Membe kuwania urais 2015...


Mkuu, huwa nikiwaambia watu hivyo hawanielewi. Nina uhakika Lowasa akipewa rungu, nchi itabadilika? akiwa PM hajawahi kupewa riport za uongo kana JK ambaye ni Rais - kwa sababu watendaji wanajua akili yake si ya kivivu. Kama kosa alifanya, nina uhakika ameshajifunza na kujirekebisha. Huyu cheka cheka na bongo flava hatatupeleka popote zaidi ya shimoni tu.
Ikiwa atakuwa rais, kufikia 2015 inawezekana hata chai wengi wakashindwa kunywa kutokana na mfumko wa bei - watanzania wengi wanaweza wasimuda kununua sukari. to name the few.
 

Labda tuwe na mgombea binafsi ndio hivi vitatekelezeka maana atayakwepa mengi
 
Mnajiombea mabaya...Kumbuka dictator wengi wanataka kuambiwa kile wanachotaka kukisikia.Mmeona Kenya mama Kibaki alivyopiga watu vibao na Russia watu wanavyopotezwa.
Bora tubaki na huu uhuru wetu wakutoa hasira zetu hapa Jamboforums kuliko kukosa yote.
 
Hivi jamani Membe ana Digrii kweli? habari nilizo nazo ni kuwa hana.........mbali na hilo kichwa cha panzi!
 
Tunahitaji mabadiriko na haya mabadiriko sijui yataletwa na nani
Ndani ya CCM hakuna mtu mwenye sifa ya kuendelea kuwa Rais wa nchi hii basi wanalazimisha tu
 

Ukiwa raia mwema huwezi kupotezwa. Kwa waandishi wa habari wa TZ anatakiwa festi ledi kama mama kibaki. Wengi ni vibaraka na wameshanunuliwa na wanasiasa.
Bakora tu ndizo zinaweza kuwaamsha.
 
Hivi jamani Membe ana Digrii kweli? habari nilizo nazo ni kuwa hana.........mbali na hilo kichwa cha panzi!
Membe ana MA aliipata Johns Hopkins University USA. Nilimwona kwa macho yangu wakati wa graduation. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
 

Kwa sifa hizi, ukilinganisha Lowassa na Membe, inaonekana Lowassa anafaa zaidi... lakini tunaweza kumfikiria na Wassira? - I mean sura yake ni ya kidikteta zaidi kuliko hawa
 
..kwangu mimi huu uchaguzi umekwisha na JK ndiyo Rais.

..matokeo haya yamenisikitisha sana, kwasababu naamini kabisa Slaa au Lipumba ni more capable kuliko JK.

..sasa CCM ina tabia ya "kujivua ngozi" ngozi kila inapofikia wakati wa kubadilisha mgombea Urais.

..kwa mtizamo wangu January Makamba, Magufuli, Membe na Migiro, wanapaswa kuangaliwa kwa umakini sana kuelekea mwaka 2015.

..wapinzani wajiandae jinsi ya kupambana na yeyote kati ya hao itakapofika 2015.
 
JokaKuu swala la January Makamba kuwa rais 2015 ondoa kabisa akili mwako kwa sababu kuu mbili CCM wana katiba ya siri isiyoandikwa mathalani rais wa sasa ni mwislamu ajaye ni lazima kuwa mkristo moja kwa moja J Makamba anakuwa nje ya mashindano pili atakuwa ni waziri junior jambo ambalo wakongwe hatakubali kabisa.

Magufuli haweze kwasababu hana mtandao kwenye chama yeye ni mchapa kazi tu kama Mizengo Pinda, kuhusu Membe ana maadui wengi akiwamo lowassa huyu kupita itakuwa kazi ukizingatia kuwa ni swahiba wa Kikwete na CCM wanataka kukoma kwa Kikwete Revolution by 2015 akilazimisha nchi itakwenda upinzani pia CCM wanataka rais ajaye atoke Bara na si Pwani kwani Tanzania imekuwa na marais wanne mmoja pekee Julus Nyerere ndiye aliyetoka bara wengine wote ni mwambao wa bahari ya hindi Ali Hassani Mwinyi, Benjamini Mkapa na Jkaya Kikwete kuuonezea Membe mwana pwani mwingine haitawezekana kabisa.

Urais 2015 uko wazi chunga sana Lowassa, Sumaye, Mwandosya na Rose Migiro
 
Heri mama Migiro at least nitampa kakura kangu ambako hakataniuma roho
 
Ata mwandosya nae anafaa kimtindo ingawa CCM ya leo haitaki watu ambao wanastand on what they say.
CCM ya leo wanataka watu wenye mzaa mzaaaaaaaaaaa
 
MAGHUFULI JOHN POMBE(PHD) / ASHA ROSE MIGIRO wanafaaa kuongoza nchi

 
Mama Tibaijuka mmemuweka wapi? Pinda je? Dr. Bilali???

Pinda tayari alishasema hii ndio mara yake ya mwisho. Wapiga kura wametoa message kali kwa hiyo CCM itajipanga 2015. Sidhani kama watamsimamisha mbabaishaji au mshikaji wa Kikwete. Lakini yote hayo pia yatategemea jinsi Kikwete atakavyoendesha nchi miaka 5 ijayo.
 
wakitaka CCM kushinda kirahisi wamweke Dr Harison George Mwakyembe, ila kama jadi yao CCM haitaki mtu mkweli au msomi mwenye msimamo
wenyewe na vuvuzelas, period
 
Sijaipenda thread hii mi nkijua baada ya 2010 mchakachuo, Dr.SLAA atawashika tena, siwezi fikiria mwingne kwa sasa. Kwa CCM yeyote watakaemtaka ila mwanamke haitawezekana kwa sasa, sori 4 this.

Siwachukii wamama ila kdogo upresidaa unataka kijeba, kutunisha misuli, kumbuka tangu mama Zakia meji aharibu pale benki kuu,watawala waliapa kutorudia kosa. Halafu kuhimili siku 71 za kampeni mwanamke hawezi sana sana kama bado anauona mwezi,sori 4this bt guess wote mu watu wazma.

Nasema na nina uhakika Tz ya leo mikononi mwa mwanamama bado sana!
 
Kiongozi yeyote wa CCM hawezi kuleta mabadiliko ya kuwasaidia watz..tusidanganyike, CCM machine is corrupt to the core kama kansa na hakuna tiba tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…