Membe kuwania urais 2015...

Wakati watu wanafikiria siasa za Kyela kule.. siasa nyingi za mwaka huu zitakuwa ni huko Lindi.. kutanoga!!

Mwanakijiji, kama una maana kwenye jimbo la Membe kule hakuna kitakachonoga mana hakuna mpinzani anayemnyima usingizi Membe....mpinzani wa Membe ni Shaibu ambaye yeye kazi yake kila uchaguzi nikutafuna ela za wapinzani wa Membe (RA, EL & Co) huku akiwaambia wapiga kura wake wampigie Membe!!

Kutakakonoga ni jimbo la Mudhihiri (Mchinga) ambalo hadi sasa tayari watu 7 wametangaza kuchuana naye akiwemo dada moja mashuhuri Mayasa, jimbo la lindi mjini, na Rwangwa (ambako Majogo anapiga speed za kurudi).
 
Geoff, huu ni upuuzi mtupu anaotuletea GT ktk thread hii. GT katumwa na MAFISADI wanaoimaliza nchi hii, nae kwa njaa zake kakubali kutumiwa bila kufanya utaifiti wa kutosha ili ajenge hoja itakayokubalika. Anataka watu ktk JF wamuhukumu Membe bila kosa. Huyu ni muongo mkubwa. Lazima aje na majibu ya mwaswali yangu ili tumtendee haki Membe, otherwise, nitaamini kwa kiasi kikubwa kuwa AMENUNULIWA na MAFISADI. Nasema hivi kwa sababu najua undani wa sakat la Membe na Mafisadi.
 
Kitendawili ninakiona kwenye umri. Yeye na Lowasa ifikapo 2015 watakuwa na miaka 62. By CCM standards watakuwa wazee. CCM inataka uwe 'kijana' wa umri wa miaka 57 ili kugombea. JK was 57. So was Mkapa. Will CCM move away from its tradition?
 
GT, umeingia choo cha jinsia tofauti nawe. Wahenga walisema, "UKIVULIWA NGUO NI VIZURI UCHUCHUMAE". Hii thread uliyoileta itakutokea puani kama ile ya Vitambulisho. Umezidi uongo wewe, na hapa sio sehemu ya kutuletea stori za kufunga kanga au kutunga ushanga.
 
Marigawe, ni lini ulimsikia Membe amesema kuwa nataka kugombea Urais mwaka 2010?
 
Mzee Mwanakijiji, napenda kukuhakikishia kuwa kama hadithi za kunoga ktk Mkoa wa Lindi basi tuzitegemee ktk majimbo mengine lakini sio la Membe. Huyu mtu amefanya mengi saaaaana kwa wananchi wa jimbo lake. Sidhani kama wananchi wale watakuwa WASHENZI wa kutomchagua tena kuwa Mbunge wao. Nina imani ni watu waliostaarabika na wana UTU.
 
Maligwe, hivi ni kweli umri ni tishio la usalama wa nchi? Lakini lini ulimsikia Mmembe akisema kuwa atagombea Urais mwaka 2010? Mbona na wewe naona kama unapita alipopita GT? Can u respond to my call please? I want to make this record very clear. Mukome kushabikia uzandiki.
 
GT upo wapi? Nakusubiri wewe tumalizane ili niende kufanya kazi zangu nyingine. Umezidi uongo na kumchukia Membe wewe. Hebu ibuka tumalizane kwanza.
 
GT, ktk thread hii nitakufa nawe. Nasema hivi kwa sababu najua mengi sana, bahati mbaya yale niyajuayo ndio umeyaleta hapa. Wewe sio mkweli wa kuaminiwa. Naenda kudunda mzigo, lakini nakuhitaji ujitokeze, or else nitakuumbua sana, na heshima uliyojijengea ktk JF itapungua kama sio kufa kabisa. Naomba kukuita FISADI mtoto kwa sasa wakati naondoka.
 
Duh!
Tunasubiri round 2. So far 1-0.
 
GT haonekani lakini kasema atamwaga ugali Chechetuka kasema kama GT atamwaga ugali yeye atamwaga mboga yetu macho wakimwaga mimi nitazoa mwishoni kabisa
 
Chechetuka nadhani unaelewa juu ya kuwa kingozi bora, zipo sifa nyingi na katika hizo kiongozi hapaswi kuwa mropokaji na mwenye jazba katika kujibu au kutenda sasa kama hizo mende oh sorry Membe hana tusiziseme? Anyways siwashangai wengine ni makatibu wa wawabunge kule majimboni.....! Kama unaona hasira na jazba hazihatarishi usalama wa nchi me ntakusaidiaje? Jiulize alivyojibu kwa jazba mahojiano nje ya Prado lake alipokuwa akihojiwa na mtangazaji na mtangazaji angeuliza tena kwa jazba, na watazamaji wakawa na jazba kungekalika kweli? Best chanzo cha ukosefu wa amani ni hasira ambazo tunashindwa kuzicontrol. Nilikuwa msituni ila nasisitiza ukweli tutausema tu nyie msemao tukikosoa viongozi wa chama tunakichafua chama hatutakuwa na jinsi. Best ni vijimambo tu ila data tunazo!
 

Mmmh! Chechetua kama hautajali hebu tujuze ndugu yetu hayo mengi saaaaana aliyoyaafanya Membe jimboni kwake.
 
Mmmh! Chechetua kama hautajali hebu tujuze ndugu yetu hayo mengi saaaaana aliyoyaafanya Membe jimboni kwake.
Cheche mpaka sasa sijaona hoja ya msingi uliyoisimamia inayomlinda membe.
 
Nachelea kusema kwamba GT ndiye anayempandisha Membe chati, na kwa moto huu Membe ana nafasi mzuri tu ya kuingia Ikulu kama akigombea.

Wanasema pafukapo moshi
 








Marigawe, ni lini ulimsikia Membe amesema kuwa nataka kugombea Urais mwaka 2010?



GT upo wapi? Nakusubiri wewe tumalizane ili niende kufanya kazi zangu nyingine. Umezidi uongo na kumchukia Membe wewe. Hebu ibuka tumalizane kwanza.





Chechetuka Gegedua
Senior Member
Join Date
28th May 2009
Total Posts
60


duh!
Kaazi kweli kweli!
 
GT

Hivi hizi tuhuma za wewe kwenda kuomba kazi foreign ni za kweli? Inaonekana Checheguta Gegedua anakupata vizuri tuweke sawa hapo ili mjadala uendelee.

Kama uliomba hakuna ubaya wewe ni mbongo na una haki kama mtu yoyote yule kufanya hivyo, na kama ni kweli kwa nini umekuja na hizi tuhuma za Membe? Huoni hapo itakuwa kidogo na mashaka? Mushkeli? Sina wasiwasi na tuhuma ulizotoa kwa jinsi Membe alivyo na mawaziri wengi tu wa Chama Cha Majambazi siku hizi za kuelekea uchaguzi kuwa Mafisi waroho waliopindukia kutaka kupata ubunge nk Shillingi millioni 46 za kiinua mgongo pamoja na millioni 40 za shangingi si haba. Vile vile tunakumbuka mradi wa vitambulisho jinsi alivyo mshiriki kwa njia moja au nyingine.

Tuweke sawa hapa mkuu maana tetesi zinasema Membe atakuwa kule UK hivi karibuni na members wetu wa kule wanaweza kumuwahi kwa maswali kede kede kabla hajarejea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…