mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,663
- 18,036
Vijana wengi waliozaliwa miaka ya themanini na kuendelea huwa wanakejeli sana siasa ya mwalimu Nyerere ya ujamaa na kujitegemea!! Hawajui kama Tanzania ilikuwa inaheshimika sana duniani kote! Wengi wanaamini kuwa hali ngumu ya kiuchumi ya Tanzania ilisababishwa na ubovu wa siasa ya ujamaa na kujitegemea!! Leo nitatumia kigezo cha thamani ya pesa ili kuakisi kiwango cha uchumi wa Tanzania kuanzia mwaka 1961 baada ya uhurui hadi mwaka 2020.
Jedwali hapo linaonesha kuwa tangu Rais Nyerere alipoipokea Tanganyika (1961) hadi Tanzania mwaka 1978 shilingi ya Tanzania ndio ilikuwa na nguvu kuliko pesa za Kenya na Uganda, Dola 1 ilikuwa sawa na Tsh 7.71. Huo mwaqka wa 1978 vilifumuka vita vya kagera. Iddi Amin alivamia nchi yetu. Nyerere akatangaza vita dhidi ya Amin na vita ile tulishinda lakini ilikomba na kuharibu kabisa uchumi wetu!
Vita ya Kagera iliisha mwaka 1980 na hapo ndio tunaona shilingi yetu inaporomoka na kuwa dola 1 = Tsh 8.22 na ndipo walipoanza kutupiga gepu watu wa kenya. Kwa hiyo vijana mjue siyo ujamaa na kujitegemea uliotuporomosha bali ni vita ya kagera.
Kama ujamaa ungetuporomosha tungeona hasa poromoja hilo kuanzia mwaka 1967 baada ya kutangazwa kwa azimio la Arusha. Lakini hali ya kiuchumi haikutetereka kwa kuanzishwa kwa azimio la Arusha badala yake uchumi uliimarika sana. Tulikuwa na viwanda vingi na tulikuwa tunasafirisha sana mazao nchi za nje kama pamba, katani, kahawa, korosho nk.
Mwaka 84 kukawa na ukame wa kutisha sana na kukawa na njaa kubwa kiasi cha kupewa msaada wa unga toka marekani (almaarufu kama unga wa yanga maana ulikuwa wa njano). Hilo likawa ni tukio lingine la kutuporomosha!
Sasa mwaka 1985 akapokea mzee Ruksa (Mwinyi) dola ikiwa ni Tsh 17.47. Sera za mzee huyu ziliporomosha pesa yetu kwa asilimia 1119% (toka Tsh 17.47 hadi Tsh 195.60 kwa dola moja ya marekani). Kipindi hiki pesa yetu ilikosa kabisa thamani!! Vijana walikuwa wanatembea na maburungutu ya fedha ambazo hazikuweza kuwafikisha popote! Wafanyakazi walidharaulika sana kipindi hiki! Hadi awamu ya Mwinyi inamalizika dola moja ilikuwa na thamani ya Tsh 574.76. Tangu mwanzo wa awamu ya pili mwaka 1985 hadi mwisho wa awamu hiyo ya mzaa ruksa mwaka 1995 fedha yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 5579.6%.
Mkapa alianza awamu yake ya tatu mwaka 1995 dola moja ikiwa ni Tsh 574.76 na alimaliza awamu yake mwaka 2005 dola moja ikiwa ni Tsh 1128.93. Kwa kipindi cha Mkapa shilingi yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 196.42%. Pamoja na lawama kwa Mkapa ya kuuza mashirika yetu kwa bei ya kutupa na yeye mwenyewe kujiuzia kiwanda cha chuma kwa bei ya kuchekesha, lakini alizuia sana kasi ya kuporomoka kwa thamani ya shilingi yetu!! Wafanyakazi walianza kupata tena heshima kipindi cha Mkapa!!
Kikwete alianza awamu yake ya nne mwaka 2005 dola moja ikiwa ni Tsh 574.76 na alimaliza awamu yake mwaka 2015 dola moja ikiwa ni Tsh 1991.39. Kwa kipindi cha Kikwete shilingi yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 346.47%. Hapa tunaona tena ongezeko la kushuka kwa thamani ya shilingi yetu lakini si kama kipindi cha mzee Ruksa! Wafanyakazi walifaidi sana kipindi cha Kikwente maana alikuwa anaongeza mshahara kila mwaka kwenda sambamba na thamani ya pesa!
Magufuli alianza awamu yake ya tano mwaka 2015 dola moja ikiwa na thamani ya Tsh 1991.39 na alimaliza sehemu ya kwanza ya awamu yake mwaka 2020 dola ikiwa na thamani ya Tsh 2294.15. Kwa kipindi cha Magufuli sehemu ya kwanza ya awamu ya sita shilingi yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 115.2%. Wafanyakazi walifunga mkanda kipindi hiki maana hawakuongezewa kabisa mshahara na walipitia kipindi kigumu lakini kwa MATUMAINI kuwa uchumi unajengwa kwanza hatimaye mishahara iongezwe!
