Hata ninyi mmeyafuga. Soma Marko 3. Tatizo mmefundishwa kanisani kutukana badala ya kujifunza. Hebu niambie kanisani kwa nini huwa mnayafukuza mapepo yatoke? Yanakaa humo? Kuhusu suratul Jin kwenye Quran tumeyapa sura au wewe ndio huelewi? Sura inasema kundi moja la majini liliisikia Quran inasomwa yakasema hakika Quran hii ni ajabu tuaamini imetoka kwa mwenyezi Mungu. Haya hebu niambie tatizo nini hiyo sura? Kama ina tatizo na sura kwenye biblia ya Marko nayo itakuwa na matatizo kama Quran maana humo ndio tunaambiwa majini yalipomwona Yesu yalimkiri kuwa ni mwana wa Mungu. Yaani yaliposema hivyo ndio na binadamu nao wakamwita Yesu mwana wa Mungu baada ya kuyasikia majina yanamwita hivyo. Twende kimaandiko.