Membe jiandae kisaikolojia

Membe jiandae kisaikolojia

thetallest

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2017
Posts
8,271
Reaction score
9,114
Siasa ni mchezo mchafu sana ,mara nyingi mwenye nguvu hua ni yule mwenye dola,especially nchi za kiafrika.

Ndio maana wale wajanja ambao hujua wamepora wakiwa kwenye madaraka muda ukiisha hukaa kimya kujilia vyao taratibu.

Sasa naona umechokoza mzinga wa nyuki kumbuka ulikua kwenye system unataka kupambana na system,ambayo inakujua kindakindaki ABC zako.kukumaliza ni jambo dogo sana.

1-Imetajwa dola million ishirini (20)za Gaddafi ,unatakiwa utoe maelezo ya kutosha.

2-kutamalaki kwa dawa za kulevya awamu yako.

3-utakatishaji fedha uliokithiri awmu yako.

4-ugonvi wa Tanzania na malawi/ Tanzania na Rwanda ukiwa waziri wa mambo ya nje uhusiano ulikua mbaya.

5-ulileta makampuni mengi ya kitapeli ambayo mengi yalikua hayalipi kodi,ikiwemo kuuza kipande cha ardhi Bagamoyo kwa wageni pia kuikabidhi gas ya mtwara na Lindi kwa mkataba wa kinyonyaji. hapa nakumbuka Simbachawene aliuleta huu mkataba bungeni kwa haraka,ni wabunge 60 tu waliopitisha ,wapinzani kina Lissu walisema serikali ina haraka gani?
,jiandae kupangua hoja ikiwa wewe ndio uliowaleta.
6-una makampuni na mahotel huko Lindi na mtwara ambayo inasemekana yaliongoza kwa ukwepaji kodi,jiandae kupambana na TRA,

Mengi yataibuka na usije shangaa ukapewa kesi ambayo utahangaika nayo sana,itakupa uchovu wa akili na mwili.

Kwakua bado una ndoto za kuwa rais wa nchi hii komaa,ila system huwezi ishinda hata siku moja,hili nawe unajua, na kwa vile wanadamu tumeumbwa na kiburi nakuachia wewe mwenyewe uchague,Lowassa aliliona hilo ,na mwisho wake hua ni stroke ,diabetis au paralasing ukiwa bunkrupcy kabisa.
 
Tunatarajia 'ligi mechi fucho'. Timu membe poleni sana. ,Asante kwa bandiko hili,natumai umewaziba mdomo.
 
Usikurupuke mkuu. Maana sidhani kama yeye kakurupuka kama wewe. Kwahiyo unayoyasema lazima ame consider.

Muacheni atumie haki yake kwa mujibu wa katiba ya chama na ile ya Taifa.

Waacheni wananchi watumie haki zao kikatiba kufanya maamuzi ya nani awaongoze, ama nani wampe ajira.
 
Umemaliza kila Kitu Mkuu na namuonea mno huruma kwani yajayo hayatokuwa yakufurahisha Kwake. Hicho Kipengele chako #4 ndiyo nimekipenda zaidi. Sijajua Membe amejiamini nini wakati Yeye ni Mtu wa ' System ' tena wa ' Senior Level ' kabisa leo hii anakuja kutaka Kutunishiana Misuli na wenye ' System ' hii mpya huku akijua fika ya kwamba ' almost 65% ' ya yale aliyokuwa akiyajua ya ' System ' sasa yamebadilika na hakuna ambacho anakijua sana sana ataishia tu kupewa ' Umbea ' mdogo mdogo na ambao hautokuwa na Tija / Mantiki yoyote Kwake. Amefanya Jaribio baya sana na ambalo asipoangalia litakuja Kumgharimu mno Siku si nyingi.
 
Back
Top Bottom