" yaani "Survival of the fittest" Viongozi wetu walituandaa kwa kiasi gani ili tuingie kwenye Ubepari tukiwa na uelewa wa kutosha kupambana?
Kwa kuwa wao walizijua sheria za mchezo ndiyo maana hawakuona umuhimu wa kutuelekeza ndiyo maana wamefika mahali wanatuita wavivu/tegemezi?
Ndiyo maana Viongozi wetu wengi ni matajiri na mafisadi hasa baada ya kulitupa baharini Azimio la Arusha na miiko yake ya uongozi ili wafisidi mali za Nchi hii?
Yaani ujamaa ni mbaya kwa sababu ulisisitiza usawa, udugu na umoja? Tunu ambazo sasa hivi zinakuwa adimu katika Nchi yetu?
Simwelewi Meya wetu Msomi!
 
Back
Top Bottom