Ukiwalinganisha marais wote waliopita kwa ufanisi wao kwa miaka kumi ya mwanzo utapata kama ifuatavyo:
1. Nyerere atabakia kinara ambapo kwa miaka 10 ya mwanzo uchumi uliimarika sana kupitia kilimo na viwanda na thamani ya pesa yetu haikushuka hata kidogo badala yake ilipanda kidogo mwaka 1972 na kuwa dola 1 sawa na Tsh 7.02 hivyo kuwa na ongezeko la thamani la asilimia 1.68%.
2. Magufuli anamfuatia Nyerere akiwa ambapo kwa kipindi chake (bahati mbaya ni miaka 5 tu) pesa yetu iliporomoka kwa asilimia ndogo zaidi yaani asilimia 115.2%
3. Mkapa ni wa tatu ambapo alijitahidi kupunguza kasi ya anguko la pesa yetu. kKipindi chake pesa yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 196.42%.
4. Wa nne kwenye foleni ni Kikwete ambaye kipindi chake pesa yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 346.47%. Wa mwisho anayeshika mkia na kinara wa kuporomosha thamani ya pesa yetu ni mzee Mwinyi. Kipindi chake pesa yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 5579.6%.
Kwa kifupi awamu ya kwanza ndiyo awamu pekee iliyoweza kutunza upinzani kiuchumi hapa afrika ya mashariki na pesa yetu ndiyo ilikuwa na nguvu na ni awamu pekee ambayo pesa yetu iliongezeka thamani angalau kwa hizo asilimia 1.68%. Awamu zote zilizofuatia pesa yetu iliporomoka thamani japo kwa viwango tofauti> Mporomoko wa kutisha ni wa mzee Mwinyi.
Kwa ufafanuzi huu unaotumia data watoto na vijana wanaomkejeli mwalimu Nyerere bila shaka mtashika adabu!!
THAMANI YA SHILINGI YA TANZANIA NA ILE YA KENYA TOKA 1962 HADI 2022 DHIDI YA DOLA YA MAREKANI
MWAKA | USD | TSH | KSH | REMARKS |
1961 | 1 | 7.14 | 7.14 | Mwanzo wa Nyerere |
1962 | 1 | 7.14 | 7.14 | |
1965 | 1 | 7.14 | 7.14 | |
1970 | 1 | 7.14 | 7.14 | |
1975 | 1 | 7.37 | 7.34 | |
1978 | 1 | 7.71 | 7.73 | Mwanzo wa vita ya Kagera |
1980 | 1 | 8.22 | 7.42 | Mwisho wa vita ya Kagera |
1985 | 1 | 17.47 | 16.43 | Mwisho wa Nyerere na mwanzo wa Mwinyi |
1990 | 1 | 195.60 | 22.91 | |
1995 | 1 | 574.76 | 51.43 | Mwisho wa Mwinyi na mwanzo waq Mkapa |
2000 | 1 | 800.41 | 76.18 | |
2005 | 1 | 1128.93 | 75.55 | Mwisho wa Mkapa na mwanzo wa Kikwete |
2010 | 1 | 1395.63 | 79.23 | |
2015 | 1 | 1991.39 | 98.18 | Mwisho wa Kikwete na mwanzo wa Magufuli |
2020 | 1 | 2294.15 | 106.45 |
Jedwali hapo linaonesha kuwa tangu Rais Nyerere alipoipokea Tanganyika (1961) hadi Tanzania mwaka 1978 shilingi ya Tanzania ndio ilikuwa na nguvu kuliko pesa za Kenya na Uganda, Dola 1 ilikuwa sawa na Tsh 7.71. Huo mwaqka wa 1978 vilifumuka vita vya kagera. Iddi Amin alivamia nchi yetu. Nyerere akatangaza vita dhidi ya Amin na vita ile tulishinda lakini ilikomba na kuharibu kabisa uchumi wetu!
Vita ya Kagera iliisha mwaka 1980 na hapo ndio tunaona shilingi yetu inaporomoka na kuwa dola 1 = Tsh 8.22 na ndipo walipoanza kutupiga gepu watu wa kenya. Kwa hiyo vijana mjue siyo ujamaa na kujitegemea uliotuporomosha bali ni vita ya kagera.
Kama ujamaa ungetuporomosha tungeona hasa poromoja hilo kuanzia mwaka 1967 baada ya kutangazwa kwa azimio la Arusha. Lakini hali ya kiuchumi haikutetereka kwa kuanzishwa kwa azimio la Arusha badala yake uchumi uliimarika sana. Tulikuwa na viwanda vingi na tulikuwa tunasafirisha sana mazao nchi za nje kama pamba, katani, kahawa, korosho nk.
