Memory bomba KIhanda Camp Sumbawanga

Memory bomba KIhanda Camp Sumbawanga

nzalendo

Platinum Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,889
Reaction score
14,596
Naam kuna nyakati maishani zinabaki kuwa kumbukumbu nzuri sana.

Tanzania tumejaaliwa kuwa na mchanganyiko wa makabila mengi na tukaishi pasi kujali tofauti zetu kama dini,rang, kabila, khali n,k,

Ilikuwa ni Kihanda Camp chini ya kampuni ya Aarsleff Bam International juu ya ujenzi wa barabara,

NI mwezi wa kumi na mbili Kampuni inasimamisha kazi kutokana na sikukuu za krismasi na mwaka mpya....kwa sisi wa khali ya kawaida ambao wengi vipato vyetu ni vidogo,,,unapiga hesabu ya kutoka Sumbawanga mpaka Moshi...kwenda na kurudi mara gharama za sikukuu n.k......unaona bora utume kitu kidogo nyumbani then uendelee na mapambano.

Naam siku ya krismasi imefika tunajikuta watu kadhaa tumebaki kambini...tunaona sikukuu isipite kinyonge..tunafanya utaratibu wa Muziki vinywaji misosi n.k......sherehe inafana...raia wengi tumetoka Dar,,,kwa Kipindi hicho wimbo wa Abdul Kiba upo hewani ....raia wamelewa ...kila mara wanaomba,,wimbo wa KIZUNGUZUNGU upigwe,,,,maisha yanaendelea.

Mchizi wetu Maiko(driver) alikuwa na kabiashara kake ka kuuza vinywaji Camp,,,bila shaka siku hiyo alipiga hela....

Wengi nimewakumbuka lakini mchizi wetu Juma GOGO alishatangulia mbele za haki...nimemkumbuka dereva nadhifu Boni..wengine ni Mzee wa Mwira,,Kalinga..kuna jamaa alikuwa anaendesha NIssan nimemsahau jina mtu wa Dodoma alikuwa akijiita American...Nimemkumbuka fundi Shekivuli,,,alikuwa still fixer....Pia kulikuwa na Senior Surveyor Edom Bezu kutoka Ethiopia,,,,,,na mpare mmoja alikuwa anaitwa papaa Msofe (engineer)......hiyo ni kwa uchache na wengine wengi,


Kesho yake hatuna hata mia tumechelewa kuamka tunatembea tembea kijijini tunakaribishwa pombe za machicha tunapiga kiroho safi ili tushibe,,,mara manyunyu ya mvua,,,moto unakokwa kibaridi kwa mbali na mahindi ya kuchoma,

KUMBUKUMBU MUJARAB
 
Kwanini watu wanaotokea mkoa wa Kilimanjaro husema ametokea Moshi wakati kwao ni Rombo au Hai n.k?

Mbona mtu wa Maswa husema anatokea Maswa na sio Kishapu nyie mbona mazumbukuku sana
 
Kwanini watu wanaotokea mkoa wa Kilimanjaro husema ametokea Moshi wakati kwao ni Rombo au Hai n.k?

Mbona mtu wa Maswa husema anatokea Maswa na sio Kishapu nyie mbona mazumbukuku sana
Mie wa KB..... AKA...Kiborlony.....
Hebu nichekie kama ipo Moshi......
 
Pia kwenye sherehe hiyo tulikuwa na dada wa kiJamaica...alikuwa mreeefu kama nguzo ya umeme...
Aliweka challenge kwa kila aliye weza kuimba wimbo wa Bob...alimpatia ''Mwekundu wa Msimbazi''......
 
Kumbukumbu nzuri sana...

kulingana na wimbo huo inawezekana miaka hiyo hiyo kabla raia hawajasanuka.
Kuna mwaka mikoa mingine haikupata Mchele sana tulisomba hapo mchele kwa kilo tsh 800/= japo barabara ilitutoa jasho tulipiga pesa....
shukrani kwenu leo sumbawanga mpaka mbeya kuna lami.

Genz zungukeni africa kuna pesa nyingi sana.
 
Kumbukumbu nzuri sana...

kulingana na wimbo huo inawezekana miaka hiyo hiyo kabla raia hawajasanuka.
Kuna mwaka mikoa mingine haikupata Mchele sana tulisomba hapo mchele kwa kilo tsh 800/= japo barabara ilitutoa jasho tulipiga pesa....
shukrani kwenu leo sumbawanga mpaka mbeya kuna lami.

Genz zungukeni africa kuna pesa nyingi sana.
Sahihi kabisa.....
Vyakula bei ilikuwa chini sana,,,,Mchele wengi waliufuata mpaka kwenye bonde la Ziwa Rukwa.

Sasa umenikumbusha kipindi tunajenga barabara ya Nzega...Tinde...then Tinde....Maganzo...na Tinde...Isaka,,,Mchele ulikuwa Jelojelo kwa kilo,,nyama ya kondoo tunanunua kwa mapande siku ya jumanne mnadani nayo ni Jelojelo,,,,,na pande lilikuwa linakaribia kilo.

Kambi ilikuwa ni hapo hapo Tinde ingawa kulikuwa na kambi nyingine Maganzo.

Sasa wazungu walikuwa wananunua kondoo kwa wingi...ghafla bei ya kondoo ikawa juu kushinda mbuzi,,,kwa hiyo dili la nyama ya jelo jelo ikapotea....Kampuni ilikuwa ya makaburu Grinaker LTA...

Hapa nimemkumbuka mzee mwenzangu Nyakunga alikuwa Dereva wa Benz Powerliner..mwingine alikuwa Sir Edward au Edward mpalestina naye alikuwa akiendesha Benz poweliner Tiper,,,daah...mwingine alikuwa kijana aliitwa Frank Kamando naye... Benz,,mwingine aliitwa Wabongo RIP huyu alikuwa na sifa ya kukimbia na magari,,,,baada ya mradi alipata ajali mbaya sana,,,akakatika kichwa ....kikapatikana baada ya siku nyingi,,,na siku zote alikuwa akijitamkia kwamba kama akipata ajali hataki kupona anataka kupotea mazima (maneno huumba)...pia nimemkumbuka Major Magere RIP huyu alikuwa Security Oficer wa Kampuni ya Grinaker,,,,kila jioni tulikuwa tunapata naye kikombe chini ya mti kwenye Bar ya dada mmoja (Ester)

Daah,,,nimekumbuka mengi sana Ofisini kulikuwa na kina Bruno dada KHadija( muarabu wa Tinde)...Walter Mhasibu toka sauzi,,nk nk,,,

Kuna kichekesho kilitokea mapolisi walikamata diesel za wizi pamoja na nondo na Cement wakaleta ripoti ofisini na kumtaka project manager Mr.Frank Swift aende kutambua mali hizo za wizi,

Project Manager mwenyewe Zungu la sauzi naye muhuni tu,,,,akawaambia polisi zile mali si za kampuni ingawa diesel ya kampuni ilitambulika kwa kutiwa rangi nyekundu.... lakini mzungu aliikataa katakata....akadai diesel ya kampuni ipo kwenye matank na ndani ya mitambo......pia kwenye magari hiyo nyingine ni ya kwao waichukue,,,,,,,
 
Back
Top Bottom