Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,903
- 945
MHE. HAMIS TABASAM AWAKARIBISHA WANAMWANZA KWENYE SHEREHE ZA MEI MOSI ZITAKAZOFANYIKA SENGEREMA
Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mkoa wa Mwanza, Mhe. Hamis Tabasam amewakaribisha wananchi wa Sengerema na Mwanza kwa ujumla kushiriki maadhimisho ya sherehe za Mei Mosi zitakazofanyika Sengerema.
Mbunge wa Jimbo la Sengerema Hamis Tabasam anawakaribisha wakazi wa wilaya ya Sengerema pamoja na wananchi wa mkoa wa Mwanza kuhudhuria maadhimisho ya sherehe za wafanyakazi Mei mosi mwaka huu, zinatarajiwa kufanyika katika viwanja vya mnadani wilayani Sengerema
Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mhe. Hamis Tabasam ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Mwanza unaongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Malima kwa kupeleka Maadhimisho ya sherehe za wafanyakazi mwaka huu (MEI MOS) kimkoa kufanyika wilayani Sengerema.
Kauli Mbiu ya Mei Mosi 2023: "Mishahara Bora na Ajira za Staha ni Nguzo kwa Maendeleo ya Wafanyakazi" Wakati ni Sasa!
Mwaka 2023 Maadhimisho ya Mei Mosi Kitaifa yatafanyika Mkoa wa Morogoro katika Uwanja wa Jamhuri na Mgeni Rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.