Mwaka 84 kukawa na ukame wa kutisha sana na kukawa na njaa kubwa kiasi cha kupewa msaada wa unga toka marekani (almaarufu kama unga wa yanga maana ulikuwa wa njano). Hilo likawa ni tukio lingine la kutuporomosha!
Sasa mwaka 1985 akapokea mzee Ruksa (Mwinyi) dola ikiwa ni Tsh 17.47. Sera za mzee huyu ziliporomosha pesa yetu kwa asilimia 1119% (toka Tsh 17.47 hadi Tsh 195.60 kwa dola moja ya marekani). Kipindi hiki pesa yetu ilikosa kabisa thamani!! Vijana walikuwa wanatembea na maburungutu ya fedha ambazo hazikuweza kuwafikisha popote! Wafanyakazi walidharaulika sana kipindi hiki! Hadi awamu ya Mwinyi inamalizika dola moja ilikuwa na thamani ya Tsh 574.76. Tangu mwanzo wa awamu ya pili mwaka 1985 hadi mwisho wa awamu hiyo ya mzaa ruksa mwaka 1995 fedha yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 5579.6%.
Mkapa alianza awamu yake ya tatu mwaka 1995 dola moja ikiwa ni Tsh 574.76 na alimaliza awamu yake mwaka 2005 dola moja ikiwa ni Tsh 1128.93. Kwa kipindi cha Mkapa shilingi yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 196.42%. Pamoja na lawama kwa Mkapa ya kuuza mashirika yetu kwa bei ya kutupa na yeye mwenyewe kujiuzia kiwanda cha chuma kwa bei ya kuchekesha, lakini alizuia sana kasi ya kuporomoka kwa thamani ya shilingi yetu!! Wafanyakazi walianza kupata tena heshima kipindi cha Mkapa!!
Kikwete alianza awamu yake ya nne mwaka 2005 dola moja ikiwa ni Tsh 574.76 na alimaliza awamu yake mwaka 2015 dola moja ikiwa ni Tsh 1991.39. Kwa kipindi cha Kikwete shilingi yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 346.47%. Hapa tunaona tena ongezeko la kushuka kwa thamani ya shilingi yetu lakini si kama kipindi cha mzee Ruksa! Wafanyakazi walifaidi sana kipindi cha Kikwente maana alikuwa anaongeza mshahara kila mwaka kwenda sambamba na thamani ya pesa!
Magufuli alianza awamu yake ya tano mwaka 2015 dola moja ikiwa na thamani ya Tsh 1991.39 na alimaliza sehemu ya kwanza ya awamu yake mwaka 2020 dola ikiwa na thamani ya Tsh 2294.15. Kwa kipindi cha Magufuli sehemu ya kwanza ya awamu ya sita shilingi yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 115.2%. Wafanyakazi walifunga mkanda kipindi hiki maana hawakuongezewa kabisa mshahara na walipitia kipindi kigumu lakini kwa MATUMAINI kuwa uchumi unajengwa kwanza hatimaye mishahara iongezwe!
Ukiwalinganisha marais wote waliopita kwa ufanisi wao kwa miaka kumi ya mwanzo utapata kama ifuatavyo:
1. Nyerere atabakia kinara ambapo kwa miaka 10 ya mwanzo uchumi uliimarika sana kupitia kilimo na viwanda na thamani ya pesa yetu haikushuka hata kidogo badala yake ilipanda kidogo mwaka 1972 na kuwa dola 1 sawa na Tsh 7.02 hivyo kuwa na ongezeko la thamani la asilimia 1.68%.
2. Magufuli anamfuatia Nyerere akiwa ambapo kwa kipindi chake (bahati mbaya ni miaka 5 tu) pesa yetu iliporomoka kwa asilimia ndogo zaidi yaani asilimia 115.2%
3. Mkapa ni wa tatu ambapo alijitahidi kupunguza kasi ya anguko la pesa yetu. kKipindi chake pesa yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 196.42%.
4. Wa nne kwenye foleni ni Kikwete ambaye kipindi chake pesa yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 346.47%. Wa mwisho anayeshika mkia na kinara wa kuporomosha thamani ya pesa yetu ni mzee Mwinyi. Kipindi chake pesa yetu iliporomoka thamani kwa asilimia 5579.6%.
Kwa kifupi awamu ya kwanza ndiyo awamu pekee iliyoweza kutunza upinzani kiuchumi hapa afrika ya mashariki na pesa yetu ndiyo ilikuwa na nguvu na ni awamu pekee ambayo pesa yetu iliongezeka thamani angalau kwa hizo asilimia 1.68%. Awamu zote zilizofuatia pesa yetu iliporomoka thamani japo kwa viwango tofauti> Mporomoko wa kutisha ni wa mzee Mwinyi.
Kwa ufafanuzi huu unaotumia data watoto na vijana wanaomkejeli mwalimu Nyerere bila shaka mtashika adabu!!