Membe: Kikwete siyo kaka yangu

Membe: Kikwete siyo kaka yangu

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
104,319
Reaction score
183,521
Amesema wakati akichukua fomu hapo Dodoma.

Amesema asingeficha kama angezaliwa baba mmoja yeye na Jakaya!
Waziri Bernard Membe Achukua Fomu ya Kuomba Ridhaa ya Kuteuliwa Kugombea Nafasi ya Urais 2015

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe leo June 8, 2015 amechukua fomu za kuomba ridhaa ya kugombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma baada ya kutangaza nia hiyo jana (Jumapili).

Waziri Membe akipokelewa fomu na Mkewe Dorcas mara baada ya kukabidhiwa fomu mjini Dodoma.

Alipokelewa na makada na wafuasi wa chama hicho mjini Dodoma baada ya kukabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Oganaizesheni, Seif Khatib ambapo baada ya kupokea fomu hiyo Membe alisema; "Ninafurahi kukabidhiwa fomu hii na nina hakika kutokana na kujipima na kujiona ninafiti nafasi hii kulinganisha na waombaji wengine ni lazima tubadilishe nchi yetu kuwa nchi ya uchumi wa viwanda."

Chanzo: Michuzi
 
Katika watu walio tia mwaka huu kila nikimuangalia membe Lowasa na Samweli Sitta ni dhahiri utagundundua kuwa moja kati ya ndoto zao tangu wakiwa vijana wamekuwa wanatamani siku moja wangekuja kuwa marais.

Pia ukimwangalia Membe na Lowasa katika kutia nia wamekuwa. Wakiongea. Kwa wasiwasi kama kweli wataweza kutimiza ndoto zao za muda mrefu.

Na pia kila mmoja amekuwa anajitahidi juhudi zake na maarifa kupata ushawishi.

Ila taarifa za uchunguzi kutoka kwa watalamu wa siasa endapo mmoja wao au wote wakaukosa uraisi kuna dalili zozote mmoja wao kupata tatizo la pressure sio siri.

Katika harakati hizi kuna kupata na kuna kukosaa maana ikitokea mtu amekosaa moyoni mwake yupo tayali kukubali matokeo .

Ushauri wangu kwa wagombea wangu unadhani una moyo mwepesi ni bora ukajitoa mapema maana nina wasi wasi wagombea wangu kama huna moyo wa chuma ni bora ujitoee maana kuna dalili ya watu kupinga maamuzi ya kamati kuuu.
 
Heri ya Membe kuliko ma-mvi. Jamaa wa kaskazini ametumia, bado anatumia gharama kubwa kutafuta kuwa mpangaji magogoni,jumba namba moja nchini. Nini chanzo cha hizo pesa,nini lengo lake,atarudishaje hizo gharama. Kama CCM hawana mwingine zaidi yake, watakuwa wameshindwa asubuhi. Mr white hair hasafishiki
 
Mkuu hasafishiki kwa kivip, maana hana tuhuma wala hatujaona akiburuzwa mahakamani, au wewe una ushahidi kidogo utueleze na wana JF tuelewe.
 
Fedha za Ghadaffi zinamzuzua tu " JK amenipa Ubunge, Amenipa Uwaziri" mtamfanya nini? Membe amepanic sasa.
Amesema wakati akichukua fomu hapo Dodomd. Amesema asingeficha kama angezaliwa baba mmoja yeye na Jakaya!
 
Heri ya Membe kuliko ma-mvi. Jamaa wa kaskazini ametumia, bado anatumia gharama kubwa kutafuta kuwa mpangaji magogoni,jumba namba moja nchini. Nini chanzo cha hizo pesa,nini lengo lake,atarudishaje hizo gharama. Kama CCM hawana mwingine zaidi yake, watakuwa wameshindwa asubuhi. Mr white hair hasafishiki
Ma Presdent is Lowassa God bless Him
 
Unaonekana uko allergic na kaskazini. Fanya Uchunguzi Zaidi ujue nani katumi Zaidi. Membe ameliw a fedha zake na wapiga Ramli.
Heri ya Membe kuliko ma-mvi. Jamaa wa kaskazini ametumia, bado anatumia gharama kubwa kutafuta kuwa mpangaji magogoni,jumba namba moja nchini. Nini chanzo cha hizo pesa,nini lengo lake,atarudishaje hizo gharama. Kama CCM hawana mwingine zaidi yake, watakuwa wameshindwa asubuhi. Mr white hair hasafishiki
 
Huyu BM naye kawakusanya watu kibao wahudhurie mkutano wake. Rushwa tupu CCM
 
Heri ya Membe kuliko ma-mvi. Jamaa wa kaskazini ametumia, bado anatumia gharama kubwa kutafuta kuwa mpangaji magogoni,jumba namba moja nchini. Nini chanzo cha hizo pesa,nini lengo lake,atarudishaje hizo gharama. Kama CCM hawana mwingine zaidi yake, watakuwa wameshindwa asubuhi. Mr white hair hasafishiki

CCM MAGUFULI ndo mtu pekee mwenywe uwezo wakuwanadi wabunge wenu kwenye majukwa ja siasa na watu wakakubali vinginevyo mtatengeneza serikali ya mseto,najua urais mtapata lkn wabunge,jipange fanya maamuzi ya tija.
 
Ma Presdent is Lowassa God bless Him

Lowassa hafai hata chembe. Fisadi,raghai, afya mgogoro. Kinachompa moyo ni ushauri wa TV Joshua kuwa atashida kwa masharti ya kutoa misada misikitini na makanisani. Kweli kiongozi wa nchi anaendelea kuomba uongozi kwa watu wanaotumia nguvu za giza kuwa tawatapeli watu? Naomba Kamati kuu, huyu maumvi hatufai, mpigeni chini bila kumuonea haya.
 
Sure....ingawa nayatafuta mabadiliko nje ya ccm
 
Awe kaka yake,asiwe hatukutaki.alishakuharibia riz na mama yake as if wao wana akili kuliko wa tz milion 44.
 
We Bato hilo neno "wa kaskazini" ulilotumia ni la kibaguzi. Unabagua kikanda. Na wengine wakisema hawataki "mswahili" si na wengine hawatafurahi? Tusibaguane. Tupime hoja !!.
 
Amesema wakati akichukua fomu hapo Dodomd. Amesema asingeficha kama angezaliwa baba mmoja yeye na Jakaya!

Wakapime DNA na jk tujue ukweli!
Maana lisemwalo lipo!!!

Au tukubali kutawaliwa na ukoo wa jk!!!!!!?
 
Heri ya Membe kuliko ma-mvi. Jamaa wa kaskazini ametumia, bado anatumia gharama kubwa kutafuta kuwa mpangaji magogoni,jumba namba moja nchini. Nini chanzo cha hizo pesa,nini lengo lake,atarudishaje hizo gharama. Kama CCM hawana mwingine zaidi yake, watakuwa wameshindwa asubuhi. Mr white hair hasafishiki

Watu wote wanatumia hela,vinginevyo huelewi unachosema!
 
Back
Top Bottom