Mengi: Manji anatoa wapi kiburi na ujasiri?

Mengi: Manji anatoa wapi kiburi na ujasiri?

You dont have to look far to knw manji..angalieni board of directors ya NSSF..Link it to the present cabinet...mtamjua manji anatoa wapi kiburi!
Umesahau kuangalia na kamati ya ufundi ya yanga, udiwani CCM na kijiji cha msoga huko pia ndio kwenye nguvu zake
 
Wakati huu Kiburi kitaisha tu, anatapatapa tu aonekane bado yupo ila kiukweli mambo yashamfika shingoni. Subiri uone akitoka hospitali tu watu watamrudisha tena hukohuko chezea pressure za Jpm.
 
Raisi shikilia gia hiyo hiyo mpaka hawa wezi wa Mali za umma akili ziwakae sawa au Waikimbie nchi...


Kumbe wafanyakazi hatupewi fedha zetu za nssf na mifuko ya kijamii kwa wizi wa watu wachache kama Manji...

Nakuomba raisi watu kama hawa waliosababishia nchi hasara na maisha magumu wanyongwe kabisa sio kwenda kula kodi zetu huko magerezani.....
 
Manji ni mtoto mdogo sana,hawezi kuwa na SIRI kali na Nchi,Sema anatumiwa na nchi baada ya wao mambumbumbu kuhongwa pesa za chafu.

Mwisho wao ni hivi karibuni wala siku si nyingi,siku ambyo watanzania watapata Neema,watafurahi kuangushwa kwa hawa wamaojaribu kuiweka Nchi rehani,Machozi yananitoka sababu naomba mwalimua rudi aje aone uozo huu unaoendela katika nchi yetu
Mkuu uliomba dua njema
 
Mkuu huwezi amini saivi wanaomtetea manji aliemtukana mstusi ya nguoni Mheshimiwa Ndesa Mburo R.I.P ni wanachama wa Chadema japo na mimi ni mwanachama lakini nashangaa sana huu uzumbukuku wa hawa wenzetu.
Mkuu huu ulimwengu ni wa kuogofya sana,ndio maana muda mwingine inabidi kumeditate ili kupunguza mauzauza tunayoyashuhudia kila siku
 
Wakuu habari za leo,

Jana Baada ya kutolewa kwa shauri kati ya madai ya Manji kukashifiwa na ITV katika moja ya taarifa zake za habari, ila ITV wameshinda kwa kutokuonekana na hatia yoyote kutokana na shauri hilo.

Baada ya Kutoka ndani ,Mzee mengi akihojiwa na waandishi wa habari, aliuliza watanzania, ''Hiki Kiburi na ujasiri alionao Manji nani anampa? Mzee mengi alisema “anatoa wapi nguvu hizi?” Hii ni baada ya Manji kukosekana pale katika siku ya kutoa maamuzi. Hii mzee Mengi aliona kama ni dharau kubwa kwake. Manji aliwakilishwa na wakili wake.

Najua mna mambo mengi ila naomba tujibu swali la Mzee Mengi, Je Manji anatoa wapi kiburi cha na namna hii na ujasiri mkubwa kiasi hiki?? Nani anampa? Nani yuko juu yake?
.
Jibu ni fupi tu.
PESA!!
 
Luteni Makamba ammiminia mabusu mfadhili wa miradi
2005-07-21 14:57:21
Na Maabad Msuya, Temeke

Baada ya kushindwa kujizuia kuonyesha furaha yake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Luteni Yusuph Makamba, amejikuta akimfagilia mfadhili wa miradi mbalimbali wilayani Temeke Bwana Yusuph Manji na kumtaka agombee ubunge wa jimbo la Kigamboni kwa tiketi ya CCM.

Kama vile haitoshi Mkuu huyo wa Mkoa kwa kuonyesha ni jinsi gani alivyovutiwa na kufurahishwa na ufadhili huo, aliamua kumpa mabusu Bw. Manji kama ishara ya shukrani na furaha.

Luteni Makamba ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo, baada ya kuvutiwa na mwamko wa wakazi wa eneo hilo, naye ameahidi kuchangia Sh. milioni 1.5, kati ya hizo, milioni moja ikitoka mfukoni mwake na laki tano kwenye mfuko wa ofisi yake.

'Kusema kweli umenifurahisha sana na ili kukuonyesha ni jinsi gani umenifurahisha nakuomba usogee tena hapa karibu yangu ili nikupe busu la furaha,' akasema Mkuu huyo wa Mkoa na kisha akaanza kumimina mabusu mfululizo.

Source: Alasiri
Naona huu ni Mwaka wa kufukua makaburi... Hahahahaa
 
Wapi nilipomtetea Manji wewe! Acha kukurupuka na kuandika pumba humu. Hebu weka huo ushahidi wa kuonyesha pale nilipomtetea Manji, au ni wale wa shule za kata kusoma kumekupiga chenga!?

Siku hizi mnamtetea bwana Manji, nyie watu wa ajabu sana, si ajabu 2020 mkampa nafasi ya kugombea uraisi kupitia Chadema
 
Hahahahaha akili ndogo siku zote haishindi akili kubwa. Msimamo wangu wa 2007 hautabadilika kuhusu fisadi yoyote yule. Acha kukurupuka kuandika uzushi bila ya kuwa na ushahidi hata chembe.

Huyo BAK mrija wa aibu ulishakata, ni mnafiki Kubenea na Kipanya wakasome
 
Back
Top Bottom