Mkunazi Njiwa
JF-Expert Member
- Apr 22, 2023
- 5,510
- 4,818
UKABILA NA UKANDA
Hakufanya alichofanya hayati Kenyatta.....
Baba wa taifa hakumilikisha WAZANAKI na watu wa kanda ya ziwa raslimali za nchi......
Iko hoja ya kudai kuwa aliwajaza wazanaki katika nafasi za kumlinda.....ukiangalia hii ni hoja dhaifu kwani taifa lililokuwa linasimikwa ni lazima kiongozi wake alindwe kwa ukaribu na watu waliokula "yamini"....hayati Nyerere hakukosea.......
KUPINGA UDINI NA MADHEHEBU SHINIKIZI KISIASA
Pamoja na ukatoliki wake.....hakukubali kuusaliti UJAMAA NA KUJITEGEMEA....
Na kama angekuwa "mdini" balaa lake lisingekuwa dogo na tungeendelea "kulipia" ubaguzi huo kama ilivyo Nigeria ya Kaskazini na kusini.....mfano wake ungedhihirika mikoa ya Pwani yenye waislamu wengi na mikoa ya nyanda za juu kusini yenye wakristo wengi....hilo hatulioni.....
Dhana ya udini imekuwa ikiibuliwa na madhehebu na wanasiasa kwa malengo yao kwa kiwango cha KUTOLIGAWA taifa hili......
UVUNJWAJI WA TAASISI ZA KIDINI ILI KUSIMIKA UJAMAA NA KUJITEGEMEA
Mwaka 1968 hakukosea kuivunja EAWMS (EAST AFRICAN WELFARE MUSLIM SOCIETY) ambayo ilikuwa ni unganiko la waislam wa nchi za afrika ya mashariki ikihusisha na Kenya ambako kulikuwa na siasa za KIBEPARI na huku Tanganyika kukiwa na SIMIKO LA UJAMAA NA KUJITEGEMEA....
Hapa panahitaji tafakuri jadidi...kwa wazalendo wanaotaka fikra huru basi hawatapingana na hayati JKN kwani "EAWMS" ingeweza kutumiwa kisiasa na kijasusi na maadui wa UJAMAA WA KIAFRIKA na kuturudisha nyuma katika harakati za kujikomboa zikihusisha AZIMIO LA ARUSHA........
LUGHA MOJA YA KISWAHILI
Pamoja na kiswahili kuzungumzwa sana mikoa ya Pwani hayati JKN alijitahidi kukitawanya kiswahili nchi nzima na kuwa lugha ya taifa tofauti na kule CAMEROON ambako nchi ina "FRANCOPHONE" na "ANGLOPHONE SPEAKERS"...kwa hili hayati JKN anajipambanua kuwa tofauti na mababa wa taifa wa mataifa huru ya Afrika.....
ELIMU
Ni hayati JKN aliyeendelea kuwakumbusha raia wenzake juu ya maadui wakuu 3 wa taifa..UJINGA ,MARADHI NA UMASKINI......
Mkoloni hakuiachia TANGANYIKA CHUO KIKUU....tofauti na UGANDA ambako mwingireza alijenga chuo kikuu cha Makerere.....na hayati JKN akajenga chuo kikuu cha Dar es salaam....waliomfuatilia wakajenga vyuo vikuu vyengine kuiendeleza CHACHU iliyoanzishwa na baba wa taifa hayati JKN.....
KUUSIMIKA MFUMO WA "KOFIA MOJA" KWA RAIS NA MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI
Ya hayati Nkurunzinza na mwenyekiti wake wa CNNDD-FDD komredi Rajabu ni kukosekana kwa mawazo kuntu ya Nyerere huko Burundi.....
Ya Afrika Kusini na katiba yake ya kuwashtaki marais yameonekana kutokuwa na ubora wa mawazo ya baba wa taifa hayati JKN kwani yeye alijua wanasiasa wanaweza "kutengenezeana" zengwe kung'oana madarakani na kukaribisha kutotawalika kwa nchi na hata mapinduzi ya kijeshi yasiyo na mwisho......
Hakika taifa bora Tanzania litabaki la bahati kumpata baba wa taifa ambaye maono yake yaliutangulia muda tuliopo
Resty easy El Commandante JKN ,amen
#Hakuna Mwenye Misuli Ya Kuligawa Taifa Hili
#SiempreJMT
#Mama Kaja
Hakufanya alichofanya hayati Kenyatta.....
Baba wa taifa hakumilikisha WAZANAKI na watu wa kanda ya ziwa raslimali za nchi......
Iko hoja ya kudai kuwa aliwajaza wazanaki katika nafasi za kumlinda.....ukiangalia hii ni hoja dhaifu kwani taifa lililokuwa linasimikwa ni lazima kiongozi wake alindwe kwa ukaribu na watu waliokula "yamini"....hayati Nyerere hakukosea.......
KUPINGA UDINI NA MADHEHEBU SHINIKIZI KISIASA
Pamoja na ukatoliki wake.....hakukubali kuusaliti UJAMAA NA KUJITEGEMEA....
Na kama angekuwa "mdini" balaa lake lisingekuwa dogo na tungeendelea "kulipia" ubaguzi huo kama ilivyo Nigeria ya Kaskazini na kusini.....mfano wake ungedhihirika mikoa ya Pwani yenye waislamu wengi na mikoa ya nyanda za juu kusini yenye wakristo wengi....hilo hatulioni.....
Dhana ya udini imekuwa ikiibuliwa na madhehebu na wanasiasa kwa malengo yao kwa kiwango cha KUTOLIGAWA taifa hili......
UVUNJWAJI WA TAASISI ZA KIDINI ILI KUSIMIKA UJAMAA NA KUJITEGEMEA
Mwaka 1968 hakukosea kuivunja EAWMS (EAST AFRICAN WELFARE MUSLIM SOCIETY) ambayo ilikuwa ni unganiko la waislam wa nchi za afrika ya mashariki ikihusisha na Kenya ambako kulikuwa na siasa za KIBEPARI na huku Tanganyika kukiwa na SIMIKO LA UJAMAA NA KUJITEGEMEA....
Hapa panahitaji tafakuri jadidi...kwa wazalendo wanaotaka fikra huru basi hawatapingana na hayati JKN kwani "EAWMS" ingeweza kutumiwa kisiasa na kijasusi na maadui wa UJAMAA WA KIAFRIKA na kuturudisha nyuma katika harakati za kujikomboa zikihusisha AZIMIO LA ARUSHA........
LUGHA MOJA YA KISWAHILI
Pamoja na kiswahili kuzungumzwa sana mikoa ya Pwani hayati JKN alijitahidi kukitawanya kiswahili nchi nzima na kuwa lugha ya taifa tofauti na kule CAMEROON ambako nchi ina "FRANCOPHONE" na "ANGLOPHONE SPEAKERS"...kwa hili hayati JKN anajipambanua kuwa tofauti na mababa wa taifa wa mataifa huru ya Afrika.....
ELIMU
Ni hayati JKN aliyeendelea kuwakumbusha raia wenzake juu ya maadui wakuu 3 wa taifa..UJINGA ,MARADHI NA UMASKINI......
Mkoloni hakuiachia TANGANYIKA CHUO KIKUU....tofauti na UGANDA ambako mwingireza alijenga chuo kikuu cha Makerere.....na hayati JKN akajenga chuo kikuu cha Dar es salaam....waliomfuatilia wakajenga vyuo vikuu vyengine kuiendeleza CHACHU iliyoanzishwa na baba wa taifa hayati JKN.....
KUUSIMIKA MFUMO WA "KOFIA MOJA" KWA RAIS NA MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI
Ya hayati Nkurunzinza na mwenyekiti wake wa CNNDD-FDD komredi Rajabu ni kukosekana kwa mawazo kuntu ya Nyerere huko Burundi.....
Ya Afrika Kusini na katiba yake ya kuwashtaki marais yameonekana kutokuwa na ubora wa mawazo ya baba wa taifa hayati JKN kwani yeye alijua wanasiasa wanaweza "kutengenezeana" zengwe kung'oana madarakani na kukaribisha kutotawalika kwa nchi na hata mapinduzi ya kijeshi yasiyo na mwisho......
Hakika taifa bora Tanzania litabaki la bahati kumpata baba wa taifa ambaye maono yake yaliutangulia muda tuliopo
Resty easy El Commandante JKN ,amen
#Hakuna Mwenye Misuli Ya Kuligawa Taifa Hili
#SiempreJMT
#Mama Kaja